Monday, August 7, 2023
UMWELANI WAKOMBA MILIONI 2 MICHO CUP
Sunday, August 6, 2023
MAZINGIRA YA MICHEZO KUBORESHWA KUINUA SOKA KIBAHA
UMWELANI MABINGWA MICHO CUP
UMWELANI WATWAA KOMBE MICHO CUP
Saturday, August 5, 2023
WAKULIMA WATAKIWA KULIMA KILIMO CHA KIBIASHARA NA SIYO CHA KUJIKIMU
SEARIKALI imepanga kubadilisha kilimo kutoka kuwa cha kujikimu na kuwa kilimo cha biashara ambapo mabadiliko hayo yanafanyika kwa kuzingatia malengo ya kitaifa kama yalivyoainishwa kwenye dira ya taifa ya maendeleo 2025 na kuhakikisha kilimo ichangie ipasavyo Katika vita dhidi ya umasikini na kulenga kukuza sekta hiyo kufikia asilimia 10 ifikapo Mwaka 2030.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Balozi Pindi Chana katika ufunguzi wa kongamano la zao la Mtama Jijini Dodoma kwenye maonesho ya nanenane.
Chana amesema kuwa mipango hiyo yote ya kitaifa imeweka mkazo kwenye mapinduzi ya viwanda na kubainisha sekta ya Kilimo kama mhimili imara utakaowezesha upatikanaji wa maligrafi za viwanda.
Amesema kuwa Mikoa ya kanda ya kati kama iliyo kwa Nchi na Dunia nzima inakabiliwa na mabadiliko ya tabia Nchi ambapo Mkoa wa Dodoma na Singida imeamua kwa dhati kuendeleza zao la Mtama ambalo limekuwa likistawi vizuri kwa hali ya hewa ya Mikoa hiyo.
Kanda ya kati imeamua kufanya uhamasishaji kupitia kongamano Hilo kuhusu matumizi ya teknolojia Bora Katika uzalishaji wa Zao la Mtama lengo likiwa ni kuunga mkono na kutekeleza kwa vitendo jitihada za Dkt. Mhe. Samia Suluhu Hassan Katika kuongeza Kasi ya ukuaji wa sekta ya Kilimo kutokana na kuhakikisha usalama wa chakula na kipato kwa wananchi.
Thursday, August 3, 2023
WANNE WAFA AJALINI PWANI
MKURUGENZI wa benki ya APSA Nechi Msuya (45- 50) mkazi wa Dar es Salaam na watu wengine watatu wamefariki dunia baada ya gari walilokuwa wakisafiria kuligonga gari lingine uso kwa uso.
Monday, July 31, 2023
MAKONGAMANO YA NANE NANE KUWA NA TIJA
Na Manase Madelemu, Dodoma
MKUU wa mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamle amesema kuwa tofauti na maonesha ya miaka iliyopita ya nane nane mwaka huu 2023 yatahusisha matukio muhimu na makongamano yanayoongeza wigo wa uzalishaji bora.
Senyamule amesema hayo leo julai 31,2023 jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuelekea Maadhimisho ya nane nane mwaka kikanda.
Amesema kutakuwa na makongamano ya tasnia ya alizeti,kongamano la zao la mtama ambapo mikoa ya Dodoma na singida ilikabidhiwa jukumu la kuzalisha alizeti Kwa wingi ili kupunguza nakisi ya mafuta ya kula nchini na hivyo kuokoa fedha za kigeni.
Aidha ameongeza kuwa kutakuwepo na siku maalumu ya uhamasishaji uzalishaji kuku wa kienyeji hasa katika mkoa wa Singida unafahamika katika mikoa mbalimbali hapa nchini hadi kufikia watu kuwaita kuku wa Singida
Pia Senyamule amesema kuwa Katika maonesho ya mwaka huu kutakuwa na huduma za Afya na matibabu ya kibingwa zitakazotolewa na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Benjamin Mkapa na huduma hizi zitatolewa bure.
Kauli mbiu ya maonesha na sherehe za nane nane kitaifa Kwa mwaka 2023 ni Vijana na wanawake ni Msingi Imara wa Mifumo Endelevu ya Chakula"na kauli mbiu kikanda Kilimo ni Biashara, Biashara ni Uwekezaji.