Nimeshiriki kikao cha Baraza la Madiwani Cha Chama Cha Mapinduzi kuchagua diwani atakayegombea nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze kilichofanyika Chalinze ,mapema leo.#KaziInaendelea
Saturday, July 27, 2024
TAKUKURU DODOMA YATOA ELIMU KUELEKEA UCHAGUZI WA MITAA MWAKA HUU
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Dodoma imeendelea kutoa elimu kwa Umma kupitia makundi mbalimbali kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini unaotarajia kufanyika mwaka huu.
Naibu Mkuu wa TAKUKURU Mkoani Dodoma Euginius Hazinamwisho amesema kuwa viongozi wa Kisiasa nchini Tanzania hupatikana kupitia uchaguzi unaofanyika kila baada ya miaka mitano kwa namna mbili uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani na uchaguzi wa viongozi wa Mamlaka za Serikali za Mitaa.
"Mwaka 2024 utafanyika uchaguzi wa Serikali za Mitaa na mwaka 2025 utafanyika uchaguzi wa Serikali kuu,"amesema.
Aidha amesema kuwa kuwepo kwa vitendo vya Rushwa wakati wa kuchagua viongozi huwanyima haki wagombea na kuwakosesha maendeleo wananchi
"Jitihada za Serikali kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru na wa haki kwa wananchi wameweza kutunga Sheria mbalimbali zinazodhibiti vitendo vya Rushwa,"amesema
"TAKUKURU kwa kuzingatia kifungu cha 4 kifungu kidogo cha 2 na kifungu cha 7(d) vya Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa vina wajibu wa kuwahakikishia wadau kuweka mikakati dhidi ya Rushwa wakati wa uchaguzi.
Hata hivyo amesema kuwa katika utekelezaji wa majukumu yake TAKUKURU mwaka 2014 na mwaka 2019 ilifanya uchambuzi wa ufuatiliaji wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na mwaka 2020 ilifanya uchambuzi wa mfumo kwa uendeshaji wa uchaguzii mkuu wa Serikali wa Rais, Wabunge na Madiwani katika majimbo yote ya Uchaguzi Tanzania bara.
"Katika chaguzi zote yalikuwepo malalamiko ya vitendo vya Rushwa,katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mwaka 2014/2019 vitendo vya Rushwa vilijitokeza kama ifuatavyo kulikuwa na ugawaji wa fedha, ugawaji wa vitu, kama kanga,fulana,vinywaji na vyakula na ahadi za ajira,"amesema
Kwa upande wake Kamishna Msaidizi wa Mamlaka ya kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Mzee Kasuwi amesema kuwa athari za biashara ya Dawa za Kulevya kwenye uchaguzi wa Kisiasa zinaweza kuwa na madhara makubwa na kuathiri mchakato wa Kidemokrasia na utulivu wa jamii.
Aidha biashara na matumizi ya Dawa za Kulevya ni tatizo linaloathiri nchi nyingi dunia.
"Dawa za Kulevya zina athari Kiuchumi,kiafya, kijamii, Kisiasa, kidiplomasia, Kimazingira na usalama,"amesema
PWANI YAPATIWA WAUGUZI 120
MKOA wa Pwani umepatiwa jumla ya Wauguzi 120 ikiwa ni asilimia 50 ya watumishi walioletwa mkoani humo pia umepatiwa kiasi cha shilingi bilioni 25 kuboresha huduma za afya.
Hayo yamesemwa mjini Kibaha na Katibu Tawala Mipango na Uratibu wa Mkoa wa Pwani Edina Kataraiya ambaye alimwakilisha Naibu Waziri wa Afya Dk Godwin Mollel wakati wa Maadhimisho siku ya Uuguzi Duniani kwa Mkoa wa Pwani.
Kataraiya amesema kuwa serikali imeendelea kutatua changamoto mbalimbali za huduma za afya ikiwa ni pamoja na kuongeza wahudumu wa afya ili kuboresha utoaji huduma.
"Kada ya uuguzi ni uti wa mgongo wa huduma za afya ndiyo sababu serikali inaboresha kwani bila ya wauguzi hakuna huduma hizo hivyo toeni huduma kama kiapo chenu kinavyosema upendo, utu na uadilifu,"amesema Kataraiya.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wauguzi Tanzania (TANNA) Steven Brown amesema kuwa katika Muundo wa Utumishi wa Kada ya Uuguzi na Ukunga ambacho kinamtaka Ofisa Muuguzi kabla hajafikia Kiwango cha mwisho cha Mshahara wake yaani (TGHSG) awe na Masters ambacho ni kikwazo kwa wauguzi.
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kusirye Ukio amesema kuwa huduma wanayotoa wauguzi ni ibada na Hospitali ni madhabahu hivyo waendelee kudumisha ibada zao.
Thursday, July 25, 2024
MFUMO WA KUSAJILI MIGOGORO CMA UTAEPUSHA MALALAMIKO YA UCHELEWESHWAJI HAKI - MHE. MAGANGA
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Katibu Mkuu, Ofisini ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mhe. Mary Maganga amesema mfumo mpya wa kusajili migogoro ya kikazi kwa njia ya mtandao utaepusha malalamiko na ucheleweshwaji wa haki kwa Wananchi ikiwa ni Pamoja na kuongeza ufanisi wa utendaji wa Tume.
Mhe. Maganga ameyasema hayo leo,Julai 24,2024 Jijini Dodoma, wakati akifungua mafunzo maalum ya mfumo wa kusajili migogoro ya kikazi unaofahamika kama ‘Online Case Management’ kwa watumishi wa CMA kutoka Ofisi mbalimbali za mikoa Tanzania.
Vilevile Mhe. Maganga ameongeza kuwa,matumizi ya mifumo yanaongeza ufanisi wa utendaji kwa namna mbalimbali na pia uwezo wa kutumika katika mazingira mbalimbali bila kuhitaji kwenda katika ofisi husika kupata huduma.
"Mara nyingi tukiwa tunataka kuongeza ufanisi pa kwenda ni kwenye mifumo kwasababu mifumo unaweza kuitumia popote pale ulipo na bila kuhitaji kwenda kwa uhalisia kwahiyo tuna imani kubwa itaenda kuongeza ufanisi wa Tume yetu", amesema Mhe. Maganga.
Aidha Mhe. maganga amewataka watumishi kuendelea kusimamia haki katika ajira na kazi kwa kuhakikisha wanatatua migogoro kwa njia ya usuluhishi kwani ndio wajimu wao kwa Tume.
Vilevile ameipoingeza Tume kwa kuendelea kusuluhisha migogoro ya kikazi hadi kufikia asilimia 76% ikiwa ni hatua nzuri kulingana na mpango mpango wa kuhakikisha wanafikia asilimia 81% kwa njia ya Usuluhishina hivyo kuonekana katika hatua inayoridhisha.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) Mhe. Usekelege Mpulla amesema mfumo huu unatarajiwa kutumika kutekeleza lengo la Tume ikiwa ni kuwafikia wadau mbalimbali kwa urahisi popote walipo.
"Kwa msingi huo tunatarajia kupitia mfumo huu tuweze kuwafikia wadau wetu na kusajili migogoro kwa kutumia, simu janja ili nasi tuweze kuishughulikia kwa haraka maana hili ni takwa na ombi la muda mrefu la wadau wetu hasa wawekezaji kutaka huduma za Tume ziende kwa haraka", ameongeza mkurugenzi.
Naye Afisa Mfawidhi kutoka Ofisi ya CMA Arusha, Hermenegilda Stanslaus alisema mfumo huo utawasaidia watumishi wa Tume katika kutekeleza majukumu na kurahisisha utendaji kazi bila kuwalazimu wateja na wadau mbalimbali kufika ofisi za Tume.
WANAOZUSHA UZUSHI WATOTO KUTEKWA KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA
KUFUATIA watu wanne kukamatwa kwa tuhuma za kuzusha uzushi kuwa kuna gari aina ya Noah linateka watoto mkoa huo umetoa onyo kwa watu wanaoleta taharuki hizo kuwa hawatavumiliwa.
RAIS SAMIA SHUJAA TRENI YA MWENDOKASI (SGR)
Tuesday, July 23, 2024
MKUU WA MKOA PWANI AKABIDHI WAKUU WA WILAYA MAGARI
MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amekabidhi magari mawili kwa wakuu wa Wilaya za Kisarawe na Bagamoyo kwa ajili ya urahisishaji utekelezaji wa majukumu yao ya kazi.
Monday, July 22, 2024
UNDERSTANDING THE REASONS BEHIND THE VOLUNTARY RESETTLEMENT OF NGORONGORO RESIDENTS WITHIN THE RESERVE.
*MABULA: NCAA ENDELEENI KUBUNI MAZAO MAPYA YA UTALII NA KUYATANGAZA.*
Na Kassim Nyaki, Ngorongoro.
KAMPENI KUPINGA UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WATU WENYE UALBINO
(ATFT) KWA KUSHIRIKIANA NA HALMASHAURI YA KIBAHA MJI Yaendeleza kampeni yake ya kupinga ukatili dhidi ya watoto na watu wenye mahitaji maalum, kwakutumia michezo na sanaa, kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka (18) na kuendelea, kama njia moja wapo ya kutoa elimu kwa jamii mbalimbali, ATIFITI CUP) Itakayo zinduliwa trh 23/08/2024 ikidhaminiwa vinywaji na kampuni U-FRESH, tarehe 20/07/2024, USHIRIKI WAKO NI MUHIMU KUENEZA ELIMU TAJWA HAPO JUU.
AWESO AAHIDI KUONDOA CHANGAMOTO UKOSEFU MAJI KILUVYA
WAZIRI wa Maji Juma Aweso ameahidi kupeleka wataalamu Kata ya Kiluvya Wilaya ya Kisarawe Mkoani Pwani ili kufanya tathmini ya maeneo yenye changamoto ya maji.
Aweso alitoa ahadi hiyo kwa njia ya simu kwenye mkutano wa hadhara wa Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti uliofanyika eneo la Kiluvya Madukani kutatua changamoto za wananchi.
Alisema atatuma timu yake leo Jumatatu ili wafanye kazi hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi hao wanapata maji na kuondokana na changamoto za ukosefu wa maji.
"Ombi lenu nimelisikia Jumatatu natuma timu itakuja kufanya tathmini kwa yale maeneo ambayo yana changamoto hivyo msiwe na wasiwasi tutatatua shida hiyo,"alisema Aweso.
Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe Petro Magoti alipiga simu ili kuwapatia majibu wananchi waliokuwa wakilalamika kukosa maji kwenye baadhi ya maeneo.
Magoti alisema kuwa wananchi wawe na uvumilivu kidogo kwani serikali inawasikiza na wanafanya kazi kwa kushirikiana na ndiyo sababu amempigia Waziri wa Maji.
Alisema kuwa suala la maji ni jambo muhimu sana hivyo lazima lishughulikiwe kwa uharaka ili kuondoa changamoto ambapo Rais Dk Samia Suluhu Hassan amedhamiria kumtua mama ndoo kichwani.
Kwa upande wake meneja wa DAWASA Emanuel Mbwambo alisema kuwa mpango uliokuwa ni mwezi wa Agosti kuhakikisha baadhi ya maeneo yenye changamoto yanafikiwa na huduma hiyo.
Mbwambo alisema kuwa baadhi ya maeneo ambayo yana changamoto ya ukosefu wa maji kwenye Kata hiyo.
Moja ya wananchi aliyejitambulisha kwa jina la Meri Charles mkazi wa eneo la Makurunge Majumba 6 alisema kuwa maji kwao hawana maji kabisa.
Charles alisema kuwa wao wanakunywa maji ya bwawani huku wanafunzi wakitakiwa kubeba maji lita tano kwa ajili ya matumizi mbalimbali ya shuleni.
Sunday, July 21, 2024
JISAJILI KWENYE KANZI DATA KWA USALAMA WAKO.
Jeshi la Polisi Mkoani Pwani kwa kushirikiana na Maafisa usafirishaji Wilaya ya Kibaha (bodaboda) limezindua zoezi la uvaaji viakisi mwanga katika Wilaya hiyo ili kuwezesha kuwa rasmi na kuepuka kukumbwa na majanga mbalimbali ikiwemo kuporwa vyombo vyao vya moto.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani Kamishina Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Pius Lutumo amewataka maafisa hao kuhakikisha wanajisajili katika kanzi data ili kutambulika wao na vijiwe wanavyofanyia kazi.
Amesema endapo wadau hao watajisajili kati kanzi data na kutii sheria za usalama barabarani ajali zitapungua kwa kiasi kikubwa, matukio ya wizi kwa kutumia Bodaboda yatakwisha na wahalifu wanaojificha kwa mgongo wa bodaboda watadhibitiwa.
Lutumo amewakumbusha madereva waliosajiliwa kwenye kanzi data kutowaazima viakisi mwanga vilivyo na namba za utambulisho kwa wenzao ambao hawajajisajili kwani wanaweza kufanya matukio ya kihalifu na viakisi mwanga vikatumika kama utambulisho wa watuhumiwa hao kisha kuchukuliwa hatua za kisheria.
Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Maafisa Usafirishaji Wilaya ya Kibaha Mwinyichande Mungi amesema watatekeleza zoezi hilo kwa weledi na kuhakikisha kila anayetaka kufanya kazi hiyo anafuata taratibu ikiwa ni pamoja na kujisajili na kupata namba ya utambulisho.
Aidha mwenyekiti wa CCM Kata ya Kongowe Saimon Mbelwa amewataka madereva hao kutambua kazi yao ina mchango mkubwa kwa jamii hivyo wale wenye kuingia kwenye kazi hiyo kwa lengo la kufanya vitendo vya Uhalifu wanapaswa kupigwa vita na kufichuliwa.
MADEREVA WA SERIKALI PWANI WAKUMBUSHANA UWAJIBIKAJI
Na Mwandishi wetu, KIBAHA
CHAMA cha Madereva wa Serikali Mkoa wa Pwani kimewakumbusha madereva kuwajibika katika majukumu yao Ili waweze kupata haki zao wanazostahili.
Mwenyekiti wa Chama hicho Michael Mbilinyi aliyasema hayo Julai 21 katika mkutano uliofanyika mjini Kibaha ambao ulihudhuriwa na viongozi wa chama hicho kutoka Halmashauri za mkoa wa Pwani .
Katika mkutano huo ambao ulilenga kujadili mambo mbalimbali ya chama uliambatana na semina elekezi ilivyokuwa ikielezea wajibu wa madereva wawapo kazini na mambo ya kufuata kabla hawajadai haki zao za msingi.
"Tutekeleze wajibu wetu halafu tutadai haki zetu za msingi, tuzingatie kufuata muda wa kazi na lugha sahihi pindi tunapokuwa na viongozi wetu utii na uwajibikaji utaondoa ukakasi wakati wa kudai haki," amesema Mbilinyi.
Mwenyekiti huyo amesema chama hicho ambacho uongozi wake ni kuanzia ngazi ya Taifa pamoja na mambo mengine kinatetea haki za madereva kwa mwajiri pindi anapoenda tofauti lakini pia dereva akienda kinyume wanamrudisha kwenye maadili.
Katibu wa chama hicho Isack Chambo aliwasisitiza wanachama kuzingatia michango waliyoiweka Ili kuendelea kuwa hai lakini pia kufanya mambo ambayo yapo ndani ya chama hicho kwa mujibu wa katiba yao.
Naye mmoja wa Wajumbe wa mkutano huo kutoka Halmashauri ya Chalinze Mkombozi Maskuzi ameomba viongozi wao kuwaandalia semina elekezi za mara kwa mara lakini pia waweatembelee kwenye maeneo yao huku wakizingatia kutoa taarifa sehemu zao za kazi Ili kuonyesha umuhimu wa nafasi zao.
Mjumbe mwingine aliyeshiriki mkutano huo Briton Kidinzi amewataka madereva kuwa mfano kwenye utendaji kazi wao mahala pa kazi kwa kufuata Sheria na maadili.
Mwisho
Wednesday, July 17, 2024
FANYENI UCHUNGUZI WA MACHO ANGALAU MARA MOJA KWA MWAKA
Na Mwandishi Wetu, Dodoma
Wananchi wameshauriwa kufanya uchunguzi wa macho angalau mara moja kwa mwaka ili kubaini kama kuna viashiria vya shambulizi la ugonjwa wa sukari katika jicho, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Macho, Dkt Joshua Mmbaga, ameshauri.
Dkt Mmbaga, ambaye anatoka Kliniki ya Macho ya Hospitali ya Benjamin Mkapa (BMH) ameyasema leo wakati akiwasilisha mada katika programu maulumu ya mafunzo maarufu kama Continues Medical Education (CME) inayotolewa kila Jumatano ikihusisha watumishi wote wa BMH.
"Ugonjwa wa kisukari ambao unasababisha kiwango cha sukari katika damu ambacho kinaharibu seli ambazo zinaenda kuharibu mishipa ya damu na kusababisha kuwa mishipa milaini hivyo kupasuka kirahisi na kusababisha kuvuja damu na kupoteza uwezo wa kuona," amesema Dkt Mmbaga.
Dkt Mmbaga ametaja sababu za ugonjwa wa kisukari kuwa ni ulaji wa vyakula vyenye kiwango kikubwa cha sukari,wanga na unywaji wa kiwango kikubwa na uliopitiliza wa pombe, akisema hii inasabisha ugonjwa wa kisukari ambao baadae unaenda kushambulia jicho.
Dkt. Mmbaga ametaja dalili za ugonjwa huu kuwa ni kutokuona vizuri, kuona mawingu mawingu, kuona kama vijidudu vinaelea angani na kuona vitu katika maumbo yamebadilika au ghafla kupoteza uwezo wa kuona .
“Nashauri watu kufanya uchunguzi wa macho angalau mara moja kwa mwaka hata kama huna tatizo la sukari lakini pia watu wajihusishe na mazoezi ya viungo ili kujiweka katika hali nzuri ya kiafya.” amesema Dkt Mmbaga.
Dkt. Mmbaga ametoa wito kwa wenye matatizo wa kisukari wafike Hospitali Benjamin Mkapa wachunguze macho yao na kufata masharti ya madaktari wao na waliokutwa na tatizo hilo waanze matibabu mara moja ili kuepuka kupata madhara makubwa zaidi.
Tuesday, July 16, 2024
WATAKIWA KUACHA IMANI ZA KISHIRIKINA KUPATA UONGOZI
VIONGOZI wanaowania nafasi za uongozi wametakiwa kuacha kuwa na imani kuwa viungo vya watu wenye Ualbino vinasaidia kupata uongozi.