Na Mwandishi Wetu, Kibaha
tweeterMWENDESHA
aliyetambulikia kwa jina moja la Omary (25) mkazi wa mtaa wa Lumumba wilayani
Kibaha mkoani Pwani amekutwa amekufa kwa kujinyonga kwenye mkorosho.
Akizungumza
na waandishi wa habari leo mjini Kibaha mwenyekiti wa mtaa huo Gidion Tairo
amesema kuwa tukio hilo
limetokea Julai 25 mwaka huu majira ya saa 2 asubuhi.
Tairo
amesema kuwa mwaili wake ulikutwa ukiwa unaninginia huku akiwa amejinyonga kwa
kutumia kamba ya Manila huku pembeni yake
kukiwa na chupa ya bia aina ya Safari.
Amesema
mwili huo uligunduliwa na moja ya majirani zake ambaye jina lake halikuweza
kufahamika mara moja amabaye alitoa taarifa kwake na yeye kuwasiliana na
polisi.
Aidha
amesema marehemu ambaye alikuwa akifanyia shughuli zake Kibamba CCM wilaya ya
Kinondoni Jijini Dar es Salaam kabla ya mauti kumkuta alikuwa haonekani
nyumbani na hakuonekana kuwa na matatizo yoyote.
Amebainisha
kuwa marehemu alikuwa akiishi kwenye nyumba na Roja Kwayu wa Jijini Dar es Salaam na ndiye
alikuwa akiisimamia nyumba hiyo.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo
kamanda wa polisi mkoani Pwani Ulrich Matei amesema kuwa marehemu hakuacha
ujumbe wowote.
Matei
amesema kuwa polisi wanaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo ili kujua nini chanzo cha kifo chake, na
mwili huo umehifadhiwa kwenye hospitali ya Tumbi kusubiri ndugu kwa ajili ya
mazishi, baada ya uchunguzi wa daktari.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment