KAMPUNI ya TCCIA Investment inatarajia kuongeza mtaji wake na kufikia bilioni 47 kutoka bilioni 37 ambazo zimewekezwa kwenye masoko mbalimbali ya hisa.
Hayo yamesemwa Mjini Kibaha na Mtendaji Mkuu wa kampuni hiyo Peter Kifungomali wakati akizungumza na wanahisa wa mkoa wa Pwani juu ya hisa walizowekeza.
Kifungomali amesema kuwa ongezeko hilo ni hadi itakapofika mwaka ujao wa fedha ambapo thamani imeongezeka kwa asilimia 53 kwa mwaka 2022.
Kwa upande wake makamu mwenyekiti wa chemba ya wafanyabiashara ya TCCIA Mkoa wa Pwani sehemu ya biashara Fadhili Gonzi amesema kuwa baadhi ya wanahisa walikuwa na maswali mengi juu ya fedha zao.
Naye mmoja wa wanahisa Ayubu Mtawazo amesema kuwa hisa ni moja ya sehemu salama ya kuwekeza fedha ambapo watu wengi wamenufaika.
Clara Ibihya amesema kuwa manufaa ya hisa ni makubwa kwani ukishawekeza fedha zako hupati tena usumbufu kutakiwa marejesho bali unasubiri kupata fedha.
No comments:
Post a Comment