Na
John Gagarini, Kibaha
WANACHAMA
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wilayani Kibaha mkoani Pwani
wametakiwa kujitokeza kwa wingi ili kukipigia kura chama hicho kwenye uchaguzi
mkuu Oktoba mwaka huu na si kujitokeza kwa wingi kwenye kura za maoni pekee.
Hayo
yalisemwa na katibu wa CCM jimbo la Kibaha Mjini Abdala Mdimu wakati akiwanadi
wagombea watano wa chama wanaowania kuteuliwa Ubunge wa Jimbo hilo kwenye kata
ya Picha ya Ndege na Lulanzi.
Mdimu
alisema kuwa wanachama wanaotarajiwa kupiga kura za maoni watakuwa wengi ikiwa
na maana kwenye uchaguzi wa ndani ya chama lakini nje ya chama yaani uchaguzi
mkuu wanachama hawajitokezi kwa wingi.
“Sasa
tubadilike kwani CCM ndicho chama chenye wanachama wengi ikilinganishwa na
vyama vingine lakini utashangaa wapinzani wanashinda kwa kura nyingi ambazo
nyingine zinatoka humuhumu huku wengine wakiwa hawajitokezi kupiga kura lakini
kura ndani ya chama ni nyingi sana,” alisema Mdimu.
Alisema
kuwa wanachama wote ambao wamekidhi vigezo wanapaswa kujitokeza kupiga kura kwa
wingi ndani ya chama na kwenye uchaguzi mkuu kwani kutojitokeza kwenye uchaguzi
mkuu utasababisha ushindi kuwa mdogo.
“Tunataka
ushindi wa kishindo kama ilivyokuwa kwenye uchaguzi wa Serikali za Mitaa ambapo
mlijitokeza kwa wingi na chama kushinda kwa kishindo tunataka wembe huo huo
muuendeleze kwani ushindi uko dhahiri,” alisema Mdimu.
Aidha
alisema kuwa Wanaccm hawapaswi kuimba wimbo wa ushindi huku hawafanyi kazi
kwani wanatakiwa kufanya kazi ili baadaye waje kuimba wimbo wa ushindi kwani
moja wapo kati ya wanaowania nafasi ya kuwakilisha chama nafasi ya ubunge ni
wazuri.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Kibaha
MUWANIA
Ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Kibaha Mjini wilayani Kibaha
mkoani Pwani Rugemalila Rutatina amesema kuwa endapo atateuliwa atakuwa
kiongozi na si mtawala.
Aliyasema
hayo juzi kwenye kata ya Picha ya Ndege mjini Kibaha wakati akiomba kura kwa
wanachama wa matawi ya kata hiyo na kusema kuwa uongozi bora ndiyo
utakaowaletea maendeleo wananchi wa Jimbo hilo.
Rutatina
ambaye ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM NEC kutoka Jimbo hilo
alisema kuwa nafasi hiyo ni uongozi wa kuonyesha njia na si kuwa mtawala kwani
mtawala yeye ni kutumia nguvu na kuelekeza pasipo yeye kuwajibika.
“Kiongozi
ni kuwajibika wewe mwenyewe na kuwaonyesha njia watu unaowaongoza lakini
mtawala yeye hana muda wa kutumikia wananchi zaidi ya kuamrisha jambo ambalo
halifai kwani si shirikishi kwa wananchi,” alisema Rutatina.
Alisema
kuwa ilani inajibu masuala yote ya maendeleo kwani imegusa sekta zote ikiwemo
afya, elimu, ardhi, barabara, umeme, maji, mawasiliano na huduma zote za
kijamii.
“Endapo
mtanichagua nitazingatia mambo matatu ambayo ni ushirikishaji wananchi, ardhi, siasa
safi na uongozi bora naamini katika haya yatasaidia kukabiliana na changamoto
zilizopo ili kuwaletea maendeleo,” alisema Rutatina.
Wagombea
wengine wanaowania nafasi hiyo ya kukiwakilisha chama kwenye kinyanganyiro cha
Ubunge kwenye Jimbo hilo ni Silvestry Koka anayetetea kiti hicho, Abdulaziz
Jab, Rashid Bagdela na Idd Majuto.
Mwisho
No comments:
Post a Comment