Thursday, July 30, 2015

HABARI ZA PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
MGOMBEA Ubunge anayewania kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye Jimbo la Kibaha Mjini Abdulaziz Jad Maarufu kama Mwarabu amesema kuwa wana CCM wasichague mbunge ambaye ni sawa na mfadhili kwani atakwamisha shughuli za maendeleo katika Jimbo hilo.
Jad aliyasema hayo juzi mjini Kibaha kwenye mkutano wa wagombea wa ubunge wa CCM kuomba kura kwenye kata ya Maili Moja na kusema kuwa baadhi ya wabunge ni sawa na wafadhili ambao hutoa misaada kwa msimu.
Alisema kuwa wabunge wa namna hiyo hujitokeza wakati wa vipindi vya uchaguzi lakini wakishachaguliwa na uchaguzi ukipita hawaonekani tena kwani maendeleo yake yatakuwa ya msimu na si endelevu.
“Sisi wakazi wa Jimbo la Kibaha tunahitaji Mbunge wa kutuletea maendeleo na si mfadhili ambaye anatoa misaada kwa msimu hasa ule wa uchaguzi na mkishamchagua hamuoni tena hadi baada ya miaka mitano,” alisema Jad.
Aidha alisema kuwa wabunge wa namna hiyo wanaleta maendeleo ya msimu lakini endapo watamchagua yeye atawaletea maendeleo endelevu na si ya msimu kama wanavyofanya baadhi ya wafadhili.
“Baadhi yao ni wafadhili lakini wanavaa kofia ya uongozi hawa hawatufai lakini mkinichagua mimi nitawaletea maendeleo enedelevu na si yale ya msimu ambayo yametudumaza,” alisema Jad.
Alibainisha kuwa endapo ilani ya chama itatekelezwa kwa ufanisi basi maendeleo yatapatikana kwani inajibu changamoto zilizopo kwenye sekta zote za maendeleo pia aliahidi kuondoa makundi yaliyojitokeza katika kipindi hichi cha uchaguzi.
Mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
SERIKALI imeombwa kuajiri watu wenye taaluma ya sheria kwenye mabaraza ya ardhi ili kupunguza migogoro ya ardhi iliyopo kwenye maeneo mengi ya miji na vijiji.
Hayo yalisemwa Bagamoyo na Raya Fereji makamu mwenyekiti wa asasi isiyo ya kiserikali ya Mkombozi wilayani Bagamoyo mkoani Pwani wakati wa mafunzo ya sheria ya ardhi kwa waandishi wa habari na wadau wa ardhi wilayani humo.
Fereji alisema kuwa mabaraza ya ardhi yanaendeshwa na watu wasiokuwa na taaluma ya sheria wakati masuala yenyewe ni ya kisheria hali ambayo inasababisha migogoro ishindwe kwisha.
“Mabaraza haya yanaundwa na watu maarufu kwenye maeneo yao lakini hawana taaluma ya kisheria licha ya kuwa utatuzi wa migogoro ya ardhi unakwenda kisheria,” alisema Fereji.
Alisema kuwa ili migogoro hiyo ipungue hakuna budi kuwatumia watu wenye taaluma ya sheria ili kukabiliana na migogoro hiyo am,bayo imekithiri.
“Hata kama itashindwa kuwatumia watu wenye taaluma hiyo basi iyapatie mafunzo ya sheria mabaraza hayo kwani uzoefu unaonyesha kuwa maamuzi mengi yanayotolewa ya utatuzi wa migogoro ya ardhi inakuwa na kasoro nyingi,” alisema Fereji.
Kwa upande wake mwanasheria wa Kujitegemea Boka Lyamuya alisema kuwa migogoro mingi ya ardhi inashindwa kutatuliwa kutokana na baadhi ya watendaji  kwenye maeneo hayo kupindisha sheria.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WAGOMBEA wa nafasi za Ubunge na Udiwani mkoani Pwani wametakiwa kuweka ajenda ya kuhifadhi misitu kama sehemu ya kampeni zao za kuomba nafasi za uongozi.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha ofisa Mradi wa  Kuhifadhi Misitu ya Asili Tanzania (TFCG) Yahaya Mtonda alisema kuwa misitu hiyo endapo itaundiwa sera nzuri itasaidia kurejesha uoto wa asili ambao umetoweka kutokana na uharibifu wa mazingira.
Mtonda alisema kuwa misitu hiyo imekuwa ni chanzo kikuu cha upatikanaji wa mvua pamoja na hali ya hewa nzuri pia kukabiliana na mmomonyoko wa ardhi hivyo wawania nafasi za uongozi lazima watoe kipaumbele cha jinsi gani ya kukabiliana na hali hiyo ya uharibifu wa mazingira.
“Mabadiliko ya tabianchi  yanatokana na uharibifu wa misitu hivyo wawania nafasi za uongozi lazima wabebe suala hilo kama ajenda muhimu wanaponadi sera zao ili kuokoa misitu ya asili na ile isiyo ya asili,” alisema Mtonda.
Aidha alisema kuwa moja ya misitu ya asili hasa ile iliyojirani na Jiji la Dar es Salaam ambayo ni Kazimzumbwi na msitu wa Pugu iliyopo wilayani Kisarawe ni muhimu kwani ndiyo inayochuja hali ya hewa na kuifanya iwe nzuri.
“Kama mnavyofahamu Jiji la Dar es Salaam lina zalisha hewa mbaya kutokana na magari, viwanda na shughuli mbalimbali za kimaendeleo hivyo misitu hii ni kama mapafu ya kupumulia hivyo kutufanya tupate hewa nzuri lakini endapo isingekuwepo basi athari za kiafya zingekuwa kubwa sana,” alisema Mtonda.
Aliwataka wananchi kuwauliza wagombea kuwa wameweka mikakati gani ya kuhifadhi misitu na utunzaji wa mazingira ili kukabiliana na uvunaji holela wa misitu kwenye mkoa huo.
Mwisho.   
  Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI wa Kijiji cha Minazimikinda kata ya Ruvu kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani wamemwomba Waziri wa Ardhi na Makazi Wliam Lukuvi kutembelea Kijiji chao ili kukabiliana na mgogoro wa muda mrefu baina yao na Kijiji cha Kwala.
Moja ya wakazi wa Kijiji hicho Mohamed Palu alisema kuwa mgogoro huo ni wa muda mrefu na umekuwa ukiwachukulia muda mrefu kuutatua bila ya mafanikio hivyo kushindwa kufanya shughuli za maendeleo.
Palu alisema kuwa mgogoro huo umesababisha shughuli za kimaendeleo katika eneo hilo kukwama kutokana na kila upande kudai eneo hilo ni la upande mwingine.
“Tumetumia njia nyingi za kusuluhisha mgogoro huu lakini hadi sasa hakuna hatua zozote zilizofikiwa kuumaliza mgogoro huo hivyo tunaona endapo waziri atakuja anaweza kuutatua,” alisema Palu.
Alisema kuwa kamati ya Bunge inayoshughulikia migogoro ya ardhi ilifika Kijijini hapo mwezi Machi mwaka huu lakini hadi sasa hakuna taarifa yoyote juu ya suluhu ya mgogoro huo.
“Mgogoro huu na mingine iliyopo Kijijini ni moja ya changamoto kubwa zinazotukabili hivyo endapo waziri atakuja atatusaidia kuitatua na hivyo itasaidia wananchi kuendelea na shughuli za maendeleo,” alisema Palu.
Aidha alisema kuwa baadhi ya viongozi wa Vijiji wamekuwa wakichangia migogoro hiyo kutokana na kutozingatia ramani za vijiji hivyo hali inayosababisha kuwa na migogoro hiyo.

 Baadhi ya wanachama wa CCM kata ya Maili Moja wakiwasikiliza watia nia wa CCM walipokuwa wakimwaga sera jana mjini Maili Moja
Mwisho.    
Wawania nafasi ya Ubunge kupitia chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini mkoani Pwani kuanzia kushoto Rashid Bagdela Iddi Majuto, Abdulaziz Jad, Silvestry Koka na Rutatina Rugemalila

Tuesday, July 28, 2015

LIGI NETBALL PWANI KUFANYIKA AGOSTI 3 MWAKA HUU

Na John Gagarini, Kibaha
CHAMA Cha Mpira wa Pete mkoani Pwani kinatarajia kufanya mashindano ya mchezo huo Agosti 3 mwaka huu ili kupata timu itakayopanda ligi daraja la pili Taifa itakayowakilisha mkoa huo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha mwenyekiti wa chama hicho Fatuma Mgeni alisema kuwa jumla ya timu 14 zitachuana kwenye michuano hiyo itakayofanyika kwenye uwanja wa Bwawani maili Moja Kibaha.
Mgeni alisema kuwa wanatarajia kila wilaya itatoa timu mbili ili mashindano yawe na uhalisia wa mkoa kwa kushirikisha timu za wilaya hizo.
“Tayari tumeshawapa taarifa wilaya zote waandae timu ili ikifika wakati walete timu zao ziweze kuwakalisha wilaya zao nah ii ni moja ya kuhamasisha mchezo huo maeneo mbalimbali ya mkoa,” alisema Mgeni.
Alisema kuwa awali mashindano hayo yalikuwa yafanyike Julai 10 mwaka huu lakini kutokana na sababu ambazo zilishindwa kuzuilika ilibidi mashindano hayo yasogezwe mbele.
“Maandalizi yako vizuri na tayari timu zimeshaplekewa taarifa za kushiriki mashindano hayo ambayo yatapandisha timu moja kwenda daraja la pili Taifa japo kuna uwezekano wa kupandisha timu mbili ila hilo bado halijawa wazi sana,” alisema Mgeni.
Aidha alizitaka timu zinazotarajiwa kushiriki michuano hiyo kujiandaa kikamilifu ili kushirikia michuano hiyo ili mkoa uweze kupata timu nzuri.
Mwisho.

     

CCM JITOKEZENI KWA WINGI KWENYE KURA ZA MAONI NA UCHAGUZI MKUU

Na John Gagarini, Kibaha
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wilayani Kibaha mkoani Pwani wametakiwa kujitokeza kwa wingi ili kukipigia kura chama hicho kwenye uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu na si kujitokeza kwa wingi kwenye kura za maoni pekee.
Hayo yalisemwa na katibu wa CCM jimbo la Kibaha Mjini Abdala Mdimu wakati akiwanadi wagombea watano wa chama wanaowania kuteuliwa Ubunge wa Jimbo hilo kwenye kata ya Picha ya Ndege na Lulanzi.
Mdimu alisema kuwa wanachama wanaotarajiwa kupiga kura za maoni watakuwa wengi ikiwa na maana kwenye uchaguzi wa ndani ya chama lakini nje ya chama yaani uchaguzi mkuu wanachama hawajitokezi kwa wingi.
“Sasa tubadilike kwani CCM ndicho chama chenye wanachama wengi ikilinganishwa na vyama vingine lakini utashangaa wapinzani wanashinda kwa kura nyingi ambazo nyingine zinatoka humuhumu huku wengine wakiwa hawajitokezi kupiga kura lakini kura ndani ya chama ni nyingi sana,” alisema Mdimu.
Alisema kuwa wanachama wote ambao wamekidhi vigezo wanapaswa kujitokeza kupiga kura kwa wingi ndani ya chama na kwenye uchaguzi mkuu kwani kutojitokeza kwenye uchaguzi mkuu utasababisha ushindi kuwa mdogo.
“Tunataka ushindi wa kishindo kama ilivyokuwa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo mlijitokeza kwa wingi na chama kushinda kwa kishindo tunataka wembe huo huo muuendeleze kwani ushindi uko dhahiri,” alisema Mdimu.
Aidha alisema kuwa Wanaccm hawapaswi kuimba wimbo wa ushindi huku hawafanyi kazi kwani wanatakiwa kufanya kazi ili baadaye waje kuimba wimbo wa ushindi kwani moja wapo kati ya wanaowania nafasi ya kuwakilisha chama nafasi ya ubunge ni wazuri.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MUWANIA Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wilayani Kibaha mkoani Pwani Rugemalila Rutatina amesema kuwa endapo atateuliwa atakuwa kiongozi na si mtawala.
Aliyasema hayo juzi kwenye kata ya Picha ya Ndege mjini Kibaha wakati akiomba kura kwa wanachama wa matawi ya kata hiyo na kusema kuwa uongozi bora ndiyo utakaowaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo.
Rutatina ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM NEC kutoka Jimbo hilo alisema kuwa nafasi hiyo ni uongozi wa kuonyesha njia na si kuwa mtawala kwani mtawala yeye ni kutumia nguvu na kuelekeza pasipo yeye kuwajibika.
“Kiongozi ni kuwajibika wewe mwenyewe na kuwaonyesha njia watu unaowaongoza lakini mtawala yeye hana muda wa kutumikia wananchi zaidi ya kuamrisha jambo ambalo halifai kwani si shirikishi kwa wananchi,” alisema Rutatina.
Alisema kuwa ilani inajibu masuala yote ya maendeleo kwani imegusa sekta zote ikiwemo afya, elimu, ardhi, barabara, umeme, maji, mawasiliano na huduma zote za kijamii.
“Endapo mtanichagua nitazingatia mambo matatu ambayo ni ushirikishaji wananchi, ardhi, siasa safi na uongozi bora naamini katika haya yatasaidia kukabiliana na changamoto zilizopo ili kuwaletea maendeleo,” alisema Rutatina.
Wagombea wengine wanaowania nafasi hiyo ya kukiwakilisha chama kwenye kinyanganyiro cha Ubunge kwenye Jimbo hilo ni Silvestry Koka anayetetea kiti hicho, Abdulaziz Jab, Rashid Bagdela na Idd Majuto.
Mwisho 

Friday, July 24, 2015

VULLU, MGALU WATESA UBUNGE VITI MAALUMU PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
 MBUNGE wa Viti Malumu Zainab Vulu ameshinda kwenye uchaguzi wa Viti Maalumu kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Pwani kwenye uchaguzi kwa kupata kura 342.
Uchaguzi huo ambao ulifanyika juzi mjini Kibaha ulishuhudia Mbunge mwingine wa viti maalumu wa mkoa huo Subira Mgalu naye alifanikiwa kushinda kwa kujipatia kura 296.
Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nancy Mtalemwa aliyejinyakulia kura 145 huku Alice Mwangomo kura 45, Dk Zainab Gama kura 43, huku Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga na wengine watano wakiambulia kura saba kila mmoja.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kibaha Mjini Dk Zainab Gama alishinda kupitia mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO) ambaye alijinyakulia kura 394 akifuatiwa na Elizabeth Maya 37 na Esta Juma kura 15.
Nafasi ya ubunge kupitia nafasi ya ulemavu mshindi alikuwa ni Sita Sakawa aliyepata kura 262 ambaye alimshinda Tungi Mwanjala aliyepata kura 178, kwa upande wa ubunge wafanyakazi Hawa Chakoma alishinda kwa kupata kura 354 akimshinda Julieth Mjale aliyepata kura 82.
Upande wa Vyuo vikuu mshindi alikuw ani Dk Alice Kaijage ambaye hakuwa na mpinzani alipata kura 453 ambapo jumla ya wapiga kura walikuwa zaidi ya 450.
Moja ya wasimamizi wa uchaguzi huo mkuu wa mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo ambaye alitangaza matokeo hayo alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na chama.
Ndikilo alisema kuwa uchaguzi ulikwenda vizuri na kutokana na ukomavu wa wagombe ahakukutokea matatizo yoyote kwani kila upande uliridhika na matokeo hayo bila ya kupinga.
Kwa upande wake Zainab Vullu aliwashukuru wapiga kura kwa kuweza kumchagua kuwa mwakilishi wao na kusem akuwa atahakikisha anakabiliana na changamoto hususan kwa akinamama kwa kuwawezesha kwa mafunzo ya ujasiriamali.
Mwisho.


HARAKATI ZA UCHAGUZI ZAENDELEA

Na John Gagarini, Kibaha
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wametakiwa kuacha tabia ya kukumbatia makundi mara baada ya uchaguzi wa ndani kumalizika kwani yanasababisha chama kushinda kwa tochi.
Hayo yalisemwa juzi na mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Maulid Bundala wakati akiwanadi watia nia waliojitokeza kuwania kuchaguliwa na chama hicho kupeperusha bendera kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Bundala alisema kuwa makundi hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa chama kushindwa kutokana na mshikamano na ushirikiano kutokuwepo kwenye chaguzi mbalimbali ambazo zinahusisha vyama vingi vya siasa.
“Kipindi hichi ni kigumu sana kuwa na kundi siyo tatizo lakini mara atakapopatikana mgombea mmoja wa ubunge makundi yanatakiwa kwisha na kubakia kundi moja tu la CCM ambalo linatakiwa lipambane na wapinzani,” alisema Bundala.
Alisema kuwa kwanini chama kishindwe kwa mbinde kwa ushindi wa tochi wakati kina wanachama wengi ukilinganisha na vyama vya upinzani lakini inaonekana kushindwa kunatokana na kukumbatiwa kwa makundi hayo.
“Makundi yanatakiwa yaishe mara uteuzi wa mwanachama mmoja ambaye atawakilisha chama kwenye uchaguzi tatizo linguine ni wanachama kumpenda mtu badala ya kukipenda chama na kuachana na tabia ya kuwasema vibaya wagombea kwani wote ni Wanaccm,” alisema Bundala.
Aliwataka wanaccm ambao wanasifa ya kupiga kura za maoni za kuchagua mbunge kwenye kura za maoni wanapaswa kuwa hai kwa kulipia kadi za chama, wawe wameorodheshwa kwenye daftari la tawi na wawe na kadi ya kupigia kura.
Mwisho.
 Na John Gagarini, Kibaha
WATIANIA wanne wa Jimbo la Kibaha Mjini wilayani Kibaha mkoani Pwani kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) wameendelea kumwaga sera zao kwa wanachama ili waweze kupata fursa ya kuchaguliwa na chama hicho kwa kupigiwa kura za maoni kupata mgombea mmoja zinazotarajiwa kufanyika Agosti Mosi mwaka huu. 
Wagombea hao ambao ni Silvestry Koka ambaye anatetea kiti chake Rugemalila Rutatina, Idd  Majuto, Abdala Bagdela na Abdulaziz Jab wakiwa kwenye kata ya Kibaha na Kongowe wote kila mmoja alijinadi kwa staili ya aina yake ikiwa ni njia ya kuomba kuchaguliwa kwenye kura za maoni ili kukiwakilisha chama hicho kwenye nafasi ya Ubunge wa Jimbo hilo.
Kwa upande wake Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa NEC CCM, Rugemalila Rutatina alisema kuwa ilani ya chama ni nzuri sana lakini tatizo ni kwamba wasimamiaji ndiyo chanzo cha kushindwa kufikiwa kwa maendeleo.
Rutatina alisema kuwa endapo atachaguliwa athakikisha anaisimamia ilani ya chama ambayo ina majibu ya changamoto zote zinazowakabili wananchi na atakuwa kiongozi na si mtawala na kuwa ubunge ni ajira huku wananchi wakiwa ndiyo waajiri wa wabunge.
Silvestry Koka alisema kuwa katika uongozi wake amefanya mambo makubwa ikiwa ni pamoja na kukabiliana na changamoto ya maji ambapo ameweza kuhakikisha maji yanapatikana mitaa 14 ambapo kwa sasa kuna mradi mkubwa ambao utafanya Jimbo hilo kutokuwa na tatizo la maji.
Alisema anaomba achaguliwe tena ili aweze kukamilisha mipango iliyobaki kwani anauwezo wa kuongoza na kufanikisha maendeleo ya Jimbo hilo ambalo kwa sasa liko kwenye mchakato wa kuwa manispaa.
Abdulaziz Jaab alisema kuwa endapo atachaguliwa kwenye nafasi hiyo ya Ubunge kupitia CCM yeye atasimamia maendeleo endelevu na si uongozi wa nadharia ya kuongoza kwa msimu kama baadhi ya viongozi wanavyofanya.
Jab alisema kuwa kwa kushirikiana na wananchi atahakikisha anawashirikisha wananchi kwenye suala zima la maendeleo na si kujikita zaidi kwa vipindi huku muda mwingi wanachi wakiwa hawafikiwi hadi msimu wa uchaguzi.
Idd majuto yeye alisema kuwa wanCCM wanatakiwa kuacha kuchagua viongozi ambao wanatumia rushwa kupata uongozi kwani wanachangia kuzorotesha maendeleo ya wananchi kwani wanawanunua wananchi kama nyanya.
Alisema kama mgombea anatoa rushwa wao wale lakini wakati wa kuchagua waangalie nani anayefaa kuwa kiongozi na kuacha kuchagua viongozi wanaofanya rushwa kama kigezo cha kuwa kiongozi kwani hawafai.
Abdala Bagdela alisema kuwa endapo atachaguliwa atahakikisha kila mwananchi anamiliki nyumba ili aweze kuishi kwenye makazi bora huku fedha za ujenzi zikitokana na vyama vya kuweka na kukopa VICOBA.
Alisema kuwa atahakikisha anaweka mazingira mazuri kwa wajasiriamali wadogo kwa kuwaondolea kero za sheria zinazowabana ili waweze kufanya kazi zao bila ya usumbufu wanaoupata lengo wafanikiwe kujikwamua na hali ngumu.
Mwisho.
Na John Gagarini, Mufindi
WATIA nia watatu wamejitokeza kupambana na Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini ambaye ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mahmoud Mgimwa ambaye anattetea kiti chake kwenye Jimbo hilo ambalo limeganywa na kutoka Jimbo lingine la Mafinga Mjini .
Katibu wa CCM Jimson Mhagama alisema kuwa kwa sasa watia nia wote wanapitishwa kwa wanachama ili waeleze sera zao kwa wanachama ambao watawapigia kura za maoni zinazotarajiwa kufanyika Agosti Mosi mwaka huu ili kupata Mbunge atakayepambana na vyama vya upinzani.
Mhagama aliwataja wagombea wengine kuwa ni Dk Godfrey Kalinga, Godfrey Ngupula na Exaud Kigahe ambao kwa sasa wako kwenye zoezi la kunadi sera zao kwa wanachama ili wawachague mmoja aweze  kupeperusha bendera ya chama.
Kwa upande wa Jimbo la Mafinga Mjini ambalo limemegwa kutoka Jimbo la Mufindi Kaskazini jumla ya wagombea watano watachuana kwenye kinyanganyiro hicho ambao ni Zuber Ngullo, Cosato Chumi, Paul Myinga, Benjamin Balali, James Mgimwa.
Aidha alisema kuwa Jimbo la Mufindi Kusini jumla ya watia nia 15 wamejitokeza kuwania nafasi hiyo ambao ni Dickson Lutevele, Mary Miho, Golden Ally, Dionis Myinga, Frank Mng’olage, Dk Prosper Mfilinge, Anton Mpiluka, Charles Sanga, Menrad Kigola, Wende Ngahala, Faustin Mhapa, Marcelin Mkini, Dk Alex Sanga, Albert Chalamila na Robert Malangalila.   
Mhagama alisema kuwa wagombea wote ni wa CCM na wana sifa za kuwa wabunge kinachotakiwa ni wanachama kuchagua mmoja ambaye wataona anafa

Na John Gagarini, Bagamoyo

WAJUMBE wa mkutano mkuu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake  Tanzania kupitia Chama Cha Mapinduzi (UWT) Wilaya ya Bagamoyo mkoa wa Pwani wamechagua madiwani wake wa viti maalumu baada ya kufanyika kwa uchaguzi wa nafasi hiyo.

Kwenye uchaguzi huo  ulihudhuriwa na wajumbe wapiga kura 958 kutoka Tarafa saba zilizomo katika wilaya hiyo,uchaguzi ambao ulisimamiwa na Pilli Augostino ,aliyesaidiwa na Husna Ally huku mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya Almasi Masukuzi na katibu wake Kamote Kombo wakifuatilia mchakato mzima.

Katika kinyang’anyiro hicho kilikuwa na jumla ya wagombea 22 waliojitokeza kuwania nafasi hiyo kutokea kwenye Tarafa saba zilizomo wilayani humo ambazo ni Msoga, Chalinze, Msata, Miono, Kwaruhombo, Mwambao na Yombo.

Pilli alisema kutoka Tarafa ya Chalinze kura za washindi katika mabano ni Mwanakesi Madega (555) dhidi ya Nuru Mhami (78), Tarafa ya Kwaruhombo Asha Mtunye (35), Tatu Mpongo (443) na Tunu Mpwimbwi (476). Tarafa ya Msoga Zaituni Kawogo (57), Matha Patel (400) na Maria Moreto (426).

Tarafa ya Msata Sophia Issa (89), Anzeni Rajabu (294), Rehema Mno (484). Tarafa ya Miono Tukae Kilo (321), Sijali Mpwimbwi (612). Tarafa ya Mwambao Nuru Abdallah (5), Leonia Fransic (11), Shumina Sharifu (172) Sinasud Onelo (199) Hapsa Kilingo (563). Tarafa ya Yombo Togo Omary (205), Nuru Mohamed (260)na Elizabeth Shija (458).

Katika mchakato huo ngazi ya kapu Togola alipata  (81), Sinasud (175), Sophia (118), Zaituni (31), Tukae (103), Leonia (140), Magazin (210), Shumina (308), Tatu (274), Nuru Mohamed (18), Asha (5), Nuru (4), Mhami (49), Matha (289), Anzeni (45). Hivyo Shumina Sharifu na Martha Patel.

Baada ya kutangaza matokeo hayo,Pilli aliwataka madiwani hao kwenda kufanyakazi ili kuhakikisha wagombea wote wanaotokea ndani ya CCM wanashinda kwa kishindo kwani kinyume chake ushindi huo ni kazi bure.

Mwisho.
 Na John Gagarini, Kibaha
WANACHAMA wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wametakiwa kuacha tabia ya kukumbatia makundi mara baada ya uchaguzi wa ndani kumalizika kwani yanasababisha chama kushinda kwa tochi.
Hayo yalisemwa juzi na mwenyekiti wa CCM Kibaha Mjini Maulid Bundala wakati akiwanadi watia nia waliojitokeza kuwania kuchaguliwa na chama hicho kupeperusha bendera kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.
Bundala alisema kuwa makundi hayo yanachangia kwa kiasi kikubwa chama kushindwa kutokana na mshikamano na ushirikiano kutokuwepo kwenye chaguzi mbalimbali ambazo zinahusisha vyama vingi vya siasa.
“Kipindi hichi ni kigumu sana kuwa na kundi siyo tatizo lakini mara atakapopatikana mgombea mmoja wa ubunge makundi yanatakiwa kwisha na kubakia kundi moja tu la CCM ambalo linatakiwa lipambane na wapinzani,” alisema Bundala.
Alisema kuwa kwanini chama kishinde kwa mbinde kwa ushindi wa tochi wakati kina wanachama wengi ukilinganisha na vyama vya upinzani lakini inaonekana kushindwa kunatokana na kukumbatiwa kwa makundi hayo.
“Makundi yanatakiwa yaishe mara uteuzi wa mwanachama mmoja ambaye atawakilisha chama kwenye uchaguzi tatizo linguine ni wanachama kumpenda mtu badala ya kukipenda chama na kuachana na tabia ya kuwasema vibaya wagombea kwani wote ni Wanaccm,” alisema Bundala.
Aliwataka wanaccm ambao wanasifa ya kupiga kura za maoni za kuchagua mbunge kwenye kura za maoni wanapaswa kuwa hai kwa kulipia kadi za chama, wawe wameorodheshwa kwenye daftari la tawi na wawe na kadi ya kupigia kura.

Mwisho.

Wednesday, July 22, 2015

POLISI PWANI WAKAMATA SILAHA WALIZOPORWA POLISI NA HABARI MBALIMBALI

Na John Gagarini, Kibaha

JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kukamata silaha aina ya Sb Mchine Gun (SMG) ikiwa na risasi 30 kwenye magazini ambayo majambazi waliwapora askari eneo la Yombo Jijini Dar es Salaam Aprili 15 mwaka huu.

Mbali ya silaha hiyo pia walikamata silaha nyinge mbalimbali zikiwemo bunduki nne, risasi 153, mabomu na nyaya za milipuko katika msako maalumu wa kusaka wahalifu wanaodaiwa kuhusika katika matukio kadhaa yakiwemo ya uvamizi wa vituo vya Polisi na taasisi za fedha Mkoani humo na mikoa jirani ukiwemo wa Dar es Salaam.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani humo Jafari Ibrahim alisema silaha hiyo iliporwa na majambazi hayo kutoka mikononi mwa polisi waliokuwa doria kisha kutoweka nayo ambayo ilikuwa ni ya kituo cha polisi cha Tazara.

Kamanda Ibrahimu alisema kuwa silaha hiyo ilikuwa na namba 14302621 pia silaha nyingine iliyokamatwa ni Short Gun yenye namba G 74533 ambayo iliporwa Juni 10 mwaka huu kwenye kituo cha mafuta cha Mogas kilichopo Mkata wilaya ya Handeni mkoani Pwani.

“Kukamatwa silaha hizi ni mafanikio ya operesheni iliyofanywa na jeshi katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita na tunawapongeza wananchi kwa ushirikiano waliouonyesha uliofanikisha kukamatwa kwa silaha hizi na vitu vingine,” alisema Ibrahim

Alisema kuwa mbali ya silaha zilizotajwa hapo juu pia waliweza kukamata silaha nyingine ambazo ni Visu 11,Mapanga 4,Majambia 3,Risasi 20 za SMG, Risasi 103 za Shortgun, Milipuko ya mabomu 3,Vipande vidogo vya nondo 42,fyuzi zilizotegwa 24,Fyuzi tupu 56,Water Gel Explosive 3, Silicon Rubber 100% moja, Nyaya 3 za Milipuko, Bunduki 2 zilizotengezwa kienyeji pamoja na bunduki moja aina ya Rifle.

"Sihala hizi zote zipo hapa kwetu na kwa kweli ndugu waandishi kama silaha zingeendelea kuwa mikononi mwa wahalifu ni wazi kuwa madhara kwa mali na maisha yetu yangekuwa hatarini,ninyi kama wadau muhimu katika jitihada za kupambana na wahalifu kupitia vyombo vya habari mnao wajibu wa kuendelea kuelimisha jamii kuendelea kushirikiana na jeshi la Polisi katika mapambano haya yanayohitaji nguvu ya pamoja,” alisema Ibrahim

Aidha alisema kuwa ni wazi kuwa mafanikio haya yametokana na jamii kutoa ushirikiano mkubwa kwa polisi katika kuwabaini wahalifu,kubaini matishio ya kiusalama na maficho ya magenge ya kihalifu kwenye mapori mbalimbali yaliyopo mkoani Pwani.

Alibainisha kuwa mbali ya kukamata silaha hizo pia wamekamata wahalifu 27 wanaotuhumiwa kuhusika katika matukio mbalimbali ikiwemo la uporaji silaha kituo cha polisi Yombo Dar es Salaam na waliohusika kwenye uporaji taasisi za kifedha  na taratibu za kuwafikisha mahakamani zimekamilika.

Mwisho
Na John Gagarini, Kibaha
HUKU mchakamchaka wa kuwania nafasi za ubunge na udiwani zikiwa zinaendelea nchini jumla ya wagombea wanne kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Jimbo la Kibaha Mjini watachuana kupata mgombea mmoja atakayepeperusha bendera ya chama hicho kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba mwaka huu.
Kwa mujibu wa katibu wa CCM Kibaha Mjini Abdala Mdimu alisema kuwa wagombea hao ndani ya chama ndiyo waliorejesha fomu za kuomba ridhaa ya kuchaguliwa na Wanaccm ili kugombea nafasi hiyo.
Mdimu alisema kati ya wagombea hao waliorejesha fomu ni pamoja na aliyekuwa mbunge wa Jimbo hilo Silvestry Koka ambaye atachuana na wanaccm wengine watatu ambao nao wameomba kuwania nafasi hiyo.
Aliwataja wagombea wengine kwenye kinyanganyiro hicho kuwa ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu CCM Taifa NEC Jimbo hilo Rugemalila Rutatina, Idd Majuto, Rashid Bagdela na Abdulaziz Jaab.
Katika Jimbo la Kibaha Vijijini jumla ya wagombea sita wamejitokeza kuwania nafasi hiyo akiwemo aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini Dk Ibrahim Msabaha watakaopambana na Mbunge wa Jimbo hilo Hamoud Jumaa.
Katibu wa CCM Kibaha Vijijini alisema kuwa wengine wanaowania nafasi hiyo ndani ya chama ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu Taifa NEC Jimbo hilo Allen Bureta, Hussein Chuma, Janeth Munguatosha na Shomary Sangali.
Mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
JUMLA ya wagombe 10 wa nafasi ya Ubunge wamerejesha fomu za kuwania kuchaguliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwenye Jimbo la Bagamoyo Mkoani Pwani ambalo nafasi yake inatetewa na Waziri wa Elimu na Mafunzo Dk Shukuru Kawambwa.
Kwa mujibu wa katibu wa CCM wilaya ya Bagamoyo Kombo Kamote alisema kuwa wengine waliorejesha fomu ni pamoja na Meya wa Mji Mdogo wa Bagamoyo Abdul Sharifu.
Kamote aliwataja wengine kuwa ni Muharami Mkenge, Salim Abeid, Mbonde Mbonde, Methew Yungwe, Maulid Mtulya, Fabian Said, Lekesani, Mvule na Chacha Wambura.
Katika Jimbo la Chalinze mbunge wa Jimbo hilo Ridhiwani Kikwete anatarajiwa kupambana na aliyewahi kuwa Mwenyekiti wa Klabu ya Yanga Iman Madega.
Wengine ni pamoja na Mbaraka Tamimu, Changwa Mkwezu, Omar Kabanga. Katika hatua nyingine  jumla ya wagombea 18 wa ubunge viti maalum mkoani Pwani watawania kuchaguliwa bada ya kurejesha fomu za kuwania nafasi hiyo ndani ya chama.
Mwisho.
Na John Gagarini, Iringa
WAFADHILI toka nchi ya Australia wametoa fedha zaidi ya shilingi bilioni 11 kuchangia mradi mkubwa wa maji kwenye Jimbo la Mufindi Kaskazini wilayani Mufindi mkoani Iringa.
Akizungumza na waandishi wa habari mjini Mafinga Mbunge wa Jimbo hilo Mahmoud Mgimwa alisema kuwa wafadhili hao wametoa fedha hizo ili kukabiliana na changamoto za maji kwenye Jimbo hilo.
Mgimwa ambaye pia ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii alisema kuwa fedha hizo zitatumika kwenye mradi mkubwa ambao utaondoa kabisa tatizo la maji kwenye Jimbo hilo.
“Mradi huu ni mkubwa na utaondoa kabisa changamoto hii ya maji kwani baadhi ya maeneo hayapati maji lakini mara utakapokamilika utakabili tatizo hilo na kubaki historia kwani maeneo yote yatapata maji ya uhakika,” alisema Mgimwa.
Alisema kuwa huku wafadhili hao wakitoa fedha hizo serikali nayo itachangia kiasi cha shilingi milioni 130 ambapo wafadhili hao watakuja na kuangalia mradi huo jinsi utakavyoendeshwa.
“Katika bajeti ya mwaka 2014/2015 serikali ilitoa kiasi cha shilingi milioni 500 kwa ajili ya kununua pampu tatu kutoka nchini Afrika Kusini na Arusha ambazo zitafanya maji yaweze kutoka kwa uhakika ambapo kwa sasa utokaji wake si mzuri kutokana na uchakavu wa miundombinu yake zikiwemo pampu hizo,” alisema Mgimwa.
Aidha alisema kuwa katika bajeti ya mwaka 2015/2016 serikali imetoa shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya maji ili kukabiliana na uchakavu.
Mwisho.
Na John Gagarini, Iringa
MBUNGE wa Jimbo la Mufindi Kaskazini na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Mamhoud Mgimwa amewaomba wadau mbalimbali wa maendeleo kusaidia kupatikana kwa vifaa vya X-Ray kwenye hospitali ya Mafinga ambayo ni ya Wilaya ya Mufindi ili iweze kutoa huduma zake kwa uhakika.
Mgimwa alisema kuwa hospitali hiyo ambayo imeboreshwa na kuwa ya kisasa kupita hospitali zote za mkoa wa Iringa inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa vifaa hivyo.
Alisema kuwa Mgimwa yeye pamoja na wananchi wa Jimbo hilo pamoja na serikali wamefanikiwa kuifanya hospitali hiyo kuwa ya kisasa na kutoa huduma bora lakini changamoto yake ni X-Ray.
“Tunaishukuru serikali kwani ilitoa kiasi cha shilingi milioni 600 ambazo zilitumika kufanya kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujenga wodi nzuri hivyo tunaomba wadau mbalimbali waendelee kujitokeza kuisaidia kukabilina na changamoto zilizopo,” alisema Mgimwa.
Aidha alisema kwa sasa hospitali hiyo ina jumla ya vitenda 10 vya kujifungulia akinamama ambapo kila kitanda kina thamani ya shilingi milioni 1.2.
“Kwa jumla huduma ya afya kwenye hospitali yetu ya wilaya ni nzuri licha ya kwamba kuna changamoto kidogo lakini hata hivyo tunaendelea kukabiliana nazo ili ziweze kuboreka,” alisema Mgimwa.
Alibainisha kuwa kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo watazikabili changamoto zilizopo ili wananchi waweze kupata huduma bora mara waendapo kupata huduma.

Mwisho.  

Monday, July 20, 2015

NAIBU WAZIRI ATOA MSAADA WA BATI NA SIMENTI KWA SHULE

Na John Gagarini, Iringa

KATIKA kukabiliana na changamoto za ukosefu wa nyumba za walimu Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini wilayani Mufindi mkoani Iringa Mahamoud Mgimwa ametoa bati 70 na mifuko 30 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za walimu wa shule ya Msingi ya Mpanga Tazara.
Akizungumza na wakazi wa Kijiji hicho alipotembelea kuangalia shughuli za maendeleo alisema kuwa ameamua kutoa vifaa hivyo ili kuhakikisha wlaimu wanakaa kwenye mazingira mazuri.
Mgimwa ambaye ni Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii alisema kuwa wananchi wa Kijiji hicho walikuwa na kilio cha muda mrefu cha walimu kukosa nyumba za kuishi hivyo ameona ni vema akatoa vifaa hivyo ili viweze kusaidia katika ujenzi wa nyumba za walimu.
“Kama mnavyojua mazingira ya huku yako pembezoni hivyo lazima kuyaweka vizuri ili watumishi hao waweze kukaa sehemu ambayo ni nzuri ili waweze kufanya kazi zao kwa amani,” alisema Mgimwa.
Alisema kuwa sekta ya elimu ina changamoto nyingi lakini yeye kwa kushirikiana na wananchi atahakikisha wanazikabili kwa kutoa misaada mbalimbali ili kuboresha mazingira ya usomaji.
“Awali shule hii ilikuwa na tatizo la choo lakini tulipigana na kuhakikisha choo kimejengwa tunakwenda kutatua changamoto zilizopo hatua kwa hatua ili kuhakikisha sekta ya elimu inapata mafanikio,” alisema Mgimwa.
Aidha alisema kuwa wazazi nao wanapaswa kuhakikisha wanachangia michango mbalimbali kwa ajili ya wanafunzi ili waweze kupata elimu inayotakiwa kwani kuna baadhi ya changamoto zinaweza kutatuliwa na wazazi.
Kwa upande wake Diwani wa kata ya Mpanga Tazara Flavian Mpanda alimshukuru mbunge huyo kwa kutoa vifaa hivyo na kusema kuwa vimekuja wakati muafaka kwani ujenzi wa nyumba za walimu ilikuwa ni changamoto kubwa.
Mpanda alisema jitihada zinazofanywa na mbunge huyo kuhakikisha shule hiyo inakuwa na mazingira mazuri zinapaswa kupongezwa na wapenda maendeleo.
Mwisho.

BARABARA YATENGEWA BILIONI MUFINDI KASKAZINI



Na John Gagarini, Iringa
BARABARA ya Kinyanambo C hadi Kisusa yenye urefu wa kilometa 131kwenye Jimbo la Mufindi Kaskazini wilaya ya Mufindi mkoani Iringa imetengewa kiasi cha shilingi billioni 1.2 kwa ajili ya matengenezo ya kawaida.
Hayo yalisemwa na Mbunge wa Jimbo la Mufindi Kaskazini Mahmoud Mgimwa wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mpanga Tazara akielezea juu ya kukabiliana na changamoto ya barabara katika Jimbo hilo.
Mgimwa alisema kuwa fedha hizo zimetengwa katika kipindi cha bajeti ambayo imeanza mwezi huu na tayari ujenzi wa barabara hiyo umeshaanza kwa kuweka makalavati ikiwa ni hatua za mwanzo za ujenzi huo.
“Barabara hii tayari imeshakabidhiwa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) mkoa kutoka Halmashauri ya mji wa Mafinga hali ambayo sasa imeipandisha hadhi hivyo itakuwa kwenye mikakati ya kuwekewa lami kupitia kampuni ya (MCC),” alisema Mgimwa.
Alisema kuwa matengenezo hayo yataboresha ubora wa barabara hiyo ambayo ni tegemeo na kuifanya kupitika wakati wote bila ya usumbufu na kurahisisha mawasiliano kwa wananchi na kwa wakulima ili waweze kupeleka mazao yao kwenye masoko baada ya kuvuna.
“Barabara hii ambayo inapita kwenye maeneo ya Itimbo, Ihalimba, Usokamu, Mapanda na Kisusa itakuwa ni moja ya barabara amabzo ziko kwenye mpango wa kuboreshwa na baada ya kupandishwa hadhi halmashauri itapata unafuu ambapo fedha ambazo zingetumika kuitengeneza sasa zitatumiwa kwenye shughuli nyingine za maendeleo,” alisema Mgimwa.
Aidha alisema kuwa barabara nyingine ni Kinyanambo A yenye urefu wa kilometa 151 ambayo inapita maeneo ya Msavanu, Mkombavanu, Sadani na Madibila nayo ujenzi wake tayari umeanza.
Pia alisema kuwa barabara ya Johns Corner yenye urefu wa kilometa 107 tayari imejengwa kwa kiwango cha lami urefu wa kilometa tano nab ado ujenzi wake unaendelea.
Alibainisha kuwa barabara hiyo inapita kwenye maeneo ya Mtili, Ifwagi, Mdabulo, Ihanu, Lulanga hadi Mpanga Tazara iko kwenye mpango wa kupandishwa hadhi ili ichukuliwe na (TANROADS), na barabara ya Mpanga Tazara hadi Mlimba ambayo imetengwa kiasi cha shilingi milioni 800.
“Barabara ya Mpanga Tazara hadi mlimba kwani inaunganisha wilaya mbili za Mufindi na Kilombero ni muhimu sana kwa ajili ya kurahisisha usafiri kwa wakulima kupeleka mazao yao kwenye masoko ambayo yana bei nzuri kama vile Makambako, Kilombero, Mbeya na Dar es Salaam,” alisema Mgimwa.
Mgimwa alisema kuwa barara nyingine ziko kwenye mchakato wa kuwapata makandarasi kwa ajili ya kuanza ujenzi katika bajeti inayoanzia mwezi huu wa Julai.
Mwisho.
Na John Gagarini, Iringa
JIMBO la Mufindi Kaskazini wilayani Mufindi mkoani Iringa linahitaji Transfoma 60 ili kukabiliana na changamoto ya ukosefu wa umeme kwenye kata tatu za Mpanga Tazara, Ikwea na Ikongosi.
Changamoto hiyo ya ukosefu wa umeme iko kwenye kata hizo kati ya kata 13 za Jimbo hilo ambapo upatikanaji wa Transfoma hizo utasaidia kuondoa kabisa ukosefu wa nishati hiyo kwa baadhi ya vitongoji.
Akizungumza na waandishi wa habari juu ya changamoto kwenye Jimbo la Mufindi Kaskazini, Mbunge wa Jimbo hilo Mahmoud Mgimwa alisema kuwa kwa sasa mchakato wa kutafuta Transfoma unaendelea.
“Thamani ya Transfoma moja ni kati ya shilingi milioni 40 na 60 na tunaendelea kuhakikisha vinapatikana ili kuondoa kabisa tatizo la umeme ndani ya jimbo letu lakini eneo kubwa tayari wanapata umeme,” alisema Mgimwa.
Alisema kuwa anaamini kuwa umeme utapatikana muda si mrefu na kuwataka wananchi kutokuwa na wasiwasi juu ya upatikanaji wa nishati hiyo muhimu ya umeme.
Aidha alisema kuwa maeneo mengi kwa sasa yanapata umeme hadi vijijini na sehemu chache zilizobaki tatizo hilo litakwisha na jitihada zinaendelea ili kufanikisha suala hilo.
Mwisho.    

Thursday, July 9, 2015

CHANGAMOTO BVR ZAIBUKA KIBAHA


Na John Gagarini, Kibaha

ZOEZI la uandikishaji Daftari la Kudumu kutumia mfumo mpya wa (BVR) wilayani Kibaha mkoani Pwani limekumbwa na changamoto ikiwemo wananchi kutumia muda mwingi kuandikishwa.

Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Ungindoni Kata ya Kongowe waliozungumza na Wapo Radio leo wamesema kuwa zoezi hilo linakwenda taratibu sana kutokana na waandikishaji.

Wananchi hao ambao ni Leonard Mhina na Seleman Kumchaya wamesema kuwa wanasiku mbili lakini hadi leo siku ya tatu bado hawajafanikiwa kuandikishwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mtaa wa Ungindoni Juma Njwaka amesema kuwa wananchi wanaoshindwa kuandikishwa ni wale ambao wanashindwa kufuata utaratibu.

Naye Ofisa Mtendaji wa Mtaa huo wa Ungindoni Magesa Lukale amesema kuwa maopareta wa mashine hizo wanafanya kazi vizuri labda tatizo ni kwa wazee ndiyo wanaochukua muda mrefu kutokana na kujieleza.

Mwisho.

Tuesday, July 7, 2015

WATU ZAIDI YA MILIONI 11 WAANDISKISHWA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA NCHINI

Na John Gagarini, Msoga
JUMLA ya watu milioni 11,248,194 wameandikishwa kwenye daftari la kudumu la wapiga kura zoezi ambalo linaendelea kwa sasa hapa nchini likiwa limeingia mkoani Pwani.
Hayo yalisemwa leo kwenye Kijiji cha Msoga kata ya Msoga wilayani Bagamoyo na mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Taifa Damian Lubuva alipokuwa anampa taarifa Rais Dk Jakaya Kikwete mara baada ya kujiandikisha.
Lubuva alisema kuwa malengo ni kuandikisha watu milioni 21 hadi 23 kote nchini mara zoezi hilo litakapokamilika kati ya Julai mwishoni au Agosti mwanzoni kama hakutatokea matatizo.
“Hadi sasa ni mikoa 11 inaendelea na zoezi ambayo ni Mwanza Shinyanga, Geita, Simiyu, Mara, Manyara, Arusha, Kilimanjaro Morogoro na jana ulianza mkoa wa Pwani,” alisema Lubuva.
Aidha alisema kuwa changamoto zilizojitokeza ni za kawaida hasa kutokana na mfumo huu kuwa ni mpya kwani kila jambo jipya lina changamoto zake.
“Mfumo huu ni mpya hivyo lazima kuwe na changamoto za hapa na pale lakini zoezi linakwenda vizuri na tunaamini kuwa tutafanikiwa kama tulivyopanga,” alisema Lubuva.
Mkoa wa Pwani una jumla ya vituo 1,752 na mashine za BVR 932 ambapo kata ya Msoga kuna jumla ya vituo 17 zoezi hilo kwa mkoa wa Pwani lilianza jana na litamalizika Julai 20.   
Mwisho.