Na John Gagarini, Kibaha
BAADA ya dereva wa Texi Richard Ponera (36) mkazi wa
Mwendapole wilayani Kibaha mkoani Pwani kupotea kwa siku nane amepatikana akiwa
ameuwawa na kuporwa gari alilokuwa
akiliendesha.
Marehemu ambaye alikuwa akifanyia shughuli zake kwenye kituo
kikuu cha Mabasi cha Maili Moja wilayani humo alipotea Agosti 6 Mwaka huu
majira ya saa 1 usiku alipokodishwa na watu wawili wasio fahamika waliojifanya kuwa
ni wateja.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani humo Mrakibu Msaidizi wa Polisi (SSP) Athuman
Mwambalaswa alisema kuwa mwili wake ulitupwa vichakani.
Kamanda Mwambalaswa alisema kuwa mwili wa marehemu ulikutwa
huko eneo la Mihande Mashambani Mlandizi wilayani Kibaha ukiwa umeharibika vibaya
huku gari alilokuwa akiendesha lenye
namba za usajili T 905 BHT aina ya Corolla nyeupe.
“Chanzo cha mauaji hayo ni katika kuwania mali ambayo ni
gari hilo ambalo halijapatikana na hakuna mtu ambaye amekamatwa hadi sasa na
bado uchunguzi unaendelea kuwatafuta watu waliohusika na tukio hilo,” alisema
Mwambalaswa.
Alisema kuwa jeshi hilo linaendelea kufuatilia juu ya tukio
hilo na halitasita kumchukulia hatua kali za kisheria watu waliohusika na tukio
hilo la kusikitisha, marehemu alizikwa juzi na ameacha watoto wawili ambao ni
Ruben (14) anayesoma kidato cha kwanza St Anne na Kontrada anayesoma darasa la
sita shule ya Msingi Jitegemee Jijini Dar es Salaam.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment