Thursday, December 12, 2024
NMB YAKABIDHI VIFAA VYA KUJIFUNGULIA NA MASHUKA HOSPITALI YA WILAYA YA RUFIJI UTETE
Sunday, December 8, 2024
MAFUNZO KWA VIONGOZI VIJANA KUTAIMARISHA VYAMA
ILI kuwa na vyama vya siasa imara na kuwa na serikali imara vyama hivyo vimetakiwa kuwa na mafunzo kwa viongozi vijana ili waendeleze maono ya waasisi wa vyama vya ukombozi Kusini mwa Afrika.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar Dk Mohammed Said Mohammed wakati wa akifunga Mafunzo ya 13 ya uongozi vijana kutoka vyama sita vya ukombozi Kusini mwa Afrika kuhusu masuala ya maendeleo kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Kibaha.
Mohamed amesema kuwa kuwekeza kwenye mafunzo kwa vijana itakuwa na vyama imara ambavyo vitajenga serikali zenye uwezo.
"Historia ya vyama hivi sita ni kuwa vinamshikamano wa kweli tangu enzi hizo kujenga ukombozi wa siasa kwa maono ya waasisi hivyo vijana hawa wanapaswa kurithishwa ili wawe viongozi bora,"amesema Mohamed.
Amesema kuwa ili kuleta ufanisi wa vyama na nchi yapaswa kuwekeza elimu na mafunzo kwa vijana ili kuleta mafanikio na yanategemea kwa kuwa na maono ya waasisi wa mataifa hayo.
"Mafunzo haya ni bora kwani yamezidi kuwandaa vijana kuwa viongozi bora wa baadaye kwa mustkbali wa vyama na nchi kwa ujumla,"amesema Mohamed.
Aidha amesema kuwa wanaishukuru nchi ya China kupitia Chama Cha Kikomunisti cha CPC ambacho kimekuwa kikivisaidia vyama hivyo sita rafiki na imesaidia Afrika kwenye sekta za afya usafiri, na viwanda.
"Wahitimu muwe kigezo cha kujenga masoko ya pamoja na masoko na nchi ya China ni muhimu sana kwani ushirikiano wa kibiashara kati ya nchi hizo ni kubwa pia tunashukuru chama cha CPC kwa kufadhili wa mafunzo haya,"amesema Mohamed.
Kwa upande wake Mkuu wa Shule hiyo ya Uongozi ya Mwalimu Nyerere Profesa Marcelina Chijoriga amesema kuwa mafunzo mbalimbali ya uongozi yamekuwa yakitolewa kwa vijana kupitia vyama hivyo.
Chijoriga amesema kuwa mafunzo hayo ni kuwaandaa vijana ili kuwa viongozi bora wa baadaye ambapo wanafundishwa juu ya masuala ya maendeleo na kujifunza maono ya viongozi ambao ni waasisi wa mataifa hayo kwa kushirikiana na CPC.
Mafunzo hayo siku 10 yaliwashirikisha viongozi vijana zaidi ya 100 kutoka vyama vya ANC-Afrika Kusini, CCM-Tanzania, FRELIMO-Msumbiji, MPLA-Angola, SWAPO-Namibia na ZANU-PF-Zimbabwe.
KIBAHA SHOPPING MALL YAZINDULIWA DC AWATAKA WANANCHI WASIENDE DAR ES SALAAM KILA KITU KIPO
MKUU wa Wilaya ya Kibaha Nickson John amezindua soko la kisasa (Kibaha Shopping Mall) lenye thamani ya shilingi milioni 8 ambalo litakuwa likiingizia Halmashauri ya Mji Kibaha kiasi cha shilingi milioni 660.7 kwa mwaka.
John amezindua soko hilo ambalo linamilikiwa na Halmashauri ya Mji Kibaha lipo kwenye eneo la kitovu cha Mji (CBD) amesema kuwa huo ni mradi wa kimkakati ambapo fedha za ujenzi zimetokana na fedha kutoka serikali kuu.
Amesema kuwa soko hilo ni mkombozi kwa wananchi wa Kibaha ambapo haitawalazimu kwenda Jijini Dar es Salaam kufuata bidhaa lakini bidhaa hizo zitakuwazikipatikana kwenye soko hilo ambalo limejengwa kwa miundombinu ya kisasa.
"Kuanzia sasa mtakuwa mnanunua hapa na hamtahitajika kufuata bidhaa Jijni Dar es Salaam hivyo mtapunguzagharama za nauli pamoja na muda ambao mneutumia kufuata bidhaa ambapo hapa zitapatikana kwa bei ya jumla na rejereja",amesema John.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa amesema kuwa mradi huo umeshakamilika na umeanza kazi ambapo kwa sasa uko kwenye kipindi cha matazamio.
Shemwelekwa amesema kuwa soko hilo lina sehemu mbalimbali ikiwa ni pamoja maduka 63, super market moja, kumbi za benki mbili, Atm mbili, eneo la kuchezea moja ni ya chakula mawili, eneo la kuangalia michezo moja, ukumbi wa mikutano mmoja, maegesho ya pikipiki 50, taxi 10, magari 100 na bajaji 30.
mwisho.
Friday, December 6, 2024
HALMASHAURI YA MJI KIBAHA KUZINDUA KIBAHA SHOPPING MALL
Akizungumza na waandishi wa habari Mjini Kibaha ofisa masoko wa soko hilo la kisasa Sabrina Kikoti amesema kuwa soko hilo limejengwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu na Halmashauri ya Mji Kibaha.
Kikoti amesema kuwa huduma zote zitapatikana ambaapo bidhaa zitauzwa kwa bei ya jumla na rejareja litafungua fursa kwa wananchi wa Kibaha na litatoa ajira na kufufua uchumi wa Kibaha.
“Mgeni rasmi kwenye ufunguzi huo anatarajiwa kuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John ambapo wananchi wa Kibaha wtaanufaika kwani walikuwa wakifuata bidhaa Jijini Dar es Salaam huku wengine watapata ajira kupitia biashara,”amesema Kikoti.
Naye ofisa mapato wa Halmashauri ya Mji Kibaha Luna Kakuru amesema kuwa jengo hilo la kibiashara lina maduka 74 ya biashara ambapo bidhaa zitauzwa kwa bei ya jumla na rejareja.
Kakuru amesema kuwa maratajio yao ni kukusanya kiasi cha shilingi milioni 660 kwa mwaka ambapo mapato yataendelea kuongezeka kutokana na kodi mbalimbali zitakazokuwa zikitozwa hapo ambapo wanapangisha mita za mraba kiasi cha shilingi 15,000.
Nao baadhi ya wafanyabiashara Charles Chandika amesema kuwa ametumi fursa kupangisha hapo ili aweze kufanyabiashara ambapo pia litachangamsha Mji wa Kibaha ambapo lengo ni kuhakikisha wanatoa huduma bora na za kisasa na kuwafikia wananchi.
Chandika amesema kuwa bei watakayouza ni rafiki na hawatakuwa na sababu ya kwenda mbali kuzifuata Jijini Dar es Salaam kwani wataokoa muda na gharama za nauli kufuata bidhaa mbali.
Naye Lydia Vicent ambaye amenufaika kwa kuchangamkia fursa ambapo alikosa sehemu ya kufanyia biashara na wanampongeza Rais kwa kuwapatia fursa wafanyabiashara ambapo fedha zilizotolewa na serikali zimefanikisha kujenga soko hilo.
Vicent amesema kuwa soko hilo litafungua fursa za kibiashara kwa wananchi wengi ambapo ni sehemu ya kukuza uchumi kwa mwananchi mmoja mmoja na Watanzania kwa ujumla.
WAOMBA MABORESHO YA BARABARA YA MOROGORO KUPUNGUZA FOLENI KIBAHA
WAJUMBE wa Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Pwani wameiomba serikali kuhakikisha uboreshaji wa Barabara ya Morogoro ili kupunguza msongamano uliopo kwa sasa ambapo asilimia 85 ya magari kwenda nje ya Dar es Salaam yanapita barabara hiyo.
Wakizungumza kwenye kikao cha bodi ya barabara
kilichofanyika Mjini Kibaha Mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema
kuwa kwa sasa kuemkuwa na foleni kubwa sana ambayo imekuwa ni changamoto kubwa
kwa magari yanayotumia barabara hiyo.
Koka alisema kuwa mipango inayotarajiwa kufanywa ifanyike
kwa haraka ili kukabiliana na hali hiyo ambayo imekuwa ni kero kubwa kwa
watumiaji kwani foleni imekuw ani kubwa sana na kusababisha watu kushindwa
kwenda kwa wakati kwenye shughuli zao.
“Tunashauri mpango wa uboreshaji uendane na ukuaji wa Mji wa
Pangani na eneo la Shirika la Elimu (KEC) ni maeneo ambayo yatakuwa na
uboreshaji mkubwa hivyo uboreshaji huo uzingatie maeneo hayo kupitia mpango
endelevu wa uboreshaji barabara,”alisema Koka.
Alisema kuwa katika mpango endelevu huo wa uboreshaji
barabara pia uangalie kwa kuwa na barabara za juu na vivuko au madaraja kwa
ajili ya watu kuvuka na eneo ambalo linapaswa kufanyiwa kazi ni kuanzia Mizani
ya zamani hadi Kwamathias.
“Pale Picha ya Ndege na Mkuza nako ni kipaumbele kwa kuwa
ndiyo kwenye maungio napo papewe kipaumbele wakati wa mpango endelevu wa
uboreshaji wa barabara zetu kwani mji wetu kwa sasa umekuwa na magari ni mengi
sana,”alisema Koka.
Naye Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Muharami Mkenge alisema
kuwa barabara hiyo ya Morogoro ni changamoto kubwa sana hivyo inapaswa
iangaliwe kwa ukaribu ili kupunguza kero hiyo ya msongamano wa magari ili
wasafiri waweze kwenda safari zao kwa wakati.
Mkenge alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo hivyo kuna
haja ya kuboresha barabara zingine ikiwa ni pamoja na ile ya Makofia Wilayani
Bagamoyo hadi Mlandizi Wilayani Kibaha yenye urefu wa kilometa 35 itasaidia
kupunguza msongamano kwani magari yanaweza kupita huko kama barabara ya
Morogoro kuna foleni kubwa.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge
alisema kuwa kuwe na maombi maalumu ambayo yatakuwa ni vipaumbele kwa ajili ya
kuwaondolea kero ya wananchi kwani barabara ni kiungo muhimu cha maendeleo.
Kunenge alisema kuwa mahitaji ya barabara kwa Mkoa ni
makubwa lakini changamoto iliyopo ni upatikanaji wa fedha hivyo ni vema kukawa
na vipaumbele ili vianze na baadaye kufuatiwa na mahitaji mengine.
Kwa upande wake meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Pwani Mhandisi Baraka Mwambage amesema mpango uliopo ni uboreshaji wa barabara za zamani na upanuzi wa maeneo yenye msongamano wa magari.
Mwambage amesema kuwa kwa upande wa barabara ya zamani ya kuanzia Sheli mpaka DAWASA wamefanya kazi za matengenezo kwa kuchonga barabara, kuweka kifusi cha udongo na changarawe,upanuzi wa maingilio yote mwanzo na mwisho ikiwa ni pamoja na kuongeza urefu wa makalavati yaliyopo, kujenga mitaro ya zege na kuchimba mitaro ya kawaida.
Amesema katika kipande cha Picha ya Ndege-Msufini kazi zilizofanyika ni pamoja na kuchonga barabara, kuweka kifusi cha changarawe na kujenga makalavati.
Aidha ukarabati wa Barabara ya zamani ya Morogoro umefanyika kuanzia Mlandizi-Ruvu JKT, TRC Relini-Mzunguko wa Vigwaza na upanuzi wa maeneo ya miji kwa Barabara kuu ya Morogoro umefanyika eneo la Kwa Mwarabu mita 350, TANESCO mita 290 na Chalinze mita 850 ili kupunguza msongamano kwa eneo la kuingia mji wa Chalinze.
Mwisho.
MAFIA WALILIA BOTI ZA MWENDOKASI
Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Halmashauri ya Mafia Juma
Ally kwenye kikao cha bodi ya barabara ya Mkoa wa Pwani kilichofanyika Mjini
Kibaha.
Ally lisema kuwa wanaishukuru serikali kuwapatia boti kwenda
Mafia lakini boti hiyo hutumia masaa mengi ambapo ni kati ya masaa sita au saba
tofauti na boti zinazoenda Zanzibar ambazo hutumia nusu ya masaa hayo.
“Usafiri tunaotumia unasaidia lakini ungeboreshwa kwa kupata
boti ambazo zinatumia injini badala ya hizoi ambazo zinatumia kasi ili tusafiri
kwa haraka tofauti na ilivyosasa,”alisema Ally.
Alisema kuwa boti hizo za sasa zinatumia pangaboi lakini
tunashauri tupatiwe zile ambazo ni jeti ambazo mwendo wake ni wa kasi.
“Tukipata boti za mwendo kasi hata watalii wataongezeka
lakini kwa sasa wtaalii ni wachache kwani tunapata watalii 10,000 lakini
usafiri huo ukipatikana wataongezeka na tutakuwa na watalii wengi hivyo
kuongeza mapato ya Halmashauri yetu,”alisema Ally.
Aidha alisema kuwa kutokana na kutokuwa na boti hizo za
mwendokasi kabla ya kufanya safari lazima kuwe na maji mengi jambo ambalo ni
changamoto kubwa lakini ingekuwa boti za kasi zingefanya safari tu bila ya
kusubiri maji kuwa mengi.
“Ombi letu lingine tunaomba Bandari ya Kisiju Wilayani
Mkuranga iboreshwe ili itumika kwani kula ni rahisi tofauti na Bandari ya
Nyamisati iliyopo Wilayani Kibiti hilo nalo tunaomba lifanyiwe kazi kikubwa ni
kurahisisha usafiri wa wakazi wa Mafia,”alisema Ally.
Kwa upande wake mkuu wa Mkoa wa pwani akitoa ushauri alisema
kuwa jambo kubwa ni kuangalia maslahi mapana ya wananchi hivyo miradi
mbalimbali izingatie vipaumbele kutokana na maeneo na vitakavyoendana na
vipaumbele vya Rais.
Kunenge alisema kuwa wajumbe wanapaswa kuangalia vipaumbele
kwa uhalisia kwani fedha ni ndogo hasa ikizingatiwa nchi ilfanya uchaguzi ambao
umetumia gharama kubwa hivyo kuwe na vipaumbele katika utekelezeji wa miradi.