Thursday, November 16, 2017

WENGI WAMWAGA ALBERT NGWADA




Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani Anastazia Amas akizungumza wakati wa kuaga mwili wa Albert Ngwada kwenye ofisi za CCM Kibaha Mjini.

 Baadhi ya waombolezaji wakiaga mwili wa Ngwada



 Baadhi ya waombolezaji wakiangua vilo baada ya kuuaga mwili wa Ngwada

Vijana wa CCM wakiwa wamebeba jeneza lililokuwa na mwili wa Ngwada 


 Mama wa Marehemu katikati akiwa anabembelezwa wakati wa kuaga mwili wa mwanae kwenda mkoani Iringa kwa ajaili ya mazishi.
 Katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu akitoa taarifa fupi ya marehemu wakati wa kuaga kwenye ofisi za CCM Kibaha Mjini 
Na John Gagarini, Kibaha

KATIBU wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Pwani Anastazia Amas juzi aliwaongoza wanachama na wananchi wa wilaya ya Kibaha kuaga mwili wa Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM mkoa wa Pwani kuwakilisha Kata ya Pangani Albert Ngwada kwa ajili ya mazishi mkoani Iringa ambaye alifariki dunia Novemba 13 mwaka huu.

Akiongea wakati wa kuaga mwili wa marehemu Ngwada kwenye ofisi za CCM Kibaha Mjini Amas alisema kuwa chama kimepata pigo kutokana na kifo hicho cha mjumbe wa CCM.

Amas alisema kuwa ili kumkumbuka marehemu wanachama wanapaswa kufanya kazi za chama kwa uaminifu na uadilifu ili kuleta maendeleo ndani ya chama na kwa wananchi wa Kibaha kama alivyokuwa Ngwada.

“Natoa pole kwa ndugu na wote walioguswa na msiba huu ambao umewagusa watu wengi na ndiyo maana watu wamejaa hii yote inaonyesha jinsi gani mlivyokuwa mnamkubali kutokana na utendaji wake kikubwa ni kuenzi utendaji wake,” alisema Amas.  

Awali akitoa maelezo mafupi juu ya marehemu katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu alisema kuwa kutokana na utendaji wake kazi mzuri marehemu alipandishwa cheo kutoka Katibu msadizi wa kata ya Pangani na kuwa kaimu katibu msaidizi wa CCM Kibaha Mjini mwaka 2015

Mdimu alisema kuwa marehemu alitumikia nafasi hiyo kama msiadizi wake hadi mwaka 2017 baada ya kuletwa katibu msaidizi toka Magu ambapo Aprili alichaguliwa kuwa mjumbe wa mkutano mkuu wa mkoa toka kata ya Pangani nafasi aliyokuwa nayo hadi anafariki dunia.

Awali marehemu alianza kukitumikia chama mwaka 2007 hadi mwaka 2012 alipochaguliwa kuwa katibu kata Pangani hadi 2017 Juni 2015 alipanda daraja na kuwa Kaimu katibu Msaidizi hadi Aprili 2017.

Alisema kuwa mwaka huu mwezi Mei alichaguliwa kuwa Mjumbe wa mkutano mkuu wa mkoa kupitia kata ya Pangani  na tarehe 4 Oktoba alipata ajali ya Pikipiki huko eneo la Kidimu majira ya saa 1:30 usiku na kupelekwa Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Pwani ya Tumbi na baadaye alihamishiwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.

Aidha marehemu alifariki dunia wakati akiendelea na kliniki baada ya kutolewa Hospitali na alitarajiwa kuzikwa jana kwao mkoani Iringa na alizaliwa mwaka 1982.

Mwisho.
















No comments:

Post a Comment