KAMISAA wa Sensa Tanzania Bara Anne Makinda amewataka wadau wa maendeleo nchini kutumia takwimu za sensa ambazo zimefanywa kisayansi ili kutumia rasilimali kikamilifu.
Makinda aliyasema hayo Mjini Kibaha wakati wa mafunzo ya sensa kwa kamati ya mkoa na viongozi wa ngazi ya mkoa.
Alisema kuwa kwa kutumia takwimu hizo itasaidia wakati wa kupanga bajeti hivyo kuweka matumizi mazuri ya rasilimali ambapo viongozi mbalimbali wanapaswa kutumia matokeo ya sensa hiyo ili kuleta maendeleo kwa wananchi.
Naye Balozi Mohamed Haji Hamza Kamisaa wa Sensa Tanzania Zanzibar alisema kuwa hadi Juni mwakani machapisho 200 yatatolewa ili kuwajengea watu uelewa juu ya ripoti ya sensa.
Mwakilishi wa mtakwimu mkuu Adela Temba alisema kuwa matokeo ya sensa hutolewa kwa awamu ambapo ripoti kuu nne zimeshazinduliwa na Rais Dk Samia Suluhu Hassan.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge ambaye alikuwa mgeni rasmi alisema kuwa takwimu za sensa ni muhimu sana katika matumizi ya rasilimali.
No comments:
Post a Comment