Thursday, June 23, 2016

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho

KITONGOJI CHA MWEMBEBARAZA KUPATA MAJI KARIBUNI


Na John Gagarini, Kibaha

WAKAZI 200 wa Kitongoji cha Mwembebaraza kwenye mamlaka ya Mji  Mdogo wa Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani wanatarajia kuanza kupata maji ya bomba mwanzoni  mwa mwezi Julai mwaka huu baada ya mradi wa maji ya mkopo kutoka Mamlaka ya Maji Safi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASCO) wilaya ya Kibaha kukamilika.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisni kwake meneja wa Dawasco wilaya ya Kibaha Erasto Emanuel alisema kuwa katika kuhakikisha wanatatua changamoto ya maji walikaa na uongozi wa Kitongoji hicho na kuwataka wananchi kuchimba mitaro kwa ajili ya kupitisha mabomba yatakayopitisha maji imeshakamilika.

Emanuel alisema kuwa mitaro hiyo ilikamilika muda mrefu lakini kulikuwa na tatizo ambalo hata hivyo walishalifanyia kazi na tayari wameshawapeka wataalamu kwa ajili ya kupima na zoezi la upimaji limekamilika wanchosubiri ni taarifa toka kwa wataalamu hao ili waanze kuyatandaza mabomba hayo.

“Maji haya ni ya mkopo ambapo mwananchi hatochangia chochote ila atalipa ndani ya miezi 12 huku akiwa analipa na bili za kila mwezi na tunatarajia hadi mwanzoni mwa mwezi Julai maji yataanza kutoka hivyo wasiwe na wasiwasi,” alisema Emanuel.

Awali wananchi hao walitoa malalamiko yao kwa meneja huyo kuwa licha ya kuambiwa wachimbe mitaro kwa ajili ya kupatiwa maji kwa kipindi cha zaidi ya miezi miwli iliyopita bila ya kupelekewa huduma hiyo ya maji.

Wakizungumza na waandishi wa habari wananchi hao wakiongozwa na Tausi Said, Mwantumu Salmin, Juma Salum na Abdala Ally walisema kuwa kutokana na tatizo la maji katika kitongoji hicho waliambiwa wachimbe mitaro hiyo kwa ajili ya kupelekewa maji ya mkopo toka Dawasco.

Walisema kuwa waliahidiwa kuwa mara watakapokamilisha zoezi hilo watapelekewa mabomba kwa ajili ya kupata maji kupitia mradi wa maji ya mkopo ambayo waliambiwa ndani ya mwezi mmoja watakuwa wamepelekewa huduma hiyo lakini mwezi unaisha hakuna kinachoendelea hadi sasa.

“Kinachotushangaza ni kwamba Kitongoji jirani cha Disunyala ambacho kiko mbele yao kimepata maji huku wao wakiwa wamerukwa na wenzao kupelekewa maji licha ya kuwa mfereji uliochimbwa ni mmoja ambapo kila kaya ilichimba mfereji huo ambao umeunganishwa kwenye vitongoji hivyo kwani ulikuwa kwenye mradi mmoja,” walisema wakazi hao.

Mwisho

Monday, June 20, 2016

MWENYEKITI WA MTAA AWAZAWADIA WANAFUNZI WALIOFANYA VIZURI

Na John Gagarini, Kibaha

MTAA wa Zegereni wilayani Kibaha mkoani Pwani umewapa zawadi mbalimbali wanafunzi wa darasa la saba waliofanya vizuri kwenye mitihani yao ya katikati ya muhula.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati wa kukabidhi zawadi hizo kwa wanafunzi hao Rashid Likunja alisema kuwa ameweka utartibu huo kwa wanafunzi wa darasa la saba ili kuwapa hamasa ya kufanya vizuri kwenye mtihani wa kumaliza darasa la saba.

Likunja alisema kuwa zawadi anazotoa ni mfuko wake aliouanzisha kwa ajili ya kuwapa hamasa ya wanafunzi wa mtaa huo kusoma kwa bidii na kuongeza ufaulu.

“Unajua mtaa huu hakuna shule ya msingi ambapo wanafunzi huwabidi kwenda kusoma mtaa jirani wa Visiga ambapo wengine wanatembea kilometa nane kila siku hivyo kuwakatisha tamaa watoto hivyo kutotilia makazo elimu,” alisema Likunja.
Aidha alisema kuwa kabla ya kuanza utaratibu huo wanafunzi wa mtaa huo walikuwa wakishika nafasi za nyuma kuanzia 35 na kushuka chini lakini a kwa sasa wameanza kuhamasika na wameweza kuingia kwenye 10 zaidi ya wanafunzi watano.

“Nimeanzisha mfuko wa kuwasaidia wanafunzi wa mtaa wetu naomba na wadau wengine wajitokeze kusaidia ili zawadi ziwe kubwa kwani nianazotoa ni ndogo lakini naamini wadau zaidi watajitokeza kuniunga mkono juu ya suala la elimu ambalo nimelipa kipaumbele cha kwanza,” alisema Likunja.

Moja ya wazazi ambao mwanae kapewa zawadi baada ya kuwa moja ya wanafunzi walioingia kwenye 10 bora Mwajabu Suleiman alisema kuwa mwenyekiti wao amewapa changamoto kubwa ya kuwahamasisha wanafunzi kusoma kwa bidii.

Suleiman alisema kuwa watamuunga mkono mwenyekiti wao kwa kuwahamasisha watoto wao kusoma kwa bidii ili wawe chachu ya wanafunzi wenzao wanaoanza madarasa ya awali.


Mwisho.    

SIDO YATUMIA DOLA MILIONI 2

Na John Gagarini, Kibaha

SHIRIKA la Kuendeleza  Viwanda Vidogo Vidogo (SIDO) kwa kushirikiana na wafadhili wake limetumia kiasi cha dola milioni mbili za Kimarekani kwa ajili ya kutoa mafunzo ya uzalishaji bidha za vyakula zisizo na madhara kwa wajasiriamali zaidi ya 700.

Mratibu wa mafunzo hayo Happines Mchomvu alisema kuwa mafunzo hayo ambayo yametolewa kwa kipindi cha miaka miwili kwa lengo la kuhakikisha bidhaa wanazozalisha zinakuwa hazina madhara kwa watumiaji zinakuwa na usalama.

Mchomvu alisema kuwa mbali ya kuwa na usalama pia zinakuwa na viwango vya wa ubora wa kimataifa ili viweze kuuzwa sehemu yoyote ile duniani.

“Mafunzo hayo yalikuwa na malengo ya kuboresha bidhaa za maembe, viungo na asali ambapo wameweza kuwajengea uwezo wajasiriamali hao kutoka mikoa ya Tabora, Singida, Shinyanga, Morogoro, Pwani na Dar es Salaam,” alisema Mchomvu.

Aidha alisema lengo ni kuhakikisha wajasiriamali kote nchini kuanzia ngazi ya mikoa hadi kwenye mitaa wanazalisha bidhaa zenye ubora na viwango kwa lengo la kuwa na soko la uhakikka la ndani na nje ya nchi ambapo bidhaa za Tanzania zinapendwa kutokana na uhalisia wake.

Kwa upande wake ofisa udhibiti wa ubora kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Magdalena Sademaki alisema kuwa kupitia mafunzo hayo wajasiriamali hao wameweza kutengeneza mifumo yao kimataifa kwa kupambana na vihatarishi ili visiweze kuingia kwenye vyakula.
Sademaki alisema kuwa katika kuhakikisha wajasiriamali hao wanatengeneza bidhaa zenye viwango wanashirikiana na SIDO kuwatambua ili waweze kufikia viwango vya uzalishaji wa bidhaa bora ili ziendane na viwango vya kimataifa.

Na mmoja wa wajasiriamli ambaye amehudhuria mafunzo hayo Zaloki Mohamed ameishukuru SIDO kwa kuwapatia elimu juu ya viwango vya bidhaa  wanazozalisha kwa kuzingatia  utaratibu wa viwango vya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Viwango Tanzania (TBS) na Shirika la Viwango la Kimataifa (ISO).

Mohamed  ameiomba serikali iwapunguzie tozo zinazotozwa kwa wajasiriamali ili wapate hati ya viwango ya bidhaa wanazozalisha na kuweza kufikia malengo  ya Tanzania ya kuwa na viwanda.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ufadhili wa Shirika la Biashara la Kimataifa (ITC) kupitia mpango wa kuendesha biashara wa shirika la World Trade Organisation (WTO) kwa kushirikiana na SIDO.

Mwisho. 





 

   




Saturday, June 18, 2016

WAVUNJUA VIOO VYA MADIRISHA WAPAKA KINYESI OFISI YA KATA

BOMOABOMOA YALIZA WENGI KIBAHA

MIGOGORO YA NDOA ISIWANYIME HAKI ZA MSINGI WATOTO