Saturday, May 20, 2023

VYAMA VYA USHIRIKA KUUNGANISHWA NA WADAU


Na Wellu Mtaki, Dodoma

JUKWAA la maendeleo ya vyama vya ushirika  mkoa wa Dodoma limepanga kuwaunganisha vyama vya ushirika na wadau mbalimbali wakiwemo mabenki ili kuwawezesha kifedha pamoja na kuimalika kimtaji  viweze kupata maendeleo.

Hayo ameyasema  Jijini Dodoma Kaimu Mrajisi Msaidizi Mkoa wa Dodoma Octavia Bidyanguze wakati wa uzinduzi wa jukwaa la maendeleo ya vyama vya ushirika mkoa wa Dodoma 2023.

Bidyanguze amesema mkoa wa Dodoma una vyama vya ushirika 124 vikiwemo 57 vyama vya kifedha, 49 vyama vya  kilimo na masoko na vyama vinginevyo 18 hivyo kutokana na idadi hii jukwaa la maendeleo ya vyama vya ushirika linakwenda kuwajengea uwezo kwa maana ya kutoa elimu kwa vyama hivyo.

Amesema kuwa mpaka sasa vyama hivyo vimeweza kununua hisa zenye thamani ya 146.3 ili kuwa na uwezo  wa kusaidiana kwa wale wasio na uwezo wa kifedha.

Kwa upande wake Meneja wa UDOM SACCOS LTD Erasmus Tandike amesema kuwa Moja ya mikakati walio nayo ni kujitangaza na kuhakikisha ushirika huu unaazia ngazi ya chini ili kufikia wakazi wote wa Dodoma pamoja na  kuhakikisha kila vyama vinanufaika na vinafikia malengo.

Naye Mjumbe wa bodi ya PCCB SACOOS pia ni   Mratibu wa kongamano la Central Women Connect  Rashida Mfaume amewataka wanawake kukimbilia fursa ili kuweza kujikwamua kiuchumi na kijamii kama ambayo yeye  amenufaika na ushirika huu kwa maana ya kuweza  kuwekeza pamoja na kupata nafasi ya kukopa .

Ikumbukwe kuwa moja ya lengo la jukwaa hili ni kutoa fursa vyama vya ushirika, kuwakutanisha na kubadilishana uzoefu, kuelimishana na kuweza kujifunza mambo mbalimbali ya vyama vya ushirika.




No comments:

Post a Comment