Hayo yalisemwa na Hamis Shomari ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya mipango miji na mazingira na diwani wa Kata ya Kongowe aliyasema hayo kwenye kikao cha kawaida kipindi cha robo tatu Januari-Machi cha baraza la madiwani wa Halmashauri ya Mji Kibaha.
Shomari alisema kuwa watu hao wametambuliwa ili kupimiwa viwanja 6,250 kwenye michoro 22 ambayo imeandaliwa na kuidhinishwa.
"Kazi ya upimaji wa viwanja 6,300 imefanyika na kuwasilishwa kwa ajili ya uidhinishwaji wa ramani kwa mpima ardhi wa mkoa na jumla ya viwanja 3,950 vimeidhinishwa,"alisema Shomari.
Alisema kuwa uuzaji wa viwanja katika mtaa umeanza Machi 24 ambapo wananchi walijulishwa kwa njia ya matangazo na mkutano wa hadhara ambapo hadi Aprili jumla ya ankara ya viwanja 168 vyenye thamani ya shilingi milioni 129.2 zimetolewa.
No comments:
Post a Comment