KUNDI la Whatsapp la Kibaha Huru Fikra Huru limetoa msaada wa madawati 30yenye thamani ya shilingi milioni tatu ili kusaidia wanafunzi ambao wanakabilia na upungufu wa madawati kwenye Shule za Msingi za Halmashauri ya Mji Kibaha.
Friday, April 19, 2024
KUNDI LA KIBAHA HURU FIKRA HURU LATOA MADAWATI 30
Tuesday, April 16, 2024
WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI YAONGEZA MELI ZA UVUVI BAHARI KUU
Na Wellu Mtaki, Dodoma
Wizara ya Mifugo na Uvuvi kupitia Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu (Deep Sea Fishing Authority-DSFA) imefanya maboresho katika kanuni za Sheria Uvuvi wa Bahari Kuu na kupandisha utoaji wa vibali vya uvuvi katika Bahari Kuu kutoka meli tisa mwaka 1988 hadi meli 61 mwaka 2023/24 kwa ajili ya kufanya uvuvi katika Ukanda wa Uchumi wa Bahari (EEZ) upande wa Tanzania.
Hayo yamesemwa Leo Tarehe 16 Aprili 2024 na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Abdallah Ulega wakati akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Muungano kuelekea maadhimisho ya miaka 60.
Ameeleza kuwa DSFA imeingia mkataba na Kampuni ya Albacora ya nchini Hispania kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kuchakata samaki katika Mkoa wa Tanga na kitakuwa na uwezo wa kuchakata tani 20 za samaki kwa siku, kuhifadhi tani 2,400 za samaki na kuajiri wafanyakazi zaidi ya 100.
Pia amesema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imepanga kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi kukitumia Kituo cha Ukuzaji Viumbe Maji cha Machui – Tanga kupata vifaranga vya samaki na viumbe maji wengine wakiwemo jongoo bahari kwa ajili ya kuendeleza uchumi wa buluu.
Aidha, zaidi ya wananchi milioni 4.5 wanakadiriwa kupata kipato chao cha kila siku kutokana na shughuli za Uvuvi, zikiwemo kuunda na kutengeneza boti, kushona nyavu, biashara ya samaki na mazao yake pamoja na Baba na Mama lishe.
Ikumbukwe kuwa sekta ya uvuvi ni miongoni mwa sekta tatu za Kilimo ambazo zinaajiri wananchi wengi na imeweza kutoa ajira za moja kwa moja kwa wavuvi 198,475 na wakuzaji viumbe maji wapatao 35,986.
SERIKALI YATOA BILIONI 696.7 KUPUNGUZA UMASKINI
SERIKALI imetoa shilingi bilioni 696.7 kwa ajili ya kupunguza na kuondoa umaskini kwa kaya milioni 1.3 kwenye vijiji na mitaa.
Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora George Simbachawene wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya wizara hiyo yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 60 ya Muungano.
Simbachawene amesema kuwa lengo la Serikali ya awamu ya sita na awamu zilizopita zinazoongozwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni kupunguza na kuondoa umaskini wa kipato.
Amesema Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) ulianzishwa na serikali mwaka 2000 kama mojawapo ya mikakati ya kupambana na umaskini kwa kutumia dhana ya ushirikishaji jamii.
"Jumla ya miradi 1,704 ya huduma za jamii yenye thamani ya shilingi bilioni 72 ilitekelezwa kupitia mpango huu wa TASAF awamu ya I awamu hii ilitekelezwa kwa mafanikio makubwa katika kuwapatia wananchi huduma muhimu za kijamii katika sekta mbalimbali zikiwemo za maji, elimu, miundombinu na afya,”amesema Simbachawene.
Simbachawene amesema awamu ya Pili ya TASAF ilianza utekelezaji mwaka 2005 hadi 2013 katika Halmashauri zote za Tanzania Bara na wilaya zote za Tanzania Zanzibar.
Amefafanua kuwa jumla ya miradi 12,347 ya huduma za jamii yenye thamani ya shilingi bilioni 430 ilitekelezwa wakati wa Awamu hii ya Pili ya TASAF (TASAF II).
Amesema katika miaka 60 ya Muungano, serikali inayoongozwa na Rais, Dk. Samia Suluhu Hassan inaendelea kutekeleza jitihada za kuzuia na kupambana na rushwa ili wananchi waweze kupata huduma bora.
Aidha amesema kuwa TAKUKURU kwa kutambua kuwa Skauti ni suala la Muungano kwa kushirikiana na Mamlaka ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu Uchumi Zanzibar (ZAECA) ziumeunda timu ya uratibu ya kitaifa yenye Wajumbe kutoka Chama cha Skauti Tanzania (CST), ZAECA na TAKUKURU ili kuimarisha ushirikiano katika jitihada za kupambana na rushwa.
Pia amesema Ushirikiano huu ni muhimu sana kwa ustawi wa Taifa kwa kuwa Skauti wapo katika kundi la vijana na ni “Jeshi kubwa” ambalo tumeshuhudia likitoa mchango chanya katika matukio mbalimbali ya kijamii na kitaifa.
WANAOTUKANA VIONGOZI KUCHUKULIWA HATUA ZA KISHERIA
Sunday, April 14, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI YATOA SHUKRANI KWA CHUO CHA VETA MKOA WA PWANI KUWAPATIA USAFIRI KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA 102 KUZALIWA KWA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA DODOMA
Katibu wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani ndugu Omary Abdul Punzi kwa niaba ya uongozi ameshukuru chuo cha Veta Pwani kupitia Mkuu wa chuo hicho Madam Crala Kibodya kuwezesha safari hiyo kwa kutoa usafiri wa Coaster.
Ndugu Omary Punzi amesema huo ni uzalendo mkubwa kawa wadau nchini wasisite kusaidia katika shughuli nyingine.
Maadhimisho hayo yaliyofana yaliyohudhiliwa na Wananchi wengi wanafunzi na makundi mengine Mgeni Rasmi alikuwa Mheshimiwa Dkt Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
MWAKILISHI WA BALOZI WA UGANDA YAPONGEZA UBUNIFU WA TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU JULIUS KAMBARAGE NYERERE MKOA WA PWANI
Akipokeaa Tshirt hizo yeye na mke wake katika maadhimisho hayo ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere lililofanyika katika Ukumbi wa Mji wa Mtumba Mkoani Dodoma tarehe 13.4.2024
MEJA JENERALI BALOZI ANSELM BAHATI SHIGONGO ATUMA SALAMU ZA MKOA WA PWANI KONGAMANO LA MIAKA 102 YA KUZALIWA KWA MWALIMU NYERERE DODOMA

Mh Meja Jenerali Balozi Bahati ameyasema hayo katika maadhimisho ya kitaifa ya miaka 102 ya kuzaliwa kwa Mwl Julius Kambarage Nyerere yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mtumba Mjini Dodoma tarehe 13.4.2024 maadhimisho hayo yalihudhuliwa na Mh Daktari Philip Mpango Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Amewaomba wadau wa maendeleo nchini waende Mkoani Pwani kwa ajili ya uwekezaji wa viwanda na shughuli mbalimbali za kimaendeleo.