CHAMA Cha Soka Wilaya ya Kibaha (KIBAFA) kimefanya uchaguzi wake Mkuu na kupata viongozi watakaokiongoza chama hicho kwa kipindi cha miaka minne ambapo Robert Munis amechaguliwa kuwa mwenyekiti.
Monday, July 3, 2023
MUNIS ACHAGULIWA MENYEKITI KIBAFA
WAANDISHI WA HABARI WAULA UCHAGUZI WA SOKA WILAYA YA KIBAHA (KIBAFA)
Saturday, July 1, 2023
MHE.MASANJA ACHANGISHA MILIONI 95 ZA UJENZI WA KANISA LA WAADVENTISTA WASABATO SDA PASIANSI MWANZA
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja ameongoza harambee ya kuchangia ujenzi wa nyumba ya ibada ya Kanisa la Waadventista Wasabato SDA Pasiansi kwenye Jimbo Kuu la Nyanza Kusini leo mkoani Mwanza na kupata kiasi cha shilingi milioni 95. 2 ambapo fedha taslimu zilikuwa shilingi milioni 47.3 na ahadi shilingi milioni 47.8.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Masanja amelipongeza kanisa la SDA Pasiansi kwa kuanza ujenzi wa kanisa hilo jipya ambalo ujenzi wake ulianza mwaka 2022 huku waumini wa kanisa hilo wakiwa wameshafanikiwa kuchangia shilingi milioni 56 za ujenzi.
"Serikali inatambua mchango wa kanisa hili katika sekta ya Elimu na Afya. Ujenzi wa kanisa hili ni wito na wajibu wa kila mmoja wetu" amesema Mhe. Masanja
Amesema lengo kuu la kufanya harambee hiyo ni kutafuta fedha za ujenzi wa kanisa na fedha zinazohitajika ni zaidi ya milioni 200.
Amewaomba waumini wa kanisa hilo waendelee kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo na pia kuendelea kuiombea Tanzania iendelee kuwa na amani, umoja na upendo.
Naye, Mchungaji wa Kanisa la SDA Pasiansi Harun Kuyenga amesema mradi huo wa ujenzi la kanisa ulianza mwaka 2022 na unatarajia kukamilika mwaka 2024 na mara baada ya kukamilika kwake kanisa litakuwa na uwezo wa kubeba waumini 3000 ambapo kanisa la sasa lina uwezo wa kubeba waumini 800.
Ameongeza kuwa wameamua kujenga kanisa hilo jipya kutokana na ongezeko la waumini kutoka maeneo tofauti tofauti huku akisisitiza kuwa kwa sasa kiasi cha fedha shilingi milioni 200 zinahitajika ili kukamilisha ujenzi wa Kanisa hilo.
Katika Harambee hiyo, Mhe.Masanja pamoja na familia yake na marafiki zake walifanikiwa kuchangia ujenzi wa kanisa hilo kiasi cha shilingi milioni 51,050,000 ambapo fedha taslimu ilikuwa ni shilingi milioni 30,550,000 na ahadi shilingi milioni 20,500,000.
MHE.MARY MASANJA ATEMBELEA OFISI ZA CCM MKOANI MWANZA
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mwanza na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja leo ametembelea Ofisi za Chama cha Mapinduzi jijini Mwanza na kufanya mazungumzo na Katibu wa CCM, Mkoa wa Mwanza Ndugu Omary Mtuwa.
Pia, alipata nafasi ya kuzungumza na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza Ndugu Sixbert Reuben Jichabu.
Mhe. Masanja anatarajia kushiriki katika Harambee ya Kuchangia ujenzi wa Nyumba ya Ibada ya Kanisa la Pasiansi SDA jijini humo tarehe 1 Julai,2023.
Friday, June 30, 2023
KPC YATAKIWA KUPAMBANA NA VITENDO VYA UKATILI KWENYE JAMII
MJUMBE wa Kituo cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) Lydia Mgaya amekitaka kituo hicho kufuatilia baadhi ya matukio ya Ukatili kwa watoto na wanawake kwenye jamii ili wahusika wachukuliwe hatua.
SERIKALI YATAKIWA KUDHIBITI MABANDA YA VIDEO KWA WATOTO
KITUO cha Msaada wa Kisheria Kibaha (KPC) kimeishauri serikali kudhibiti vibanda vinavyoonyesha video maarufu kama vibanda umiza ambapo baadhi ya watoto chini ya miaka 18 kufanyiwa vitendo vya ukatili.
Wednesday, June 28, 2023
VITUO MAALUMU 175 KWAAJILI YA HUDUMA MAHUTUTI KWA WATOTO WACHANGA VYAONGEZWA
NAIBU Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema, Serikali imeongeza vituo vyenye vyumba maalumu kwa ajili ya kutoa huduma kwa watoto wachanga wenye umri kati ya sifuri mpaka mitano wenye hali mahututi (Neonatal Care Unit), kutoka 18 mwaka 2017 kufikia 175 mwaka 2023.
Amesema leo Juni 28 wakati akijibu swali la Mbunge wa viti maalumu Mhe. Zaytun Seif Swai katika kikao cha kumi na mbili, Bungeni Jijini Dodoma.
"Serikali kupitia wizara ya Afya imeweka mipango ya kupunguza vifo vya watoto wenye umri 0 hadi 1 kwa kuongeza vituo vyenye vyumba maalumu kwa ajili ya kutoa huduma kwa watoto wachanga wenye hali mahututi (Neonatal Care Unit), kutoka 18 mwaka 2017 kufikia 175 mwaka 2023." Amesema
Ameendelea kusema, Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kutoa mafunzo kwa watoa huduma juu ya namna ya kutoa huduma jumuishi kwa watoto wachanga na watoto wakubwa (Intergrated Management of Childhood Illness-IMCI) ili kuokoa vifo vya watoto hao vinavyoweza kuepukika.
Amesema, Serikali imeendelea kuimarisha huduma za kukinga na kuzuia magonjwa yanayozuilika kwa Chanjo kama vile Surua, Nimonia, kuharisha, donda koo, kifaduro, pepo punda na polio kwa kuongeza utoaji wa chanjo za Watoto chini ya Mwaka mmoja kufikia kiwango cha zaidi ya asilimia 98 ya utoaji wa chanjo ya Penta 3.
Aidha, Dkt. Mollel amesema, Serikali imeongeza vituo vinavyotoa huduma kwa watoto waliozaliwa wakiwa na uzito pungufu (Kangaroo Mother Care) ambapo kwa sasa vituo 72 na Hospitali 175 zinatoa huduma hizi, huku akiweka wazi kuwa, kwa mwaka 2023/2024 Serikali imepanga kuongeza vituo 100 ili kufikia vituo 275 ifikapo mwezi Juni 2024 vitavyosaidia kuongeza huduma hizo nchini.
Sambamba na hilo Dkt. Mollel amesema Serikali imeendelea kuongeza vifaa na vifaa tiba ikiwemo CT-SCAN zimeongezeka kutoka 3 mpaka sasa zipo zaidi ya 50, MRI zilikuwa 2 lakini mpaka sasa zipo zaidi ya 19, hivyo kumtoa kuwaondoa hofu Wabunge kuwa hata vifaa vya huduma hizo vitaenda kuwekwa kwenye vituo vyote 100 vitavyojengwa nchini.
Kwa upande mwingine Dkt. Mollel amesema, ili kukabiliana na changamoto ya gharama za matibabu kwa wazee, Wizara inaendelea kuhamasisha Wabunge na viongozi wengine pamoja na wananchi kuunga mkono Bima ya afya kwa wote ili kila mwananchi aweze kunufaika na huduma bora bila gharama kuanzia ngazi ya Zahanati mpaka hospitali ya Taifa.