Na John Gagarini, Kibaha
TATU Abdala (37) mkazi wa wilaya ya Rufiji mkoani Pwani anashikiliwa
na jeshi la polisi tuhuma za kumchoma kisu na kumwua mwanamke mwenzake kwa
madai kuwa alikuwa akitembea na mume wake Omary Abdala ambaye waliacha naye mwaka
mmoja uliopita.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamimu kamanda wa Polisi
mkoani Pwani Kamishana msaidizi wa Jeshi hilo Yusuph Ally alisema kuwa marehemu
alichomwa kisu hicho tumboni.
Ally alisema kuwa chanzo cha mauaji hayo kinatajwa kuwa ni
wivu wa kimapenzi baada ya kubaini kuwa mume wake wa zamani alikuwa na mahausiano
ya kimapenzi na marehemu baada ya wao kuachana.
“Mtuhumiwa huyo alitalakiana na mumewe ambaye walizaa naye
watoto watano naalipata taarifa ya mtalaka wake
kujenga mahusiano ya kimapenzi na marehemu Hajra kisha kumfuata
marehemu huyo nyumbani kwake na kumchoma kisu tumboni,” alisema Ally.
kujenga mahusiano ya kimapenzi na marehemu Hajra kisha kumfuata
marehemu huyo nyumbani kwake na kumchoma kisu tumboni,” alisema Ally.
Ally alibainisha kuwa mtuhumiwa alipata
urahisi wa kutenda tukio hilo kutokana na kuishi eneo la jirani na marehemu.
urahisi wa kutenda tukio hilo kutokana na kuishi eneo la jirani na marehemu.
Aidha alisema mara baada ya tukio hilo marehemu alikimbizwa
kituo cha afya cha
Muhoro na kabla ya kupatiwa matibabu alifariki dunia.
Muhoro na kabla ya kupatiwa matibabu alifariki dunia.
Aliongeza kuwa Mtuhumiwa
alikamatwa na polisi kujibu mashtaka yanayomkabili.
Mwisho
alikamatwa na polisi kujibu mashtaka yanayomkabili.
Mwisho
No comments:
Post a Comment