Friday, July 24, 2015

VULLU, MGALU WATESA UBUNGE VITI MAALUMU PWANI

Na John Gagarini, Kibaha
 MBUNGE wa Viti Malumu Zainab Vulu ameshinda kwenye uchaguzi wa Viti Maalumu kupitia Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) mkoa wa Pwani kwenye uchaguzi kwa kupata kura 342.
Uchaguzi huo ambao ulifanyika juzi mjini Kibaha ulishuhudia Mbunge mwingine wa viti maalumu wa mkoa huo Subira Mgalu naye alifanikiwa kushinda kwa kujipatia kura 296.
Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Nancy Mtalemwa aliyejinyakulia kura 145 huku Alice Mwangomo kura 45, Dk Zainab Gama kura 43, huku Katibu wa CCM mkoa wa Pwani Joyce Masunga na wengine watano wakiambulia kura saba kila mmoja.
Mbunge wa zamani wa Jimbo la Kibaha Mjini Dk Zainab Gama alishinda kupitia mashirika yasiyo ya Kiserikali (NGO) ambaye alijinyakulia kura 394 akifuatiwa na Elizabeth Maya 37 na Esta Juma kura 15.
Nafasi ya ubunge kupitia nafasi ya ulemavu mshindi alikuwa ni Sita Sakawa aliyepata kura 262 ambaye alimshinda Tungi Mwanjala aliyepata kura 178, kwa upande wa ubunge wafanyakazi Hawa Chakoma alishinda kwa kupata kura 354 akimshinda Julieth Mjale aliyepata kura 82.
Upande wa Vyuo vikuu mshindi alikuw ani Dk Alice Kaijage ambaye hakuwa na mpinzani alipata kura 453 ambapo jumla ya wapiga kura walikuwa zaidi ya 450.
Moja ya wasimamizi wa uchaguzi huo mkuu wa mkoa wa Pwani Evarist Ndikilo ambaye alitangaza matokeo hayo alisema kuwa uchaguzi huo umefanyika kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa na chama.
Ndikilo alisema kuwa uchaguzi ulikwenda vizuri na kutokana na ukomavu wa wagombe ahakukutokea matatizo yoyote kwani kila upande uliridhika na matokeo hayo bila ya kupinga.
Kwa upande wake Zainab Vullu aliwashukuru wapiga kura kwa kuweza kumchagua kuwa mwakilishi wao na kusem akuwa atahakikisha anakabiliana na changamoto hususan kwa akinamama kwa kuwawezesha kwa mafunzo ya ujasiriamali.
Mwisho.


No comments:

Post a Comment