Sunday, February 4, 2024
LIKUNJA CUP ROBO FAINALI KUTIMUA VUMBI FEBRUARI 7
MAashindano ya Likunja Cup hatua ya Robo Fainali yataanza kutimua vumbi Februari 7 uwanja wa Shule ya Msingi Zegereni kwa kuzikutanisha Misugusugu Fc na Veterani Fc kwa mujibu wa Rashid Likunja
ATAKA MIKOPO ASILIMIA 10 YA HALMASHAURI IKOPESHE VIJANA WALIOACHA MATUMIZI DAWA ZA KULEVYA
HUKU Serikali ikiendelea na mchakato wa namna ya utoaji mikopo ya asilimia 10 za Halmashauri imeombwa kuangalia namna ya kuvikopesha vikundi vya waraibu wa dawa za kulevya ili wafanye shughuli za ujasiriamali.
HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA YAIKOSHA KAMATI YA BUNGE KWA UBORA WA HUDUMA
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI imeipongeza menejimenti na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa kwa ubora wa Huduma na kuwatia moyo kwa kuendelea kuwahudumia wananchi .
Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Afya na Maswala ya UKIMWI, Mhe. Stanslaus Nyongo baada ya kupokea taarifa ya Huduma za kibingwa na bingwa bobezi zinazotolewa katika Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa iliyopo Jijini Dodoma.
Mhe. Nyongo amesema kuwa Hospitali hiyo imekuwa ya mfano katika utoaji wa Huduma bora na usafi wa mazingira na kuleta ufanisi sahihi wa uwekezaji mkubwa ulofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Sluhu Hassan.
“Hongereni kwa kazi nzuri mnayofanya ya kuwahudumia watanzania lakini pia Mkurugenzi husisite kutuma kutuma vijana wako kuendelea kujifunza ili Tanzania tuzidi kuwa kivutio cha tiba Utalii Afrika mashariki na Afrika nzima kwa ujumla”, Amesema Mhe. Nyongo.
Vile vile ametoa wito kwa uongozi huo kwendelea kuwa wabunifu katika kuongeza mapato ya hospitali hiyo ili kujiimarisha zaidi kiuchumi na kuacha kuwa tegemezi kwa serikali kuu.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Benjamin Mkapa, Dkt. Alphonce Chandika ameishukuru serikali chini ya uongozi imara wa Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa alioufanya katika Hospitali hiyo hususani katika vifaa tiba na vitendanishi, kusomesha wataalamu na upatikanaji wa dawa kwa wakati.
Saturday, February 3, 2024
TAASISI YA KUMBUKUMBU YA MWALIMU NYERERE YATEMBELEA BUNGENI
Taasisi ya kumbukumbu ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Mkoa wa Pwani yatembelea Bungeni Tarehe 2.2.2024 Kwa Mwaliko wa Mhe Subira Mgalu Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Pwani Kwa lengo la Kujifunza Shughuli za Bungeni.
Katibu wa Taasisi hiyo Mkoa wa Pwani Ndugu Omary Punzi Kwa niaba ya Taasisi alitoa Shukrani Kwa Mbunge Subira Mgalu Kwa namna alivyoipokea Taasisi na kuheshimu sambamba na hilo alipongeza Juhudi za Serikalini ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Daktari Samia Suluhu Hassani namna Bunge lilivyokuwa linafanya kazi Vizuri Kwa uchangamfu sana na Kujibu hoja vizuri
Thursday, February 1, 2024
AMEND TANZANIA LATOA MAFUNZO KWA MAOFISA USAFIRISHAJI.
Shirika la AMEND Tanzania ambalo linajihusisha na masuala ya kutoa elimu kwa wananchi kuhusu usalama barabarani limeweza kutoa elimu na mafunzo kwa maafisa wasafirishaji wa vituo tofauti katika jiji la Dodoma.
Shirika hilo ambalo lipo chini ya ufadhili wa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania limeweza kutoa elimu na mafunzo kwa maafisa wasafirishaji maarufu kwa jina la bodaboda kwa malengo ya kudhibiti wigo ajali barabarani pamoja na kuwapa mafunzo mbali mbali pamoja na utumiaji wa alama za barabarani ambazo zimekuwa zikipuuzwa na maafisa wasafirishaji hao.
Nuhu Toyi ambaye ni balozi wa mafunzo na afisa msafirishaji kutoka kituo cha UDOM jijini Dodoma amesema alibaatika kupata mafunzo ambayo yametolewa na shirika la AMEND Tanzania na kupitia mafunzo hayo yameweza kumsaidia kuendesha chombo chake kwa kujihamini bila kusababisha ajali.
“Pongezi za dhati ziende kwa Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania hususan kitengo cha afya kinachofadhiliwa na miss Vivian kwa kutambua umuhimu wa kundi hili la vijana wa bodaboda wengi ni vijana ambao tupo kati ya umri wa miaka 25. Kazi hii wengi tumekuwa tukiifanya kwa mazoea na hatuna elimu kwaio wengi tumekuwa ni wahanga wa kusababisha au kusababishiwa ajari kwasababu ya kukosa elimu barabarani lakini Ubalozi wa Uswisi nchini Tanzania umeona itakuwa ni vyema kama vijana hawa ambao ni taifa la kesho na nguvu kazi ya taifa wasiweze kudhuulika na ajali” alisema Toyi.
Kwa upande wake afisa usafirishaji, Laurenti Mayowa amesema alikuwa haelewi alama za barabarani lakini kupitia mafunzo hayo wamepokea kutoka shirika la AMEND Tanzania kwani limekuja kitofauti katika kutoa mafunzo yao kwani wamefundishwa kwa nadharia pamoja na vitendo.
“Tulipata mafunzo mazuri sana kwenye swala la uendeshaji wa pikipiki lakini pia tumeweza kufundishwa namna ya kutumia barabara lakini pia namba ya kutumi vyombo vyetu, kwa kweli mafunzo yalikuwa mazuri nimejifunza mambo mengi na mazuri na kabla ya mafunzo nilikuwa sielewi kwamba barabarani nilikuwa naendesha hovyo hovyo tu na baada ya mafunzo nashukuru mpaka sasaivi nime elewa na tulikuwa wengi sana tukifundishwa awamu kwa awamu nafikiri bodaboda takriban 230 au 250 kwa Dodoma hapa na sasahivi wame elimika”, alisema Mayowa.
Alisema alama za barabarani ilikuwa ni changamoto kwa madereva wengi , walikuwa wanaziona lakini wanashindwa kuzitumia kama ipasavyo na walidhani ni michoro tu lakini baada ya mafunzo waliweza kuelewa aina za michoro na alama zinazotumiwa barabarani.
“Tulifundishwa kuna alama za onyo, alama za amri, kuna alama za maelekezo kwaio hayo yote tumefundishwa lakini pia nimefundishwa alama nyengine ambazo nilikuwa sizielewi vizuri kama alama za michoro juu ya sakafu ya barabara hizo nazo nilikuwa sizielewi nilikuwa naona tu michoro na sielewi maana yake lakini baada ya elimu nimevielewa vizuri” alisema Mayowa
Aidha alisisitiza kwa maafisa usafirishaji kubadilika na kuwa na mahudhurio mazuri ya mafunzo yanayotolewa na shirika la AMEND Tanzania kwasababu yanafundishwa kwa vitendo pamoja na kutii sheria za barabarani.
“Tumefundishwa dereva kujihami kwaio wale ambao hawajapata mafunzo hawezi kuelewa na kutii sheria akiwa yupo barabarani na anaweza kusababisha ajali kwasababu anakuwa hana uelewa wowote na vigumu kujilinda anapotumia chombo chake”,Mayowa.
Naye afisa usafirishaji kutoka kituo cha Ndasha,Bw. Ally Rashid Ally alisema kuwa bodaboda ni ajira kama zilivyo ajira nyengine na imeteka soko kubwa la ajira kwa vijana kwenye upataji wa kipato na awali haikupewa thamani kama zilivyo biashara nyengine.
Amesema wamekuwa na madereva usafirishaji wengi lakini baadhi yao kwenye kundi hilo hawana elimu ya kutosha ya barabarani na kutambua alama zilizomo.
Aidha Bw. Ally amesema elimu iliyotewa ni msaada mkubwa kwa maafisa usafirishaji mkoani Dodoma kwani wengi wao wamekuwa na nidhamu iwapo wanatumia vyombo vyao barabarani na changamoto za ajali na vifo vimeweza kuepukika kutokana na maarifa waliopokea kutoka kwa wakufunzi kupitia shirika la AMEND Tanzania.
WIZARA YA KATIBA NA SHERIA KUENDELEA KUWEKA MIUNDOMBINU YA TEHAMA
Wizara ya katiba na Sheria imeendelea kusimamia uwekaji wa mifumo na miundombinu ya TEHAMA thabiti ili kuhakikisha wananchi wote wanafanikiwa na huduma za kisheria na wanafikiwa vizuri ikiwemo kupata elimu ya masuala ya sheria.
Hayo yameelezwa leo Januari 30,2024 jijini Dodoma na Waziri wa Katiba na Sheria Balozi Dkt.Pindi Chana wakati akikabidhi vifaa vya TEHAMA kwa taasisi za haki jinai.
"Masuala ya sheria ni vizuri wananchi nao wakayajua, uendeshaji wa kesi,upatikanaji wa nyaraka za kesi na ushahidi hukumu na maamuzi ya kesi na uwepo wa vyombo vya utoaji haki katika ngazi za jamii"Amesema
Aidha amesema serikali imejidhatiti katika kuimarisha masuala ya utoaji na upatikanaji wa haki nchini
"Kama alivosema katibu Mkuu unapochelewesha haki ni kama mtu ananyimwa haki,nisingependa tuwe wacheleweshaji wa haki hizo"
Hata hivyo ameongeza kuwa taasisi za haki jinai zimejenga mifumo mizuri ya TEHAMA ambayo inarahisisha upatikanaji wa taarifa na huduma za kisheria kwa wananchi,kwa Wakati bila urasimu na kuepusha rushwa.
"Uwepo wa mifumo ya TEHAMA na matumizi ya teknologia utawapunguzia wananchi muda na gharama za kushughulikia masuala ya kisheria na badala yake watajikita zaidi katika shughuli za Kiuchumi na maendeleo"
Awali akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bi.Mary Makondo ameeleza Kuwa mradi huu umelenga kuimarisha matumizi na fursa za TEHAMA nchini ili kurahisisha upatikanaji wa haki
Pia kuimarika kwa matumizi ya TEHAMA kunawezesha kuziunganisha taasisi za haki jinai katika mfumo mmoja wa kielectronic katika kuwasiliana kiutendaji na hivyo kuimarisha ubora na upatikanaji wa huduma za kisheria zinazotolewa na taasisi hizi
"Tangu kuanziashwa kwa mfumo huu Kazi zifuatazo zimetekelezwa ikiwa ni pamoja na upembuzi yakinifu wa mahitaji ya sekta ya sheria pamoja na haki jinai kuelekea haki mtandao,vile vile ujenzi wa miundombinu ya TEHAMA kwenye jengo la Wizara"Amesema
Aidha ameeleza Kuwa Wizara inaendelea kutumia fursa ya TEHAMA kwa kushirikiana na taasisi za serikali pamoja na wadau katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na kwa wakati.
Kwa upande wake Mkurugenzi mkuu wa Mashitaka nchini(DPP) Sylvester Mwakitalu akitoa salaam fupi za ofisi yake amesema ofisi ya Mashitaka imefarijika kupokea vifaa hivyo na vitawasaidia katika kuboresha utendaji wao wa kazi na katika kuwahudumia watanzania
Aidha tunaamini vifaa hivi vitatusaidia katika kuhakikisha kwamba haki za wananchi tunaowahudumia zinapatikana kwa wakati
Naye Mkuu wa Gereza la Msalato SSP Flavian Justine ameeleza Kuwa vifaa hivyo kwao ni muhimu kwa kuhifadhi taarifa za wahalifu,lakini pia kwa kurahisisha taarifa za mawasiliano kati ya magereza na mahakama na kuipunguzia serikali gharama za kusafirisha wahalifu kuhudhuria mahakamani.
WANANCHI WAJITOLEA KUJENGA OFISI YA MTAA ZEGERENI
WAKAZI wa Mtaa wa Zegereni Wilayani Kibaha Mkoani Pwani wamejitolea kujenga ofisi ya kisasa ya Mtaa ili kuboresha utoaji huduma kwa wananchi.