Sunday, October 8, 2023

JUMUIYA WAZAZI PWANI YATAKA MAMLAKA USIMAMIZI KUSHIRIKIANA


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kupitia Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani amezitaka mamlaka za usimamizi kushirikiana katika utoaji wa vibali ili kuondoa muingiliano wa kimamlaka.

Hayo yamesemwa na mwenyekiti wa Wazazi mkoa wa Pwani Jackso Kituka wakati wa kikao cha Baraza la Wazazi Mkoa kilichoganyika Mjini Kibaha.

Kituka amesema kuwa baadhi ya mamlaka zimekuwa zikitofautiana kimaamuzi ambapo moja inaweza ikawa inakataa huku nyingine ikiruhusu kuhusu suala fulani.

"Mfano kama vile Baraza la Taifa la usimamizi wa mazingira (NEMC) linakataza upigaji wa muziki wenye kelele ambapo ni uchafuzi wa mazingira lakini ofisi ya utamaduni inaruhusu upigaji wa muziki kwenye kumbi za starehe,"amesema Kituka.

Naye ofisa mazingira kutoka NEMC Joseph Rugatiri akijibu baadhi ya maswali kuhusu mazingira amesema kuwa vibali vya uchimbaji mchanga hutolewa na halmashauri kama taratibu za uchimbaji mchanga zinakiukwa wananchi wanapaswa kutia malalamiko kwenye ofisi za mitaa na kama hakuna marekebisho taarifa zipelekwe kwao ili wachukue hatua na kuhusu kelele za muziki alisema kila eneo lina kiwango cha sauti.

No comments:

Post a Comment