Friday, June 20, 2014
WATATU WADAKWA NA SILAHA NA SARE ZA JESHI
Na John Gagarini, Kibaha
JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kuwakamata watu watatu akiwemo mtu Daniel Mtalisi mkazi wa Kisemvule wilaya ya Mkuranga ambaye alipitia mafunzo ya kijeshi kwa tuhuma za kufanya tukio la uhalifu wa kupora silaha na vitu mbalimbali.
Mtuhumiwa huyo ambayealiwahi kupata mafunzo ya kijeshi kwenye Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi namba 833 Oljoro Arusha na namba yake ni MT. 95150.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa waandishi wa habari mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 17 mwaka huu majira ya saa 2 usiku huko Kijiji cha Kisemvule kata ya Vikindu kata ya Mkuranga wilaya ya Mkuranga.
Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao wengine wakiwa ni Khalfan Abas (25) mkazi wa Mwanambaya na Mashaka Masanja (24) mkazi wa Mwongozo Kigamboni Jijini Dar es Salaam walikamatwa baada ya polisi kufanya msako mkali na kumkuta mtuhumiwa huyo akiwa na silaha hiyo ambayo walimpora Musa Kambangwa ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanambaya.
“Watu hao walimvamia mlalamikaji ambaye alikuwa akirejea nyumbani kutoa kwenye biashara zake walimteka kisha kumpiga na walimwamuru awapeleke nyumbani kwake na kuichukua silaha hiyo bastola yenye namba A 569542 aina ya Browning, Carriber 7.65 mm, magazine 2 na risasi 23, chaja 1 ambavyo alikuwa amehifadhi nyumbani kwake,” alisema Kamanda Matei.
Aidha Kamanda Matei alisema kuwa kabla ya kukamatwa watuhumiwa hao walifanya tukio hilo Juni 11 mwaka huu huko Kijiji cha Mwanambaya ambapo walimvamia mlalamikaji akiwa na mke wake.
“Walimjeruhi kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kumsababishia maumivu makali kisha kumtaka awape funguo ya nyumba yake ili waingie ndani lakini alikataa wakaendelea kumpiga hadi alipopoteza fahamu na kuichukua funguo na kuingia ndani na kuchuakua silaha hiyo na simu 2 aina ya Nokia, Inveta , deki 1 ya Dvd na viatu pea moja kisha kutoweka na ndipo walipokuja kukamatwa Juni 17,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa baada ya tukio hilo ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kuvikuta vitu hivyo ambapo mtuhumiwa wa kwanza alikutwa na sare za Jeshi.
Alibainisha kuwa mlalamikaji anaendelea vizuri na kuwataka watu kutoa taarifa za uhalifu ili kuzuia matukio hayo ambayo yameanza kuibuka kwa wingi na watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika.
Mwisho
JESHI la Polisi mkoani Pwani limefanikiwa kuwakamata watu watatu akiwemo mtu Daniel Mtalisi mkazi wa Kisemvule wilaya ya Mkuranga ambaye alipitia mafunzo ya kijeshi kwa tuhuma za kufanya tukio la uhalifu wa kupora silaha na vitu mbalimbali.
Mtuhumiwa huyo ambayealiwahi kupata mafunzo ya kijeshi kwenye Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kikosi namba 833 Oljoro Arusha na namba yake ni MT. 95150.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa waandishi wa habari mjini Kibaha, kamanda wa Polisi mkoani humo Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Juni 17 mwaka huu majira ya saa 2 usiku huko Kijiji cha Kisemvule kata ya Vikindu kata ya Mkuranga wilaya ya Mkuranga.
Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao wengine wakiwa ni Khalfan Abas (25) mkazi wa Mwanambaya na Mashaka Masanja (24) mkazi wa Mwongozo Kigamboni Jijini Dar es Salaam walikamatwa baada ya polisi kufanya msako mkali na kumkuta mtuhumiwa huyo akiwa na silaha hiyo ambayo walimpora Musa Kambangwa ambaye ni mfanyabiashara wa Mwanambaya.
“Watu hao walimvamia mlalamikaji ambaye alikuwa akirejea nyumbani kutoa kwenye biashara zake walimteka kisha kumpiga na walimwamuru awapeleke nyumbani kwake na kuichukua silaha hiyo bastola yenye namba A 569542 aina ya Browning, Carriber 7.65 mm, magazine 2 na risasi 23, chaja 1 ambavyo alikuwa amehifadhi nyumbani kwake,” alisema Kamanda Matei.
Aidha Kamanda Matei alisema kuwa kabla ya kukamatwa watuhumiwa hao walifanya tukio hilo Juni 11 mwaka huu huko Kijiji cha Mwanambaya ambapo walimvamia mlalamikaji akiwa na mke wake.
“Walimjeruhi kwa kutumia silaha mbalimbali za jadi na kumsababishia maumivu makali kisha kumtaka awape funguo ya nyumba yake ili waingie ndani lakini alikataa wakaendelea kumpiga hadi alipopoteza fahamu na kuichukua funguo na kuingia ndani na kuchuakua silaha hiyo na simu 2 aina ya Nokia, Inveta , deki 1 ya Dvd na viatu pea moja kisha kutoweka na ndipo walipokuja kukamatwa Juni 17,” alisema Kamanda Matei.
Alisema kuwa baada ya tukio hilo ndipo walipofanya msako na kufanikiwa kuvikuta vitu hivyo ambapo mtuhumiwa wa kwanza alikutwa na sare za Jeshi.
Alibainisha kuwa mlalamikaji anaendelea vizuri na kuwataka watu kutoa taarifa za uhalifu ili kuzuia matukio hayo ambayo yameanza kuibuka kwa wingi na watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakamani mara upelelezi wa tukio hilo utakapokamilika.
Mwisho
Monday, June 16, 2014
WANAJESHI WAWILI WAFA AJALINI
Na John Gagarini, Kibaha
WATU wawili wamefariki dunia huku mmoja akijeruhiwa baada ya
magari waliyokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani
Pwani, kamishna Msaidizi mwandamizi wa polisi (SACP) Ulrich Matei amesema kuwa
ajali hiyo ilihusisha lori na gari dogo.
Kamanda Matei alisema kuwa ajali hiyo ilitokea Juni 16 mwaka
huu majira saa 1:15 usiku eneo la Chamakweza kata ya Pera tarafa ya Chalinze
wilayani Bagamoyo.
Alisema ajali hiyo ilihusisha lori aina ya Scania lenye namba
za usajili T 164 AUS na tela namba T 498 AZ likiendeshwa na Hassan Shaban mkazi
wa Dar es Salaam ambaye aligongana na gari aina ya Isuzu Carry lenye namba za
usajili Z 190 DR likitokea mkoani Morogoro.
“Waliokufa ni dereva
wa gari dogo Meja Edward Mosi ambaye ni ofisa wa Jeshi la Wananchi Tanzania
(JWTZ) kikosi cha Kinonko na mkaguzi Msaidizi wa Polisi wa wilaya ya Korogwe
mkoani Tanga Johnson Zakaria,” alisema Matei.
Aidha alisema katika ajali hiyo mtu mmoja alijeruhiwa na
kukimbizwa hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Pwani Tumbi kwa ajili ya matibabu huku
miili hiyo nayo ikiwa hospitalini hapo kusubiri ndugu kwa ajili ya mazishi.
“Kutokana na ajali hiyo jeshi la polisi linamtafuta dereva wa
lori ambaye alikimbia mara baada ya tukio hilo, ili aweze kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria,” alisema Matei.
Mwisho.
Tuesday, June 10, 2014
WAFANYABIASHARA WATAKIWA KUPIMA AFYA ZAO
Na John Gagarini, Kibaha
IDARA ya Afya ya Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani
imeanza uhakiki wa wafanyabiashara mbalimbali kama wamepima afya zao kwa mujibu
wa sheria ili watoe huduma hizo wakiwa na afya njema na endapo watashindwa
kufanya hivyo watafungiwa biashara zao.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jana mjini Kibaha ofisa afya wa Halmashauri ya Mji
wa Kibaha David Vuo alisema kuwa wafanyabiashara hao pamoja na wamiliki wa
viwanda wanapaswa kuhakikisha watoa huduma wao wanapima afya zao.
“Utaratibu huu ni wa kisheria kwani hata wafanyakazi wa
serikali kabla ya kuanza kazi wanapaswa kupima afya zao na hii ni sheria ya
afya ya mwaka 2009 namba 169 kifungu namba 17ambapo kwa sasa maofisa afya wa
kata wanafanya uhakiki kuona zoezi hilo ili taratibu stahiki zichukuliwe kwa
wale watakaoshindwa kutekeleza agizo hilo ,” alisema Vuo.
Alisema kuwa jambo hilo si geni kwani liko kisheria na
linawagusa wafanyabiashara wote na shughuli mbalimbali za wajasiriamali ambao
wanapaswa kufuata taratibu za kiafya.
“Lengo la kupima afya na kuhakikisha kuwa wahudumu hao
wanahudumia wateja wakiwa na afya njema na kama kuna atakayegundulika anapaswa
kutibiwa kwanza hadi atakapopona ndipo aendelee kutoa huduma na kutakuwa na
fomu maalumu itakayokuwa kwenye eneo la shughuli ili kuwatambua waliofanya
hivyo na wale watakaoshindwa hawataruhusiwa kuhudumiwa watu,” alisema Vuo.
Aidha alitaja magonjwa ambayo yanapimwa kuwa ni Taifodi,
Kuhara, Mkojo, magonjwa ya Kaswende, Gono, Kifua, magonjwa ya ngozi kama vile upele
na mengineyo.
“Suala la kupima virusi vya ugonjwa wa UKIMWI ni hiyari
ambapo upimaji wa magonjwa haya hayahusiani na kupima ugonjwa huo labda mhusika
atake mwenyewe ambapo upimaji huu utafanyika kwenye hospitali ya wilaya ya
Mkoani na kituo cha afya Kongowe,” alisema Vuo.
Ofisa afya huyo wa halmashauri ya Mji wa Kibaha alissema kuwa
kuhusiana na uchangiaji wa vipimo hivyo kila mhusika anapaswa kutoa kiasi cha
shilingi 5,000 kwenye ofisi ya kata kisha atapewa fomu kwa ajili ya kwenda
kupima ambapo alisema elimu ilishatolewa.
Alitaja biashara ambazo watumishi wake wanatakiwa kupima afya
zao kuwa ni mama na baba lishe, bekari, migahawa, hoteli, baa, nyumba za kulala
wageni, mashine za kusaga nafaka, maduka ya vyakula, mabucha, machinjio,
saluni, dobi, viwanda, wachoma chipsi, vilabu vya pombe za kienyeji,
wafanyakazi wa kampuni na vikundi vya ujasiriamali.
Subscribe to:
Posts (Atom)