MTAA wa Lumumba Halmashauri ya Mji Kibaha utambuzi wa wananchi waliovamia eneo imefanyika na kukamilika na jumla ya wananchi 6,052 wametambuliwa.
Hayo yalisemwa na Hamis Shomari ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira na diwani wa Kata ya Kongowe aliyasema hayo kwenye kikao cha kawaida kipindi cha robo tatu Januari-Machi cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha.
Alisema kazi ya utambuzi wa wananchi waliovamia eneo imefanyika na kukamilika na kazi ua uandaaji michoro nane yenye jumla ya viwanja 7,264 imekamilika.
"Maandalizi ya upimaji katika mtaa wa Lumumba yamekamilika na kazi ya upimaji wa viwanja na matarajio ni kupima viwanja 7,264 ambapo itakamilika ndani ya miezi miwili,"alisema Shomari.
No comments:
Post a Comment