HALMASHAURI ya Mji Kibaha imekusanya kiasi cha shilingi bilioni 3.5 sawa na asilimia 78 ya makisio ya mwaka 2022/2023 ikiwa ni mapato ya ndani ambapo ilikadiria kukusanya shilingi bilioni 4.5.
Hayo yalisemwa Mjini Kibaha na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Selina Wilson wakati wa kikao cha baraza la madiwani kwa kipindi cha robo tatu Januari hadi Machi.
Wilson alisema kuwa makusanyo hayo ni kuanzia Julai 2022 hadi Machi 2023 ambapo kwa upande wa vyanzo fungwa makisio ilikuwa ni shilingi milioni 506.7.
"Na kwa kipindi cha kuanzia mwezi Julai 2022 mpaka Machi 2023 kiasi cha shilingi milioni 587.8 kimekusanywa sawa na asilimia 116 ya makisio ya mwaka,"alisema Wilson.
No comments:
Post a Comment