Thursday, October 5, 2023

JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI MKOA WA PWANI LATOA TAHADHARI MVUA ZA EL NINO

 

*TAARIFA YA KAMANDA WA ZIMAMOTO PWANI ALIPOKUWA MGENI RASMI MAHAFALI YA 16 SHULE YA SEKONDARI KWALA - KIBAHA*

KAMANDA wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji mkoa wa Pwani SSF Jenifa Shirima kuwakumbusha wananchi  kuzingatia tahadhari zinazoendelea kutolewa kuhusu uwezekano wa kunyesha mvua kubwa za Elninyo.

Shirima ameyasema hayo alikpokuwa mgeni rasmi Mahafali ya 16 ya Kidato cha nne katika Shule ya Sekondari  Kwala iliyopo Kata ya Kwala Wilaya Kibaha na kuwataka watu wote wanaoishi maeneo hatarishi kuondoka kabla ya mvua hizo kuanza kunyesha ili kuepuka madhara.

Aidha amewaahidi kwamba atahakikisha changamoto walizoainisha atazifikisha sehemu husika ili ziweze kupatiwa ufumbuzi ambapo alitoa mchango wake fedha taslimu, vifaa vya kuzima na kung’amua moto kwa uongozi wa shule hiyo.

Pia alitoa zawadi za vifaa vya ki taaluma kwa wanafunzi wahitimu na Wanafunzi Skauti ambapo alipata nafasi ya kugawa vyeti kwa wahitimu pamoja na walimu na wanafunzi waliofanya vizuri zaidi.

No comments:

Post a Comment