Friday, December 29, 2017

RC NDIKILO AIPIGA TAFU KILUVYA UNITED MILIONI MBILI

 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo

 Baadhi ya wachezaji wa Kiluvya United inayoshiriki ligi daraja la kwanza wakimskiliza mkuu wa mkoa wa Pwani hayupo pichani walipomtembelea ofisini kwake mjini Kibaha

 Mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo akimkabidhi kiongozi wa timu ya Kiluvya United kiasi cha shilingi milioni 2 kwa ajili ya kuihamaisha iweze kushinda michezo yake na kuingia Ligi Kuu ya Voda Com

 Nahodha wa Timu ya Kiluvya United ya mkoani Pwani Ramadhan akishukuru baada ya kukabidhiwa fedha kwa ajili ya hamasa na mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo.






Na John Gagarini, Kibaha
KUELEKEA mchezo wake wa ligi daraja la Kwanza leo dhidi ya Ruvu kuwania kupanda Ligi Kuu unaotarajiwa kuchezwa  kwenye uwanja wa Filbert Bayi wilayani Kibaha mkoa wa Pwani umeipatia timu ya Kiluvya United kiasi cha shilingi milioni mbili kwa ajili ya hamasa ili waweze kushinda mchezo huo.
Akizungumza wakati wa kukabidhi fedha hizo kwa viongozi wa timu hiyo walioambatana na wachezaji ofisini kwake mjini Kibaha mkuu wa mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo alisema kuwa lengo ni kuhakikisha wanashinda mchezo huo. 
Ndikilo alisema kuwa viongozi wa timu hiyo walifika ofisini kwake na kuomba msaada wa kuisaidia timu yao ili iweze kufanya vizuri kwenye michezo yake mitano iliyosalia ya ligi hiyo na endapo watashinda watafanikiwa kupanda Ligi Kuu ya Voda Com.
“Tuko pamoja na timu yetu ambayo inawakilisha mkoa na leo tunawakabidhi fedha ambazo zimetolewa na wadau wa mkoa ili kufanikisha malengo ya kupanda Ligi Kuu kwani uwezekano huo upo,” alisema Ndikilo.
Alisema kuwa wadau wanachotaka ni timu yao kushinda kwani imeonyesha ina uwezo wa kufanya hivyo kutokana na uwezo inaounyesha wanaamini inaweza kufanya vizuri na kujiweka kwenye nafasi nzuri ya harakati zake za kiutaka kupanda daraja ili kufikia Ligi Kuu ya Voda Com.
“Wadau wa soka wa mkoa wa Pwani wamejitolea fedha hizo kama hamasa ya kufanya vyema kwenye mchezo wa leo ambao utakuwa na ushindani mkubwa kwani timu hizo ziko kwenye nafasi nzuri ya kupanda Ligi Kuu ambapo Ruvu ndiyo kinara wa kundi hilo na United wakiwa kwenye nafasi ya tatu,” alisema Ndikilo.
Aidha alisema kuwa mdau ambaye anataka kuipeleka timu ya Kiluvya United nchi ya Ulaya ya Finland atafurahi kuona timu hiyo inashinda mchezo huo na kutoa zawadi ya mwaka mpya kwa wadau wa mkoa wa Pwani.
Naye nahodha wa timu hiyo Ramadhan Ally alisema kuwa wao wkao tayari kwa pambano hilo na watahakikisha wanapambana kwa nguvu zote ili wapate ushindi na kujiweka vizuri kwenye harakati zao za kupanda daraja.
Ally alisema kuwa kutokana na kupewa fedha hizo zitawasaidia kama morali kwao kwa ajili ya kupata ushindi huo ambao utakuwa muhimu ili kuwapa raha watu wa mkoa wa Pwani.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment