Na
John Gagarini, Kibaha
CHAMA
Cha Mpira wa Pete mkoani Pwani kinatarajia kufanya mashindano ya mchezo huo Agosti
3 mwaka huu ili kupata timu itakayopanda ligi daraja la pili Taifa
itakayowakilisha mkoa huo.
Akizungumza
na mwandishi wa habari hizi mjini Kibaha mwenyekiti wa chama hicho Fatuma Mgeni
alisema kuwa jumla ya timu 14 zitachuana kwenye michuano hiyo itakayofanyika
kwenye uwanja wa Bwawani maili Moja Kibaha.
Mgeni
alisema kuwa wanatarajia kila wilaya itatoa timu mbili ili mashindano yawe na
uhalisia wa mkoa kwa kushirikisha timu za wilaya hizo.
“Tayari
tumeshawapa taarifa wilaya zote waandae timu ili ikifika wakati walete timu zao
ziweze kuwakalisha wilaya zao nah ii ni moja ya kuhamasisha mchezo huo maeneo
mbalimbali ya mkoa,” alisema Mgeni.
Alisema
kuwa awali mashindano hayo yalikuwa yafanyike Julai 10 mwaka huu lakini
kutokana na sababu ambazo zilishindwa kuzuilika ilibidi mashindano hayo
yasogezwe mbele.
“Maandalizi
yako vizuri na tayari timu zimeshaplekewa taarifa za kushiriki mashindano hayo
ambayo yatapandisha timu moja kwenda daraja la pili Taifa japo kuna uwezekano
wa kupandisha timu mbili ila hilo bado halijawa wazi sana,” alisema Mgeni.
Aidha
alizitaka timu zinazotarajiwa kushiriki michuano hiyo kujiandaa kikamilifu ili
kushirikia michuano hiyo ili mkoa uweze kupata timu nzuri.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment