KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.Friday, January 30, 2026
KATA YA VISIGA YAMSHUKURU RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN SIKU 100 KUMWAGA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO
KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.Thursday, January 29, 2026
SIKU 100 ZA RAIS DK SAMIA SULUHU HASSAN MIRADI YA MAENDELEO
KATA ya Visiga Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha inaendelea na mchakato wa kuibadilisha Zahanati ya Visiga kuwa kituo cha afya ambapo imepokea kiasi cha shilingi milioni 57 kwa ajili hiyo.
Tuesday, January 27, 2026
WANASIASA WANAWAKE WATAKIWA KUJIKITA KWENYE UCHUMI
WANAWAKE wanasiasa Wilayani Kibaha wametakiwa kupambana kukuza uchumi wao ili kukabiliana na changamoto ukatili wa kijinsia wanazozipata kipindi cha kuwania uongozi.
Monday, January 26, 2026
MITI 6,379 KUPANDWA PWANI KUMBUKIZI KUZALIWA DK SAMIA SULUHU HASSAN
MITI 6,379 itapandwa Mkoani Pwani katika kuadhimisha siku ya kumbukizi ya kuzaliwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. Samia Suluhu Hassan.
HALMASHAURI YAKABIDHI MADAWATI 4,000
HALMASHAURI ya Manispaa ya Kibaha imetoa madawati viti na meza 4,000 kwa Shule za Msingi na Sekondari vikiwa na thamani ya shilingi milioni 400.
Akikabidhi madawati viti na meza Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa Halmashauri imefanya jambo zuri la kukabili changamoto ya wanafunzi kukaa chini.
Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Kibaha Dk Nicas Mawazo alisema kuwa idadi ya wanafunzi inaongezeka kutokana na wazazi kuhamia Kibaha.
Naye Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Dk Rogers Shemwelekwa alisema kuwa walitenga kiasi cha shilingi milioni 400 kwa ajili ya kutengeneza madawati viti na meza 4,000 ikiwa kwa Shule za Msingi madawati 2,000 na Sekondari viti na meza 2,000.
Sunday, January 25, 2026
VIJANA WATUNZE AMANI
MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) NEC Taifa kupitia Jumuiya ya Wazazi Hamoud Jumaa ameitaka Jumuiya hiyo kuwapa vijana malezi mazuri ili watunze amani.
Saturday, January 24, 2026
VIJANA WAPEWE MALEZI BORA KULINDA AMANI
Jumaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibaha Vijijini ameyasema hayo Mjini Kibaha wakati akifungua kikao cha Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Pwani.
Amesema kazi ya Jumuiya hiyo ni kuhakikisha jamii hususani vijana wanakuwa na malezi bora ili kutojiingiza kwenye makundi ambayo hayana maadili mema.
"Tuwape elimu na malezi mazuri vijana wetu na tuzungumze nao juu ya amani kwani amani pia huleta afya njema na amani ndiyo kila jambo hivyo tuhubiri amani,"amesema Jumaa.
Aidha amesema vijana nchini wanapaswa kudumisha amani na kutokubali kurubuniwa ili wasivunje amani iliyopo kwani bila amani hatutaweza kufanya mambo ya maendeleo.
"Vijana wanapaswa kulinda amani kwani ndiyo msingi wa Taifa la Tanzania na wasukubali kushawishiwa na watu kuharibu amani iliyopo kwani ikipotea ni gharama kuirudisha,"amesema Jumaa.
Amewataka viongozi wa Jumuiya hiyo kuanza maandalizi ya uchaguzi wa Jumuiya utakaofanyika mwakani kwani uchaguzi ndani ya chama ni mgumu kuliko uchaguzi wa vyama.
"Muanze maandalizi na kama kuna kiongozi anaona anauwezo ajiandae kugombea kwenye chama wakati ukifika kwani Jumuiya hii ndiyo inayobeba jumuiya zote za chama,"amesema Jumaa.
Aliongeza kuwa viongozi wanapaswa kuacha alama kwa kuwa na miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kununua ardhi pamoja na ofisi za makatibu wa jumuiya kwa kila wilaya.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Mkoa wa Pwani Josiah Jackson amesema kuwa uchaguzi umekwisha kilichobaki ni kujenga jumuiya na chama.
Jackson amesema kuwa wanachama waache makandokando kwa kuwaacha waliochaguliwa wafanye kazi zao na kuwaunga mkono ambapo kwa mkoa walipata madiwani 17 kutoka jumuiya.
Naye katibu wa CCM Mkoa wa Pwani Kitte Mfilinge amesema kuwa anaipongeza jumuiya kwa kufanya vizuri kwenye uchaguzi mkuu kwani mkoa umeshika nafasi tatu za juu hapa nchini.
Mfilinge amesema kuwa Jumuiya hiyo iko vizuri kwani ina mshikamano na imetulia hivyo kwa sasa wajiandae na uchaguzi wa jumuiya mwakani lengo ni kujenga chama ili kiwe imara.
Friday, January 23, 2026
AJIPATIA KIPATO KUPITIA PANYA WEUPE
Wednesday, January 21, 2026
FIDIA LAMI MAILI MOJA SHELI-MUHEZA ZAIVA
Diwani wa Kata ya Maili Moja Ramadhan Lutambi amesema kuwa zoezi hilo ni muhimu kabla ya kuanza kutekelezwa kwa mradi huo Uboreshaji Miundombinu ya Miji Tanzania (TACTIC) kwa Manispaa ya Kibaha.
Tuesday, January 13, 2026
BAGAMOYO SUGAR YATWAA UBINGWA MKOA WA PWANI
BAGAMOYO SUGAR BINGWA PWANI
BINGWA
Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.
Monday, January 12, 2026
BAGAMOYO SUGAR MABINGWA DARAJA LA TATU MKOA WA PWANI
Bagamoyo Sugar wametwaa ubingwa kwa jumla ya magoli 4-2 baada ya fainali ya kwanza kushinda kwa kupata ushindi wa goli 1-0.
Mchezo huo ulichezwa kwenye uwanja wa Mwendapole Wilaya ya Kibaha ulikuwa mkali na kuvutia mashabiki wengi wa Kibaha na Viunga vyake.
Kwa matokeo hayo timu ya Bagamoyo Sugar watawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya mabingwa wa mikoa.
Akikabidhi kombe kwa washindi mgeni rasmi wa mchezo huo huo Fidha Helmud (Tyson) ambaye ni Rais wa timu ya Barberian inayoshiriki ligi Daraja la Kwanza alizipongeza timu hizo kwa kuonyesha ufundi mkubwa wa kusakata kabumbu.
Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Soka Mkoa wa Pwani (COREFA) Robert Munisi amesema kuwa kufuatia kuwa mabingwa wa Mkoa huo watahakikisha wanaiunga mkono kwenye mashindano yanayofuata.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa mabingwa wapya wa Mkoa wa Pwani Bagamoyo Sugar amesema kuwa kwa kushirikiana na Chama Cha Soka Wilaya ya Bagamoyo (BFA) Kelvin Mawata amesema kuwa lengo ni kuhakikisha timu hiyo inafika mbali kwa kufanya vizuri.
Mwenyekiti wa Kiduli Fc Ally Masimike amesema kuwa amekubaliana na matokeo hayo ambapo timu hiyo itarudi kambini kwa ajili ya kujiandaa na mashindano mbalimbali.
BAGAMOYO SUGAR YATWAA UBINGWA MKOA WA PWANI
BARBERIAN YAICHAPA TMA
Tuesday, January 6, 2026
KIDULI FC YAJIPANGA KUPINDUA MATOKEO ILI KUTWAA UBINGWA WA MKOA WA PWANI
Kiduli inatarajia kucheza mchezo wa marudiano Januari 12 kwenye uwanja wa Mwendapole na mshindi wa jumla ndiye atakayekuwa bingwa wa ligi daraja la Tatu mkoa wa Pwani.
Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa timu hiyo Ally Masimike amesema wamepoteza mchezo huo kwa bahati mbaya.
Masimike amesema kuwa watarudi kwenye uwanja wa mazoezi na kufanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza kwenye mchezo wao wa kwanza.
"Lengo letu ni kupambana na kuhakikisha tunashinda ili kuwa mabingwa na kuuwakilisha Mkoa wetu kwenye michuano ya Mabingwa wa Mikoa,"amesema Masimike.
Bagamoyo Sugar iliifunga Kiduli Fc kwa goli 1-0 kwenye mchezo wa fainali ya kwanza kwenye uwanja wa Mwendapole Kibaha huku mchezo wa marudiano ukitarajiwa kupigwa kwenye uwanja huo huo ikiwa ni fainali ya pili ili kupata bingwa wa Mkoa.
Mbilinyi amewataka wadau wa michezo kujitokeza kwa wingi kwenye fainali hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na ushindani mkubwa kutokana na matokeo ya mchezo wa kwanza.
Bingwa wa ligi hiyo atapata kombe na atawakilisha Mkoa wa Pwani kwenye mashindano ya ligi ya Mabingwa wa mikoa.

















