Na John Gagarini, Kibaha
RAIA wa nchi ya Ethiopia Dawita Alalo (25) amekufa alipokuwa
akipatiwa matibabu kwenye kituo cha afya cha Chalinze kata ya Bwiringu wilaya
ya Bagamoyo mkoani Pwani.
Marehemu alikuwa ni kati ya raia 48 wa nchi hiyo walikamatwa wakiwa
kwenye msitu wa kijiji cha Visakazi Ubena Zomozi tarafa ya Chalinze Agosti 22
mwaka huu, baada ya kuingia nchini bila ya kibali.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha
kaimu kamanda wa polisi mkoani humo Mrakibu Mwandamizi (SSP) Athuman
Mwambalaswa alisema kuwa marehemu ni miongoni mwa wahamiaji haramu 11 waliokuwa
wamelazwa kituoni hapo wakipatiwa matibabu.
Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 26
majira saa 7:30 usiku alipokuwa akipatiwa matibabu kituoni hapo baada ya kuugua
ugonjwa wa malaria.
Wakati huo huo mlinzi wa baa ya Silent Inn Jamat Mandama (55)
amefariki dunia baada ya kunywa pombe nyingi bila ya kula chakula.
Alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti 27 mwaka huu majira
ya saa 1 usiku huko Umwe kata ya Ikwiri wilayani Rufiji.
Aidha alisema kuwa mlinzi huyo alikutwa amekufa akiwa lindoni
kwenye baa hiyo.
Na John Gagarini, Kibaha
ASKARI sita wa jeshi la polisi mkoani Pwani wamenusurika kifo
kutokana na ajali ya barabarani baada ya gari walilokuwa wakisafiria kugongwa
na lori la mizigo.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha
kaimu kamanda wa polisi mkoani humo, Mrakibu Mwandamizi (SSP) Athuman Mwambalaswa
alisema kuwa askari hao walikuwa doria.
Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa tukio hilo lilitokea Agosti
26 majira ya saa 9:30 usiku eneo la Maili Moja Ujenzi wailayani Kibaha barabara
kuu ya Dar es Salaam Chalinze.
Alisema kuwa gari hilo lenye usajili namba PT 2012 lilikuwa
likiingia kwenye kituo cha mafuta cha Delina na kugongwa na lori hilo lenye
namba za usajili T 927 CAU na tela namba T 769 CJX.
“Lori hilo bada ya kuligonga gari hilo lapolisi kwa nyuma
likaenda kugongana na lori lingine lililokuwa likielekea Jijini Dar es Salaam lenye
namba T 672 BAC lenye tela namba T 672 BBW,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Alibainisha kuwa askari watatu walijeruhiwa vibaya ambao ni
namba F 4333 DC Tamimu ambaye amevunjika mguu wa kulia mara mbili, WP 6100 DC
Jaqline ambaye amejeruhiwa kichwani na H 3348 DC Armand ambaye amejeruhiwa
kichwani na kifuani.
“Askari wote wamelazwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa
Pwani Tumbi kwa matibabu zaidi ambapo tunaendelea kumtafuta dereva wa lori
lililosababisha ajali hiyo,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment