Thursday, July 9, 2015

CHANGAMOTO BVR ZAIBUKA KIBAHA


Na John Gagarini, Kibaha

ZOEZI la uandikishaji Daftari la Kudumu kutumia mfumo mpya wa (BVR) wilayani Kibaha mkoani Pwani limekumbwa na changamoto ikiwemo wananchi kutumia muda mwingi kuandikishwa.

Baadhi ya wakazi wa mtaa wa Ungindoni Kata ya Kongowe waliozungumza na Wapo Radio leo wamesema kuwa zoezi hilo linakwenda taratibu sana kutokana na waandikishaji.

Wananchi hao ambao ni Leonard Mhina na Seleman Kumchaya wamesema kuwa wanasiku mbili lakini hadi leo siku ya tatu bado hawajafanikiwa kuandikishwa.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Mtaa wa Ungindoni Juma Njwaka amesema kuwa wananchi wanaoshindwa kuandikishwa ni wale ambao wanashindwa kufuata utaratibu.

Naye Ofisa Mtendaji wa Mtaa huo wa Ungindoni Magesa Lukale amesema kuwa maopareta wa mashine hizo wanafanya kazi vizuri labda tatizo ni kwa wazee ndiyo wanaochukua muda mrefu kutokana na kujieleza.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment