SHULE ya Sekondari ya Tumbi imepokea kiasi cha shilingi milioni 200 kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya shule.
Thursday, May 25, 2023
SHULE ZA SEKONDARI TUMBI NA MWANALUGALI ZAPOKEA MILIONI 300
6,052 WATAMBULIWA MTAA WA LUMUMBA WALIOVAMIA SHAMBA LA MITAMBA
MTAA wa Lumumba Halmashauri ya Mji Kibaha utambuzi wa wananchi waliovamia eneo imefanyika na kukamilika na jumla ya wananchi 6,052 wametambuliwa.
Hayo yalisemwa na Hamis Shomari ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira na diwani wa Kata ya Kongowe aliyasema hayo kwenye kikao cha kawaida kipindi cha robo tatu Januari-Machi cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha.
HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAFANYA UTAMBUZI WA WALIOVAMIA ENEO MTAA WA MKOMBOZI
HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAKUSANYA MABILIONI
HALMASHAURI ya Mji Kibaha imekusanya kiasi cha shilingi bilioni 3.5 sawa na asilimia 78 ya makisio ya mwaka 2022/2023 ikiwa ni mapato ya ndani ambapo ilikadiria kukusanya shilingi bilioni 4.5.
HALMASHAURI YA MJI KIBAHA YAKUSANYA MABILIONI
Saturday, May 20, 2023
VYAMA VYA USHIRIKA KUUNGANISHWA NA WADAU
JUKWAA la maendeleo ya vyama vya ushirika mkoa wa Dodoma limepanga kuwaunganisha vyama vya ushirika na wadau mbalimbali wakiwemo mabenki ili kuwawezesha kifedha pamoja na kuimalika kimtaji viweze kupata maendeleo.
Hayo ameyasema Jijini Dodoma Kaimu Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Dodoma Octavia Bidyanguze wakati wa uzinduzi wa jukwaa la maendeleo ya vyama vya ushirika mkoa wa Dodoma 2023.
Bidyanguze amesema mkoa wa Dodoma una vyama vya ushirika 124 vikiwemo 57 vyama vya kifedha, 49 vyama vya kilimo na masoko na vyama vinginevyo 18 hivyo kutokana na idadi hii jukwaa la maendeleo ya vyama vya ushirika linakwenda kuwajengea uwezo kwa maana ya kutoa elimu kwa vyama hivyo.
Amesema kuwa mpaka sasa vyama hivyo vimeweza kununua hisa zenye thamani ya 146.3 ili kuwa na uwezo wa kusaidiana kwa wale wasio na uwezo wa kifedha.
Kwa upande wake Meneja wa UDOM SACCOS LTD Erasmus Tandike amesema kuwa Moja ya mikakati walio nayo ni kujitangaza na kuhakikisha ushirika huu unaazia ngazi ya chini ili kufikia wakazi wote wa Dodoma pamoja na kuhakikisha kila vyama vinanufaika na vinafikia malengo.
Naye Mjumbe wa bodi ya PCCB SACOOS pia ni Mratibu wa kongamano la Central Women Connect Rashida Mfaume amewataka wanawake kukimbilia fursa ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kijamii kama ambayo yeye amenufaika na ushirika huu kwa maana ya kuweza kuwekeza pamoja na kupata nafasi ya kukopa .
Ikumbukwe kuwa moja ya lengo la jukwaa hili ni kutoa fursa vyama vya ushirika, kuwakutanisha na kubadilishana uzoefu, kuelimishana na kuweza kujifunza mambo mbalimbali ya vyama vya ushirika.
Thursday, May 18, 2023
WIZARA VIWANDA NA BIASHARA KUANDAA MWONGOZO KWA WAFANYABIASHARA
MKURUGENZI wa uwezeshaji wananchi kiuchumi na maendeleo ya sekta binafsi ya TAMISEMI Conrad Milinga amesema kuwa Wizara ya Viwanda na Uwekezaji inaandaa mwongozo wa kuwawezesha wafanyabishara wajasiliamari kutambua kuwa wanapohitaji kuanzisha biashara sehemu ya kuanzia na kuishia.
Milingi ameyasema hayo Jijini Dodoma, katika kikao cha kuthibitisha rasimu ya muongozo wa wataalamu wa biashara na mpango wa kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji nchini kilichofanyika katika ukumbi wa bodi ya wakandarasi.
Aidha amesema kuhusiana na taarifa za mwenendo wa bei za vyakula nchini wanahitaji kuzipata kuanzia kwao lakini zisitofautiane na zile zinazotolewa na wizara, hivyo waweke mfumo wa taarifa watakazo kuwa wanazipata kutoka kwao.
Kwa upande wake katibu tawala masidizi wa viwanda, biashara na uwekezaji mkoa wa Kigoma Deogratias Sangu, amesema kabla ya kuanzishwa kwa idara hiyo wizara ilikuwa ikifanya, kuunda, kupendekeza pamoja na kuanzisha sera ambapo utekelezaji wa chini haukuwa thabiti kwasababu haukuwa na wasimamizi, hivyo kupitia idara hiyo wasimamizi wana mwendelezo wa majukumu yaliyopangwa yatatimizwa.
Naye katibu tawala msaidizi viwanda, bishara na uwekezaji mkoa wa Morogoro Beatrice Njawa amesema kwakuwa wamepitishwa kwenye mpango wa kuboresha mazingira ya kufanyia bishara anaamini wanaenda kusimamia na kuondoa vikwazo vyote vya kibishara na uwekezaji katika mamlaka za serikali za mitaa na mikoani ili kuweza kutangaza uwekezaji unaopatikana katika maeneo hayo.
Njawa ameongeza kuwa wakiweza kuboresha eneo hilo hasa uwekezaji na ujenzi wa viwanda maana yake wanaenda kuzipa nguvu mamlaka za serikali za mitaa na wataongeza mapato na wanaenda kuimalisha mahusiano kati ya mikoa, halmashauri pamoja na sekta binafsi zilizopo katika maeneo yao.