Sunday, November 26, 2017

USALAMA BARABARANI WAFANYA OPERESHENI USIKU WAKAMATA MADEREVA


 Kaimu Kamanda wa Kikosi cha Polisi cha Usalama Barabarani Tanzania (RTO) Mkoa wa Pwani Salum Morimori kulia akimhoji moja ya madereva waliokuika sheria za usalama barabarani huko Msata wilayani Bagamoyo katikati ni Edward Gontako kutoka kikosi hicho.

Na John Gagarini, Chalinze

KIKOSI cha Usalama Barabarani kimefanikiwa kuwakamata madereva saba wa mabasi kwa tuhuma za kufanya makosa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuendesha kwa mwendo kasi na kuzidisha abiria.

Madereva hao walikamatwa baada ya kikosi hicho kwa kushirikiana na kamati ya usalama barabarani ya mkoa kufanya oparesheni ya kushtukiza usiku kwenye barabara za Morogoro na ile inayoelekea Mikoa ya Kaskazini.

Akiongoza oparesheni hiyo kaimu kamanda wa kikosi hicho RTO mkoa wa Pwani Salumu Moromori amesema kuwa wameamua kufanya oparesheni hiyo usiku ili kubaini makosa yanayofanywa usiku na hapa anaongea na madereva ambao walikamatwa wakiwemo wa kutoka nchi ya Rwanda.

Kwa upande wake mwenyekiti wa kamati uya usalama barabarani mkoa huo Josephine Protas amesema kuwa wamefanya oparesheni hiyo usiku kufuatia malalamiko.

Naye mkaguzi wa magari wa polisi Edward Gontako amesema kuwa wamekuwa wakiwapa elimu ya kuzingatia sheria za usalama barabarani na usalama wa magari.

MWISHO

No comments:

Post a Comment