Thursday, May 26, 2016

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

MWENYEKITI AKATALIWA KWENYE MKUTANO

Na John Gagarini, Kibaha
SAKATA la Mwenyekiti wa Mtaa wa Muheza wilayani Kibaha mkoani Pwani Maulid Kipilili limechukua sura mpya baada ya wananchi wa mtaa huo kumkataa mwenyekiti huyo kwenye mkutano wa wananchi uliofanyika mtaani hapo.
Wananchi hao walimkataa mwenyekiti wao wakati wa mkutano ulioitishwa na diwani wa kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi ili kujadilia suala la malalamiko ya wananchi wa mtaa huo baada ya kuifunga ofisi ya mtaa hadi pale watakapofikia muafaka juu ya mwenyekiti wao.
Mkutano huo ambao ulifanyika mtaani hapo chini ya diwani huyo wa kata na ofisa Mtendaji wa Kata hiyo Thadeo Mtae wananchi hao walilalamika kuwa mwenyekiti wao tangu achaguliwe kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwishoni mwa mwaka 2015 hajaitisha mkutano wa wananchi.
Kabla ya kufikia hatua ya kumkataa mwenyekiti wao wananchi hao walitoa malalamiko yao mbalimbali ikiwa ni pamoja na kulalamika kuwa mwenyekiti wao haitishi vikao vya wananchi, hasomi mapato na matumizi, kutofungua ofisi hivyo kuwapa shida wananchi wanapokwenda kupata huduma za kiofisi.
Akizungumza juu ya mwenyekiti wao kushindwa kuwajibika mwananchi wa mtaa huo Kitai Mganga alisema kuwa ni pamoja na tuhuma nyingine ni kushindwa kusimamia mali za mtaa ikiwa ni pamoja na baadhi ya watu kumega na kuuziana eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi lakini hakuna hatua zozote ambazo amezichukuwa.
“Mtaa wetu una changamoto nyingi ikiwa ni pamoja na ukosefu wa maji, umeme, Shule ya Msingi, bararabara na zahanati lakini kutokana na mwenyekiti wetu kutowajibika tumeshindwa kufanya lolote hata kuweka mikakati ya maenedeleo hakuna,” alisema Mganga.
Naye Paulo Chacha alisema kuwa mwenyekiti lazima awe na wajumbe wa mtaa lakini cha kushangaza wajumbe hawapo hivyo mwenyekiti anafanya kazi peke yake jambo ambalo haliwezi kuleta mafanikio.
Chacha alisema kuwa kamati ya mtaa ni sawa na baraza la mawaziri sasa haiwezekani Rais kuongoza nchi bila ya kuwa na Mawaziri kwani maendeleo hayawezi kupatikana.
Kwa upande wake Maulid Kipilili alisema kuwa kwa upande wa mikutano alishindwa kufanya kutokana na sababu maalumu ikiwa ni pamoja na shughuli za kitaifa.
Kipilili alisema kuwa aliitisha mikutano mitatu ya dharura na miwili ya kikatiba na kuwashangaa wananchi hao kumsingizia kuwa hajafanya kabisa mikutano na mmoja wa Mei 15 ulishindwa kufanyika kutokana na akidi kushindwa kuenea.
“Kuhusu wajumbe wa serikali ya mtaa hawajafika kwa sababu mbalimbali lakini wapo na sina mgogoro na wajumbe wangu na tunafanya kazi vizuri na baadhi ya kamati zipo na zinafanya kazi kama ya maji na shule zipo na aliyeuziwa eneo la shule kama kuna mtu anaushahidi alete ili tuchukue hatua za kisheria,” alisema Kipilili.
Akielezea juu ya changamoto hiyo ya wananchi kumkataa mwenyekiti wao diwani wa kata hiyo Ramadhan Lutambi alisema kuwa kama hawamtaki wanapaswa kufuata taratibu kwani hatua ya kwanza ni hiyo.
Lutambi alisema kuwa kutokana na hali hiyo itabidi uitishwe mkutano wa dharura wa kata kujadili suala hilo na wao ndiyo watakaoamua hatma ya mweneyekiti wao.
Kufuatia kukataliwa na wananchi ofisa mtendaji wa kata ya Maili Moja Thadeo Mtae alisema kuwa hoja zilizotolewa ni 15 ambapo zimejibiwa na mwenyekiti huyo ambapo baadhi wamekataa majibu yake na nyingine wamekubali majibu.
Mtae alisema kuwa atapeleka sehemu husika kwa ajili ya majibu na hatua zaidi kwani yeye hatoweza kutoa majibu hivyo wasubiri majibu ambapo kutaitishwa mkutano mwingine.   

Mwisho.   

Monday, May 23, 2016

KIBAHA YAKAMATA KILOGRAMU 441 ZA DAWA ZA KULEVYA

Na John Gagarini, Kibaha

WILAYA ya Kibaha mkoani Pwani imefanikiwa kukamata madawa ya kulevya yenye uzito wa kilogramu 441.6 katika kipindi cha mwaka 2015 / 2016.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha ambaye pia ni wenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya amesema kuwa katika mapambano dhidi ya madawa ya kulevya kipindi cha mwaka 2015/ 2016 wamefanikiwa kukamata dawa zenye uzito wa kilogramu 441.65.

Kihemba amesema kuwa kati ya hizo Cocain na Heroin ni kilo 6.1, Bhangi kilo 418,mirungi kilo 17.5 ambapo jumla ya kesi 153 zimefunguliwa kwenye kituo cha Polisi cha wilaya ya Kibaha.

Amesema kuwa kesi zilizopelekwa mahakamani ni 132 na zilizo kwenye upelelezi ni 21 ambapo kesi za Bhangi na Mirungi zilizo kwisha mahakamani ni 57. 

aidha amesema kuwa jumla ya watuhumiwa ambao walikamatwa na bangi na mirungi ni 163 wanawake wakiwa ni 28 na wanaume ni 135 na wilaya inaendelea kutoa elimu ili watu waepukane na dawa za kulevya.


Mwisho.       

MABILIONI YATENGWA SEKTA YA ELIMU KIBAHA

Na John Gagarini, Kibaha
KATIKA kukabiliana na changamoto za elimu  wilaya ya  Kibaha mkoani Pwani imetenga bajeti ya shilingi bilioni 1,789,828,891 kwa ajili ya miradi ya maendeleo kwa shule za sekondari kwa mwaka wa fedha wa 2016/2017.
Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba na kusema kuwa fedha hizo ni kwa ajili ya kupunguza changamoto mbalimbali kwenye shule za sekondari wilayani humo.
Kihemba amesema kuwa kabla ya bajeti hiyo kupitishwa jumlaya shilingi milioni 640,424,679 zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika shule za sekondari za Zogowale na Hosteli ya shule ya sekondari ya Pangani.
Amesema kuwa pia fedha hizo zimetumika katika ujenzi wa matundu 20 ya vyoo, madarasa matano na nyumba moja ya mwalimu katika shule za sekondari za Pangani, Simbani na Ruvu Station.
Akizungumzia upande wa shule za msingi amesema kuwa katika bajeti hiyo zimetengwa kiasi cha shilingi milioni 943,144,394 kwa ajili ya miradi ya maendeleo  kwa elimu ya msingi.
Aidha amesema kuwa katika bajeti ya mwaka wa fedha ya 2015/ 2016 wilaya ilipokea kiasi cha shilingi milioni 140,254, 154 kwa ajili ya ujenzi wa ofisi ya mwalimu Kumba, vyumba 9 vya vya madarasa katika shule za Visiga, Lumumba, Bamba na Matuga.
Amebainisha kuwa fedha hizo pia zimetumika kwa ajili ya ujenzi wa matundu ya vyoo na ununuzi wa madawati 46, meza 4 na viti 6 kwa ajili ya shule ya Msingi ya Matuga.

VIONGOZI SIMBA WAWAJIBIKE


Na John Gagarini, Kibaha

UONGOZI wa Timu ya Soka ya Simba ya Jijini Dar es Salaam wametakiwa kuwajibika kutokana na matokeo mabaya ya timu kwenye mashindano ya Ligi Kuu ya Voda Com iliyomalizika mwishoni mwa wiki.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha msemaji wa Tawi la Simba Kibaha maarufu kama “Simba Tishio” Fahim Lardhi alisema kuwa viongozi hao wamekuwa wakiwawajibisha wachezaji pale wanapofanya vibaya hivyo na wao lazima wawajibike kwa hilo.

Lardhi alisema kuwa timu hiyo imefanya vibaya kwenye misimu minne na kuifanya timu hiyo ishindwe kushiriki michuano ya kimataifa kutokana na matokeo mabaya ambapo kwa msimu huu imeshika nafasi ya tatu.

“Timu ina vitengo vingi na kamati mbalimbali hivyo kama kuna kiongozi ambaye alizembea kwenye kitengo chake na kufanya timu ifanye vibaya kwa kushindwa kutekeleza majukumu yake anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi,” alisema Lardhi.

Alisema kuwa inasikitisha kuona timu inafanya vibaya kila mwaka ambapo kwa mwaka huu mwenendo wake haukuwa mzuri na kufanya timu kupata matokeo mabaya huku ikiwa imetambiwa na mtani wake Yanga kw akufungwa michezo yote.

“Tumechoka kusemwa vibaya na watani wetu hii ni fedheha kwetu tunaomba kiongozi yoyote ambaye alisababisha timu kufanya anapaswa kuwajibika kwa kuachia ngazi au kuondolewa,” alisema Lardhi.

Aidha alisema kuwa anawapongeza wanachama na wapenzi wa timu yao kwa kuwa na uvumilivu kwani kwa kipindi cha miaka minne timu yao imekuwa ikifanya vibaya lakini wametulia wakiamini kuwa timu itapata matokeo mazuri lakini imekuwa kinyume.

“Ligi imeshakwisha kila kiongozi atoe ripoti yake na kuonyesha uzaifu ulikuwa wapi ili kujipanga na msimu mwingine wa ligi ijayo ili timu ifanye vizuri na si kushika nafasi ambazo haiipi timu kushiriki michuano ya kimataifa,” alisema Lardhi.

Aliutaka uongozi kuwa makini katika usajili kwa kusajili wachezaji wenye uwezo na kuacha kusajili wachezaji wasio na uwezo kwani Simba inahitaji wachezaji wenye uwezo na si kila mchezaji anastahili kuichezea Simba kama ilivyokuwa kwa msimu huu kuwa na wachezaji wenye uwezo mdogo.

Mwisho.

VIJANA WAILILIA SERIKALI KUWAINUA KIUCHUMI

Na John Gagarini, Kisarawe

SERIKALI imeombwa kusaidia vikundi vya vijana vinavyopata mafunzo mbalimbali ya kuwainua kiuchumi ili waweze kujiajiri wakiwa Vijijini badala ya kukimbilia Mijini.

Akisoma risala ya wahitimu mbele ya mgeni rasmi ambaye ni kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima kwenye Kijiji cha Kibuta wilayani Kisarawe, Mariam Christopher alisema kuwa mafunzo hayo yatawawezesha kuweza kukabili mazingira wanayoishi huko huko waliko kuliko kukimbilia mjini kutafuta ajira.

Christopher alisema kuwa masomo waliyojifunza ni ya ufundi kwa vijana wa kata ya Kurui kupitia mradi wa kuwajengea uwezo vijana (YEE) unaosimamiwa na shirika lisilokuwa la kiserikali Plan International wilaya ya Kisarawe.

“Tunashukuru wafadhili wetu kwani tumeweza kujifunza mambo mengi ya ufundi tunaamini yatatusaidia tukiwa huku huku bali kikubwa ni Halmashauri kutuwekea mazingira mazuri ya kufanya kazi ili tuisaidie jamii ya Kijijini hasa ikizingatiwa nako kuna hitaji maendeleo,” alisema Christopher.

Alisema kuwa mafunzo hayo wameyapata kwa kina katika fani mbalimbali za upambaji, mapishi, udereva, ushonaji na utengenezaji wa mapambo na wanatarajia kuboresha shughuli hizo Vijijini ili kuleta maendeleo kwa familia zao na wao binafsi.

Aidha alisema kuwa mafunzo hayo yanafadhiliwa na Eu, Vso, Uhiki, Veta na Plan International wilayani humo na yanatekelezwa kwenye kata Sita za Kibuta, Kisarawe, Manerumango, Msimbu, Kurui na Marumbo na yanatarajiwa kuwafikia vijana 1,000 kwa kipindi cha miaka mitatu.

Kwa upande wa kiongozi wa mbio za mwenge Kitaifa George Mbijima alisema kuwa Halmashauri inapaswa kuwatengenea vijana asilimia tano ya mapato yao kwa ajili ya kuwakopesha vijana kwani suala hilo liko kisheria na wanapaswa kutekeleza ili kuwajenga vijana kiuchumi, Mwenge huo leo unatarajiwa kukimbizwa wilaya ya Rufiji.

Mwisho. 





SERIKALI KUWAWEKEA MAZINGIRA MAZURI WAWEKEZAJI

Na John Gagarini, Kisarawe
SERIKALI itaendelea kuweka mazingira mazuri kwa wawekezaji wa ndani na nje ambao watafuata taratibu za nchi ili kuongeza pato la taifa kupitia sekta ya uwekezaji ambayo kwa sasa inakuwa kwa kasi kwenye mikoa mbalimbali.
Hayo yalisemwa na kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa George Mbijima alipokuwa akiweka jiwe la msingi kwenye Bandari ya Nchi Kavu inayojengwa kwenye Kijiji cha Kazimzumbwi wilayani Kisarawe mkoani Pwani.
Mbijima alisema kuwa nchi kwa sasa iko kwenye kipindi cha utekelezaji  kwa vitendo sera ya uwekezaji ili iweze kuleta manufaa kwa wananchi pamoja na serikali ili iweze kuwaletea maendeleo wananchi kupitia uwekezaji.
“Serikali inathamini mchango wa wawekezaji kwani wana nafasi kubwa ya kuleta maendeleo kwa wananchi pamoja na nchi lakini kikubwa ni kuwa wazi wakati wa kufanya taratibu za uwekezaji ili kuondoa malumbano yanayojitokeza baina ya wananchi na wawekezaji,” alisema Mbijima.
Alisema kuwa baadhi ya wawekezaji wamekuwa wakikiuka taratibu za uwekezaji kwa kutokuwa wazi wakati wakufanya michakato ya uwekezaji kwani wanapaswa kuwa wazi kwa pande zinazohusika ili kuondoa mikanganyiko.
“”Wawekezaji wanapaswa kufuata sheria za nchi zilizowekwa ili faida inayopatikana iweze kuleta manufaa kwa wananchi wanaozunguka maeneo ya uwekezaji hivyo wanapaswa kushirikiana na wananchi ili kuondoa migogoro isiyo na tija kwa uwekezaji”,  alisema Mbijima.
Aidha alisema kuwa serikali inatoa ushirikiano na wawekezaji kwnai mbali ya kutoa ajira kwa wananchi pia serikali inapata mapato yake kupitia sekta hiyo ili iweze kuendesha shughuli zake kupitia kodi na ushuru mbalimbali.
Kwa upande wake mkurugenzi wa Kampuni ya DSM Corridor Group  Sada Shaban alisema kuwa ujenzi huo wa Bandari kavu ulianza 2013 na kukamilika mwaka huu kwa baadhi ya vitengo ukiwa umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 7.5 ambapo gharama iliyobakia ni kiasi cha shilingi bilioni 38 hadi kukamilika kwake.
Shaban alisema kuwa eneo hilo litakuwa ni hifadhi ya bidhaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na maghala ya mazao mbalimbali, madini na mizigo ya kila aina na itasaidia kupunguza msongamano barabarani kwani ikitoka hapo inapakizwa kwenye treni ambayo iko jirani na bandari hiyo. Mwenge huo ukiwa wilayani Kisarawe ulizindua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi yenye thamani ya shilingi bilioni 6.5 leo mwenge unakimbizwa wilayani Rufiji.
Mwisho.