CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
Sunday, January 5, 2025
COREFA KUANDAA VIJANA KWENYE VITUO KILA WILAYA
COREFA KUANDAA VIJANA KUPITIA VITUO KILA WILAYA
CHAMA Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) kimesema kitahakikisha kila Wilaya inakuwa na kituo cha kuandaa vijana ili kuzalisha wachezaji watakaokuja kulitumikia Taifa.
VIONGOZI WA DINI NCHINI JAMHURI YA AFRIKA YA KATI WAISHUKURU JWTZ

Wakizungumza kwa nyakati tofauti mara baada ya kutembelewa na Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe wamesema uwepo wa JWTZ umekuwa na tija sana nchini humo kwani wamekuwa wakifanya kazi zao kwa weledi wa hali ya juu.
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Mkuu wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Berberati Mhashamu Koffi Denis, Karibu Mkuu wa Jimbo hilo Padre Jean Ancelimo amesema mbali na Ulinzi wa Amani pia limekuwa likitoa misaada mbalimbali ya hali na mali huku akitolea mfano wa ujenzi wa shule ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) ambayo imepewa jina la Serengeti.
Naye Askofu Mkuu wa Kanisa la Evenjeliko (AEC) Mhashamu Lucian Nday amesema uwepo wa JWTZ nchini hapo umewafanya waishi kwa amani na zaidi ya yote limewezesha ukuaji wa lugha adhimu ya kiswahili.
Sheikh Rashid Mohamoud Arouna ni Imam wa Masjid Nuur amesema JWTZ limekuwa mstari wa mbele kwenye kila jambo ambalo wanaombwa kutoa msaada kwa ajili ya kuhakikisha nchi yao inakuwa na amani.
Kwa upande wa Kamanda wa Kikosi cha Nane cha Ulinzi wa Amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati Luteni Kanali Theofili Nguruwe amewashukuru viongozi hao na kuahidi kutekeleza majukumu yake kwa weledi wa hali ya juu.
Saturday, January 4, 2025
JESHI LA POLISI MKOANI PWANI LIMEKAMATA WATU 173 KWA TUHUMA ZA MAKOSA MBALIMBALI
Monday, December 30, 2024
NYIKA MABINGWA MKOA WA PWANI
TIMU ya soka ya Nyika imefanikiwa kutwaa ubingwa wa Mkoa wa Pwani kwa kuifunga timu ya Kiduli kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa fainali wa ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa.
Saturday, December 28, 2024
JAMII YAWEZESHWA PEMBEJEO KILIMO CHA BUSTANI WILAYA YA KIBAHA
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi kuwezesha jamii kupitia kilimo cha bustani na kukabidhi pembejeo kwa vikundi hivyo Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Evelyn Ngwira kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha amesema kuwa mradi huo utakwenda kubadilisha maisha ya jamii kwenye Kata hiyo.