Saturday, October 7, 2023

NSSF PWANI YAWA YA TATU KITAIFA UTOAJI HUDUMAFA

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoani Pwani, umeshika nafasi ya tatu kitaifa katika utoaji huduma kwa ufanisi kwa wateja wake.

Aidha mfuko huo umeahidi utendaji kazi unaoendana na kasi ya Nssf ya sasa ambayo inahitaji ujali kwa wateja na kutoa huduma bora.

Kaimu Meneja NSSF Pwani Rehema Mutungi akifunga maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja kimkoa, alieleza utoaji huduma bora kwa wateja wao ni jadi yao na imeonyesha dhahiri nafasi waliyoipata kitaifa.

"Tunahitaji kufika namba moja ,huu ni utamaduni wetu kuhudumia wateja kwa ubora na kwa wakati ,tunaamini miaka ijayo tutafanya vizuri zaidi"alieleza Rehema.

Rehema anasisitiza ushirikiano,umoja kwa watumishi na watendaji wa NSSF ili kutoa huduma kwa ufanisi.

Vilevile Rehema alihimiza ,kila mmoja kujitathmini na kuchukua hatua za haraka kukabiliana na vitendo vya rushwa ili kudumisha imani kwa wanachama na wadau.

Katika kufunga maadhimisho hayo kimkoa wametoa vyeti na zawadi kwa wa

Friday, October 6, 2023

MKOA WA PWANI KUBORESHA MAZINGIRA YA UWEKEZAJI

SERIKALI ya Mkoa wa Pwani kwa kushirikiana na Serikali Kuu itahakikisha miundombinu muhimu inayotumika kwenye maeneo ya uwekezaji inajengwa ili kuwaondolea usumbufu wawekezaji.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge alipotembelea kiwanda cha King Lion Investment (King Lion Steel Mill) kinachojihusisha na utengenezaji wa bidhaa za chuma kilichopo eneo la viwanda la Zegereni Wilayani Kibaha.

Kunenge amesema kuwa serikali inatekeleza miradi mbalimbali kwenye maeneo ya uwekezaji ikiwemo ya Barabara, Umeme, Maji na Gesi ili kuvutia uwekezaji.

Kwa upande wake meneja wa kampuni hiyo Arnold Lyimo amesema kuwa mradi huo unagharama ya zaidi ya shilingi bilioni 160 na kitakuwa kiwanda kikubwa kwa ukanda wa Afrika Mashariki na utakamilika Juni 2024 na kuanza uzalishaji.

Lyimo amesema kuwa kitakapokamilika kitazalisha chuma tani 350,000 kwa mwaka ambapo malighafi za kuzalishia chuma na zitauzwa ndani na nje ya nchi zikiwemo Uganda, Kenya, Rwanda, Burundi, Kongo na kitatoa ajira 400 za moja kwa moja 5,000 ajira za muda.

Thursday, October 5, 2023

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA PWANI LATOA TAHADHARI MVUA ZA EL NINO

 

*TAARIFA YA KAMANDA WA ZIMAMOTO PWANI ALIPOKUWA MGENI RASMI MAHAFALI YA 16 SHULE YA SEKONDARI KWALA - KIBAHA*

KAMANDA wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Pwani SSF Jenifa Shirima kuwakumbusha wananchi  kuzingatia tahadhari zinazoendelea kutolewa kuhusu uwezekano wa kunyesha mvua kubwa za Elninyo.

Shirima ameyasema hayo alikpokuwa mgeni rasmi Mahafali ya 16 ya Kidato cha nne katika Shule ya Sekondari  Kwala iliyopo Kata ya Kwala Wilaya Kibaha na kuwataka watu wote wanaoishi maeneo hatarishi kuondoka kabla ya mvua hizo kuanza kunyesha ili kuepuka madhara.

Aidha amewaahidi kwamba atahakikisha changamoto walizoainisha atazifikisha sehemu husika ili ziweze kupatiwa ufumbuzi ambapo alitoa mchango wake fedha taslimu, vifaa vya kuzima na kung’amua moto kwa uongozi wa shule hiyo.

Pia alitoa zawadi za vifaa vya ki taaluma kwa wanafunzi wahitimu na Wanafunzi Skauti ambapo alipata nafasi ya kugawa vyeti kwa wahitimu pamoja na walimu na wanafunzi waliofanya vizuri zaidi.

NSSF YAPIGA VITA VITENDO VYA RUSHWA

MFUKO wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Mkoani Pwani, imetoa rai kwa Mtumishi ama Mtendaji yeyote anaejihusisha na vitendo vya rushwa kuacha mara moja vitendo hivyo kwani vinachangia kuzorotesha utoaji wa huduma kwa wateja.

Akifungua maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja kimkoa, Meneja wa NSSF Mkoani Pwani, Witness Patrick ,amesema wanashirikiana na Taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa (TAKUKURU) kudhibiti mazingira ya vitendo vya rushwa kwenye maeneo ya kazi.

Amewaasa ,kila mmoja kujitathmini na kuchukua hatua za haraka kukabiliana na vitendo vya rushwa ili kudumisha imani kwa wanachama na wadau.

Witness ameeleza kuwa, mfuko hautamvumilia mtendaji yeyote atakaeshindwa kuendana na viwango na kasi ambayo mfuko unatarajia kuifikia.

Anasema, Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan inapinga rushwa kwa vitendo, na Nssf inaunga mkono juhudi hizi za serikali kwa kukemea masuala yote ya rushwa.

Vilevile Witness amewahimiza ,watumishi na wananchi wema kutoa taarifa za vitendo vya rushwa vinavyotendeka katika maeneo yao ya kazi kwani kutokutoa taarifa ni kushiriki rushwa.

Halikadhalika," anawasihi kutumia mfumo mpya wa NISS katika kuandikisha wanachama wengi zaidi wa mfumo wa kujichangia kwa hiari ili kuongeza wigo wa kinga ya Hifadhi ya Jamii kwa wananchi.

Naye mwanachama wa Nssf Kibaha, Vicent Ndumbili ameipongeza Nssf kwa kujali wateja wake.

Maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja ilianzishwa rasmi kimataifa mwaka 1984 kwa lengo la kutambua umuhimu wa huduma bora kwa wateja na juhudi za wafanyakazi wanaotoa huduma bora kwa wateja ambapo mwaka huu 2023 yanaanza octoba 2-octoba 6 kilele.


Mwisho

TCCIA INVESTMENT KUONGEZA MTAJI KUFIKIA BILIONI 47


KAMPUNI ya TCCIA Investment inatarajia kuongeza mtaji wake na kufikia bilioni 47 kutoka bilioni 37 ambazo zimewekezwa kwenye masoko mbalimbali ya hisa.

Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Peter Kifungomali wakati akizungumza na wanahisa wa mkoa wa Pwani juu ya hisa walizowekeza.

Kifungomali amesema kuwa ongezeko hilo ni hadi itakapofika mwaka ujao wa fedha ambapo thamani imeongezeka kwa asilimia 53 kwa mwaka 2022.

Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara ya TCCIA Mkoa wa Pwani sehemu ya biashara Fadhili Gonzi amesema kuwa baadhi ya wanahisa walikuwa na maswali mengi juu ya fedha zao.

Naye mmoja wa wanahisa Ayubu Mtawazo amesema kuwa hisa ni moja ya sehemu salama ya kuwekeza fedha ambapo watu wengi wamenufaika.

Clara Ibihya amesema kuwa manufaa ya hisa ni makubwa kwani ukishawekeza fedha zako hupati tena usumbufu kutakiwa marejesho bali unasubiri kupata fedha.


Thursday, September 28, 2023

SHULE BORA YAWAJENGEA UMAHIRI UFUNDISHAJI SOMO LA HISABATI

KATIKA kuhakikisha wanafunzi wa shule za msingi wanapata uelewa wa somo la hisabati Mkoani Pwani Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia na Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia program ya Shule Bora imewapatia mafunzo walimu wa somo hilo.

Akizungumza Wilayani Kisarawe baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa viongozi wa elimu kuhusu uboreshaji ufundishaji na ujifunzaji wa umahiri wenye changamoto katika somo la hisabati Ofisa elimu Mkoani humo Sara Mlaki amesema kuwa mafunzo kwa walimu hao yatawajengea uwezo ili kupata mbinu bora za umahiri za ufundishaji wa somo la hisabati.

Aidha mafunzo hayo yameandaliwa na Ofisi ya Rais (TAMISEMI) kwa kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia pamoja na Taasisi ya Elimu Tanzania kupitia Program ya Shule Bora ambayo inatekelezwa katika mikoa tisa ya Tanzania Bara kwa Ufadhili wa Serikali ya Uingereza na kwa Usimamizi wa Cambridge Education.

Mafunzo hayo yaliendeshwa na  wawezeshaji kutoka vyuo vya Ualimu vya Tukuyu  na Mpwapwa ambapo washiriki wa  mafunzo hayo ni viongozi wa Elimu kutoka katika ngazi ya Mkoa  wakiwemo Walimu, Walimu  wakuu, Maofisa Elimu Kata, Maofisa Elimu Awali na Msingi kutoka katika Halmashauri tisa na shule teule za Wilaya ya Kisarawe.

Wednesday, September 27, 2023

SHULE SALAMA WAJADILI KUMLINDA MTOTO


WANAFUNZI 42,000 kwenye Halmashauri ya Mji Kibaha watafikiwa na mpango wa Shule Salama wenye lengo la kuhakikisha wanakuwa salama kuanzia shuleni na wawapo nyumbani.

Hayo yalisemwa na Ofisa Elimu Watu Wazima anayesimamia afya Shuleni Halmashauri ya Mji Kibaha Juliana Mwakatenya wakati wa mafunzo kwa wadau wa Shule Salama kwenye Halmashauri hiyo.

Mwakatenya alisema kuwa mpango huo uyazifikia shule zote za msingi za serikali na za binafsi na umelenga kuhakikisha usalama wa mwanafunzi kuanzia shuleni na nyumbani ili kumlinda na changamoto mbalimbali ikiwemo vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa.

Kwa upande wake mratibu wa Shule Salama Halmashauri ya Mji Kibaha Japhary Kambi alisema kuwa mafunzo hayo yatawasaidia wadau kuwalinda watoto ili wafikie malengo yao ambapo wadau wakijua vikwazo vinavyowakabili wanafunzi itakuwa ni rahisi kukabiliana navyo na kutoa taarifa sehemu husika ili wanaofanya vitendo hivyo wachukuliwe hatua za kisheria. 

Naye Chiku Abdul ofisa mwezeshaji wa mpango huo alisema kuwa matukio mengi ya vitendo vya ukatili yamekuwa hayaripotiwi na kufanya matukio kuongezeka kwani baadhi ya wazazi au walezi wa watoto wamekuwa wakimalizana pasipo kuyafikisha matukio hayo kwenye vyombo vya sheria.

Hatibu Omary mwenyekiti wa wasilishaji wa mada alisema kuwa wanaishukuru serikali kwa kuwapatia mafunzo ambapo waliyafanyia mkoani Morogoro na wao ndiyo wanawafundisha wadau wengine kuwa ulinzi na usalama wa mtoto ni jukumu la watu wote ndani ya jamii na kuwataka kutofumbia macho vitendo vya kikatili wanavyofanyiwa watoto.