Saturday, April 29, 2023

MAPATO YA UTALII YAONGEZEKA KUPITIA ROYAL TOUR

MAPATO ya utalii yaongezeka maradufu kutokana na watalii kuongezeka nchini kutoka Dola za Marekani 1.310.34 (Sawa na Shilingi Trilioni 3.01) mwaka 2021 hadi Dola za Marekani,527.77 (sawa la Shilingi Trilioni 5.82)  ukiwa ni   matunda ya filamu  ya The Royal Tour.

Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt Hassan Abbasi  wakati akielezea mafanikio ya  mwaka mmoja tangu Mhe Dkt  Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, alipozindua  filamu hiyo Jijini Arusha.

Amesema  filamu ya THE  ROYAL TOUR imejenga hamasa kwa watalii na wawekezaji na hamasa hiyo  imekuwa na manufaa katika sekta ya usafiri wa Anga hadi kuongeza Ruti na  Miruko ikiwemo ndege ya  kimataifa KIA imeongezeka  kwa asilimia 28 kutoka miruko 6,115 April 2021 hadi 7,850 April, 2023.

Aidha  amesema kuwa  Novemba mwaka jana huko Dallas,Texas, USA, Taasisi ya Tuzo za Afrimma ilimtangaza Rais Dkt. Samia  Suluhu Hassan kuwa Rais Mwanamke wa kwanza Afrika na Kushinda Tuzo ya Mageuzi Katika Uongozi .

Pia amesema kuwa filamu ya The Royal Tour sio ya  mwisho ni mwanzo wa kuitangaza nchi kimataifa zaidi hivyo Kamati ya mwaka mmoja sasa, imepokea na inaendelea kuchambua The royal Tours nyingine .


KIBONG’OTO KUWASILISHA MPANGO KAZI WA MATOKEO YA UTAFITI WA KIFUA KIKUU-PROF. NAGU


MGANGA Mkuu wa Serikali Prof Tumain Nagu ameitaka Hospitali ya Taifa ya Magonjwa ambukizi ya Kibongóto kwa kushirikiana na Mtandao wa Watu Waliougua Kifua Kikuu na Kupona (MTUKTA) kuhakikisha wanakuja na mpango kazi wa kufanyia kazi matokeo ya utafiti wa mwaka mmoja uliofanyika wa kuchunguza watu waliowahi kuugua kifua kikuu na kupona lakini baada ya kupona hawakufatiliwa kwa karibu.

Prof Nagu ametoa wito huo Jijini Dodoma katika ufunguzi wa kikao kazi cha usambazaji wa matokeo ya mwaka mmoja ambao umeweza kushirikisha watu waliowahi kuumwa kifua kikuu na kupona lakini baada ya kupona wakawa hawafuatiliwi kwa karibu kujua maendeleo yao.

Amesema kuwa wanatakiwa kuwasilisha mpango kazi kwa wizara kulingana na matokeo waliopata kutoka katika utafiti huo uliofanyika ili kuhakikisha wanaongeza umakini dhidi ya maambukizi ya kifuu kikuu nchini.

Naye Mkurungenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Magonjwa Ambukizi ya Kibongóto iliyopo Wilaya ya Siha Mkoa wa Kilimanjaro Dkt Leonard Subi amesema kuwa kupitia utafiti huo wameweza kupata zaidi ya watu 625 ambao walikuwa katika jamii na watu hao wamefanyiwa uchunguzi tena kuona kama hawana kifua kikuu.

“Katika watu 625 tulio wafanyia uchunguzi tumeweza kugundua asilimia 24 kati yao tayari walishaugua tena kifua kikuu na wapo katika jamii na watu 8 walikuwa ni wale walio na  kifua kikuu sugu”, ameeleza Dkt Subi.

Hivyo ametoa rai kuwa kuna umuhimu mkubwa sana wa kushirikisha jamii hususani katika kuwafuatilia kwa ukaribu watu waliougua kifua kikuu na kupona ili kujua maendeleo yao katika jamii.


Friday, April 28, 2023

NDOTO YA RAIS SAMIA YATIMIA KWENYE WIZARA YA MIFUGO NDANI YA RANCHI YA KONGWA.


SERIKALI kupitia wizara ya mifugo imeweza kuongeza vifaa vya malisho ya mifugo pamoja na Ngo'mbe 1,000 katika Ranchi ya Kongwa iliyopo Dodoma huku ikiwa na malengo ya kuhakikisha inatoa huduma Bora kwa wananchi Katika sekta ya ajira na uhuzaji wa majani ya  malisho ya mifugo.

Hayo yamesemwa  Tarehe 27 April 2023 na waziri wa mifugo na uvuvi Abdalah Ulega wakati wa uzinduzi wa vifaa vya malisho ya mifugo na ukaguzi wa Ngo'mbe 1,000 Katika eneo ilo la Narco.

Ulega amesema serikali imefanikiwa kununua Ngo'mbe hao pamoja vifaa hivyo vya malisho ikiwemo matreta manne, mower 3, Hay rake 10 pamoja na bailer 3 Ili  kuboresha maeneo ya Malisho.

Amesema mpaka Sasa nyama zinazouzwa kwenye Ranchi hiyo ni tani 12,000 na kwa muelekeo unaoelekea wataenda kuuza nyama hadi tani 50 mpaka tani 1,000.

Aidha amemtaka Mkurugezi wa Nacro kupendezesha eneo ilo kwa kuweka mipaka minzuri ya eneo Ili kunusuru mifugo isitoke ndani  eneo  ilo na kuhakikisha wafugaji ambao wamepewa kitalu kwenye eneo hilo wafuge kisasa na kutafutiwa masoko.

Awali  Mkurugezi mtendaji wa Ranchi ya taifa  ( Nacro) Prof Peter Msoffe  amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/2023 serikali ilitenga fedha kiasi cha shillingi bilioni 4.65 kwa ajili ya kuboresha na kuongeza uzalishaji katika Ranchi za Kongwa na Mzeri fedha hizo zilitengwa kwa ajili ya kununulia ng'ombe wazazi, vifaa vya shamba na uchungaji wa visima virefu.

Ikumbukwe kuwa Ranchi ya Kongwa ni miongoni mwa Ranchi kongwe za taifa iliyopo mkoani Dodoma wilaya ya Kongwa na  ndiyo ya kwanza kuanzishwa na ilianza Mwaka 1948 na eneo hilo lina ukubwa wa hekta 3,8000  zenye uwezo wa kuweka uniti za mifugo 25,000.



Wednesday, April 26, 2023

MILIONI 2.9 HUPOTEZA MAISHA



TAKWIMU za kidunia zilizotolewa na Shirika la Kazi Duniani mwaka 2022 zinaonesha kwamba zaidi ya watu milioni 2.9 hupoteza maisha kutokana na ajali na magonjwa yatokanayo na kazi.

Aidha zaidi ya wafanyakazi milioni 402 huumia wakiwa kazini na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kipindi chote wanachopatiwa matibabu hadi hapo watakapopona.

Akizungumza  na Waandishi wa habari Tarehe 26 April 2023 Jijini Dodoma kuelekea maadhimisho ya siku kuelekea kilele cha maadhimisho ya siku ya kimataifa ya usalama na afya mahali pa kazi Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi,Vijana,Ajira, na Wenye Ulemavu Prof Joyce Ndalichako amesema Kwa upande wa Tanzania jumla ya ajali na magonjwa yaliyoripotiwa katika Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kuanzia Julai 2019 hadi Juni 2021 ni ajali 4,993 na magonjwa 249. Katika ajali hizo vifo vilikuwa 217.

Prof Ndalichako amesema kuwa maadhimisho hayo yatafanyika kitaifa Mkoani Morogoro katika viwanja vya Tumbaku Aprili 28,2023 na lengo kubwa la maadhimisho hayo ni kuendeleza kampeni za kuhamasisha na kuweka mazingira salama katika sehemu za kazi miongoni mwa wadau kupitia kauli mbiu mbali mbali ambazo hutolewa na Shirika la Kazi Duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu ni: “Mazingira Salama na Afya kazini ni Kanuni na Haki ya Msingi Mahali pa Kazi” (A Safe and Health Working Environment is a Fundamental Principle and Right at Work).

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa OSHA, Bi. Khadija Mwenda amesema kuwa moja kati ya eneo ambalo ajali nyingi zinaripotiwa ni katika sekta ya Uzalishaji ambapo imeajiri vijana wengi huku wengine wakiwa hawana ujuzi wa kutosha katika nafasi wanazofanyia kazi.

Mwenda amesema kuwa OSHA imejipanga vyema kuelekea maadhimisho hayo ya 19 ambapo washiriki wote watapatiwa Mafunzo ya Usalama na Afya miongoni mwa makundi mbali mbali wakiwemo wajasiriamali wadogo, wafanyakazi wa viwandani, wachimbaji wadogo pamoja na watu wenye ulemavu.

Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani ilianza mwaka1996 Nchini Marekekani Katika Jiji la New York, ambapo waathirika wa watu walioumia na kupoteza maisha wakiwa kazini hukumbukwa. Maadhimisho hayo yalikuwa yakifanywa na Chama Cha Wafanyakazi Duniani. Ilipofika mwaka 2001,Shirika la Kazi Duniani liliona kuwa ni busara kubadilisha madhumuni ya siku hiyo na kuiita “Siku ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani


Mwisho.

KUNENGE AZINDUA DARAJA LA MIPEKO

MKUU wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge leo Aprili 26, 2023 amezindua Daraja la Mipeko iliyopo Barabara ya Mwanambaya lenye thamani ya shilinigi milion 214.

Kunenge akisalimia wananchi wa Mipeko  amepongeza Dkt Samia Suluhu Hassan  kwa kuleta Maendeleo ambayo yanamgusa mwanachi wa kawaida.

Ameeleza kuwa Rais alipofanya ziara Mkoani Pwani alisema nia yake ya kuhakisha Mkoa unapata Miundombinu ya yote muhimu ya Afya, Elimu, Maji, Nishati, Barabara.

Aidha amesema kuwa mkoa huo una Mtandao wa Barabara wa km 6629 zinazohudumiwa na TANROADS na TARURA. 

Ameongeza kuwa bajeti ya kutekeleza  shughuli za Barabara kwa mwaka 2021/22 ilikuwa ni bilion75.5 na kwa mwaka 2022/23 imeongezwa kufikia bilion 81.

Amewataka Wananchi wa eneo hilo kulinda Daraja hilo na kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa  Halmshauri ya Mkuranga kupanga Mji wa Mkuranga kwa kuwa Mji huo unakuwa kwa kasi.

Kunenge ameeleza Serikali inafanyia kazi maombi ya Wananchi hao ya kujengewa Kituo cha Afya, kupelekewa Umeme na ujenzi wa Daraja.

Wednesday, April 19, 2023

WAZIRI JAFO AUPONGEZA MKOA WA PWANI KWA KAMPENI YA UPANDAJI MITI



WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Suleiman Jafo ameupongeza Mkoa wa Pwani kwa kuweka kampeni ya upandaji miti ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira.

Jafo aliyasema hayo kwenye shule ya sekondari Ruvu Mlandizi Wilayani Kibaha wakati akizundua Kampeni ya utunzaji mazingira na matumizi ya nishati mbadala kwa mkoa huo iliyoandaliwa na benki ya NMB Wakala wa Misitu Tanzania TFS Mkoa wa Pwani, ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Pwani na Taifa Gesi.

Alisema kuwa kwa kampeni hiyo kwani itasaidia kutunza mazingira pia utasaidia kutangaza teknolojia mbadala ya matumizi ya nishati mbadala baada ya kupunguza matumizi ya miti kama nishati kwa ajili ya kupikia na matumizi mengine ya binadamu ya kila siku.

Aidha alisema kuwa mkoa wa Pwani ni moja ya mikoa minne ambayo imeathirika kwa kiasi kikubwa na uharibifu wa mazingira lakini baada ya kupata maelekezo kutoka kwa Rais Dk Samia Suluhu Hassan ya kutaka mikoa hiyo iweke mipango ya kukabili hali hiyo mkoa umejiongeza kwa kuwa na kampeni hizo za kukabili changamoto za mazingira.

Awali akimkaribisha Waziri Jafo akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abubakar Kunenge Mkuu wa wilaya ya Kibaha Nickson John alisema kuwa mkoa umeweka mikakati mbalimbali ili kutunza mazingira ikiwa ni pamoja na kupanda miti million 13.5 lakini hadi sasa wameshapanda miti milioni 9.7 ikiwa ni zaidi ya asilimia 70 ya malengo ili kurejesha uoto wa asili.

Naye Mkurugenzi wa kampuni ya Taifa gesi Anjela Bhoke alisema kuwa kila mwaka hekari 400,000 za miti zinapotea kutokana na matumizi mbalimbali ya miti ambapo moja ya mikakati yao ni kujenga kiwanda cha kutengeneza mitungi ya gesi ambapo wako tayari kusambaza gesi majumbani na kwenye taasisi za umma.

Mwakilishi wa benki ya NMB Seka Urio alisema kuwa wametenga kiasi cha shilingi milioni 470 kwa ajili ya shule zitakazopanda miti 2,000 na kuitunza kwa asilimia 80 ambapo itapatiwa milioni 50, huku mshindi wa pilia kwa kupanda miti 1,500 akipata milioni 30 akiitunza kwa asilimia 70 na watatu akipata milioni 20 kwa kupanda miti 1,000 itakayokuwa imetunzwa kwa asilimia 70.


Tuesday, April 18, 2023

TANZANIA KUBORESHA MAWASILIANO

 


SERIKALI ya awamu ya sita inayoongozwa na Dkt Samia Suluhu Hassan imedhamiria kuhakikisha Tanzania inakuwa na miundombinu bora ya mawasiliano yenye kutumia Teknolojia ya kisasa ambayo italeta tija na ufanisi katika kuongeza uzalishaji na ujenzi wa uchumi na kuimarisha usalama na ulinzi wa Taifa.

Hayo yamesemwa Waziri wa Habari Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Nape Moses Nnauye katika hafla ya utiaji saini kati ya TTCL na HUAWEI kuhusu upanuzi wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano katika Wilaya 23  uliyofanyika Jijini Dodoma.

Nape amesema zaidi ya  shilingi  bilion 37 zitangharimu ujenzi wa kilometa 1,520 ambazo zitaunganisha Wilaya 23 katika upanuzi wa mkongo wa Taifa wa mawasiliano kati ya shirika la mawasiliano Tanzania na kampuni ya HUAWEI International.

Amesema kuwa mradi huu unaenda kuleta mageuzi makubwa yakiwemo kukuza matumizi ya tehama Wilaya kuongeza kasi ya ukusanyaji mapato pamoja na kuleta fursa kwa wananchi kiuchumi.



Awali kwa upande wake Mkurugezi mkuu wa TCCL  mhandisi Peter Ulanga 

Amesema mradi huu utatoa fursa nzuri kwa wizara , Taasisi za umma na Taasisi binafsi kufikisha huduma Zao kwa wateja na watumiaji wao kwa haraka na wakati kwa kuwa mkongo wa Taifa utakuwa na uwezo mkubwa wa kubeba taarifa za kutuma kwa haraka.

Monday, April 17, 2023

RIDHIWANI AGAWA ZAWADI UHIFADHI QURAAN

Nimeshiriki kugawa zawadi katika mashindano ya Kimataifa ya uhifadhi wa Quraan yaliayofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam. Namshukuru Mwenyezi Mungu kwa fursa hii.

Saturday, April 15, 2023

RIDHIWANI KIKWETE AWASHUKURU WANACHALINZE KWENYE FUTARI


Nimeshiriki futari na Wananchi wenzangu wa Halmashauri ya Chalinze pamoja na viongozi wa Chama na Serikali wa wilaya yetu. Nawashukuru sana Wananchi wenzangu kwa muitikio wenu. Asanteni sana. #RamadhanKareem #Chalinze.

Wednesday, April 12, 2023

BAJETI OFISI YA WAZIRI MKUU


Nimeshiriki kikao cha Bunge kinachojadili Bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu 2023/24. #KaziInaendelea #Bajeti2023

Friday, April 7, 2023

SERIKALI YABORESHA HUDUMA ZA MAJI.


Na Wellu Mtaki, Dodoma

SERIKALI ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dk Samia Suluhu Hassan imefanya jitihada kubwa katika kufanya mabadiliko na maboresho makubwa katika Sekta ya Maji  ikiwa pamoja na kuongeza uwekezaji katika sekta hiyo ili kukabiliana na changamoto zilizoko. 

Hayo yamesemwa na mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Sinyamule wakati wa ufunguzi wa tafiti juu ya maombi ya kurekebisha bei za huduma ya maji safi iliyoletwa na mamlaka ya maji safi na usafi wa mazingira Dodoma ( DUWASA)

Sinyamule amesema  kuwa lengo kubwa la Serikali katika kufanya mabadiliko na kuongeza uwekezaji katika sekta ya Maji ni kuongeza ubora na upatikanaji wa huduma ili kuboresha maisha ya Wananchi wake na hatimaye kufikia lengo la asilimia 95 (kwa mijini) lililowekwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ifikapo mwaka 2025.

Awali mwakilishi wa  Mkurugezi mkuu wa Ewura  George Kabelwa katika maombi hayo Mamlaka ya Maji Dodoma imeomba kufanya marekebisho ya bei zitakazotumika kwa kipindi cha miaka mitatu kuanzia mwaka 2023/24 hadi 2025/26  kwa mujibu wa maombi yaliyowasilishwa EWURA, Mamlaka ya Maji Dodoma imebainisha kuwa marekebisho ya bei ya maji yanalenga kupata fedha za kutosha kukidhi gharama halisi za uendeshaji na matengenezo kwa lengo la kuboresha huduma zitolewazo.

Aidha Mamlaka ya Maji Dodoma imeeleza kuwa bei zinazopendekezwa zitaiwezesha mamlaka kumudu gharama zote za utoaji huduma   pamoja na mambo mengine, kuendelea kuongeza ubora wa maji, kuiwezesha mamlaka kuwa endelevu na kukidhi matarajio ya wana Dodoma.  

Kwa upande wa wakilishi wa wananchi Revina Petro Lamiula  ametoa maoni kwa kusema kuwa pamoja na bei kupandishwa ila wanaitaka mamlaka ya maji safi (Duwasa) kuhakikisha wanaboresha huduma zao.

Wednesday, April 5, 2023

WATAKIWA KUTUMIA VANILLA MARA KWA MARA

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MKURUGENZI Mkuu wa Vanilla International Limited Simon Mnkondya ameitaka jamii kutumia zao la Vanilla katika matumizi ya kila siku kwani zao hilo huchochea kuwa na akili zaidi.

Mnkondya amebainisha hayo Jijini Dodoma kwenye kikao Cha wadau wa zao la Vanilla.

Amebainisha kuwa ili kuweza kuwa na akili nyingi,hata wanasayansi Duniani wamekuwa wakitumia malighafi inayopatika katika zao la Vanilla hali inayopelekea kuwa wabunifu na kubuni vitu mbalimbali.

Aidha Mnkondya amebainisha kuwa vyama vya ushirika vimekuwa vikiwaibia wakulima bila kuwatengenezea masoko ya uhakika na badala yake vimekuwa vikitengeneza wezi.

Pia amebainisha kuwa kilimo Cha Vanilla soko lake linapatikana Kwa wingi katika nchi za uarabuni na Vanilla inayonuniliwa sana ni Vanilla ya gradi la kwanza.

Katika kuuza zao la Vanilla Kwa Duniani ya sasa Mnkondya amebainisha kuwa haina haja ya kubeba mzigo kupeleka katika nchi unaweza kuuza kupitia mtandao Kwa kuandika vigezo vya zao lako la Vanilla na wateja wakakufata wenyewe.

Ameongeza kuwa zao la Vanilla halitakiwi kulimwa kiholela na badala yake amewashauri wakulima kulima,kulima Kwa pamoja kilimo Cha Block Farming.

WATAKIWA KUPINGA UKATILI

Na Mwandishi Wetu, Dodoma

MKUU wa Mkoa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewaasa wananchi wa Kata ya Chang'ombe kukubali kubadilika kupinga Ukatili kwa kushirikiana pamoja ili Mkoa wa Dodoma kuwa wa Mfano kwa maendeleo ya Taifa. 

Ameyasema hayo aliposhiriki katika Kongamano la Kupinga Ukatili Mkoa wa Dodoma lililoandaliwa na kamati ya kutokomeza Ukatili wa Kijinsia na Msaada wa Kisheria, kupitia kikundi cha Wanawake na Samia na kusikiliza kero za wananchi wake katika Mtaa wa Mazengo Chang'ombe. 

Senyamule amesema kuwa Chang'ombe bila vitendo vya kikatili inawezekana na kutoa rai kwa wazazi na walezi wa Kata ya Chang'ombe kutoficha vitendo viovu vya watoto na vijana katika jamii inayowazunguka ili jitihada za pamoja za kutokomeza vitendo vya kikatili ziweze kufanikiwa.

Aidha, Mhe. Senyamule ameendelea kumshukuru Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuimarisha Mkoa wa Dodoma kwa miradi mikubwa ya kimkati ambayo ni fursa kwa vijana ambayo ni fursa kwao kujishughulisha na shughuli za uzalishaji mali kwani wana sehemu ya kupeka nguvu kazi zao ili kujiepusha na tabia zisizo na Maadili.

"Mimi kama Mkuu wa Mkoa wa Dodoma ningetamani kila Kata, Mtaa, Kaya na kila nyumbani isiwe na mhalifu wala mtu yeyote anaefanya ukatii na unyanyasaji wa kijinsia, lakini itawezekana kama sisi wananchi tutaamua kuungana na juhudi na dhamira nzurii za Serikali 

"Vijana mjipange kubadilika sisi kama Mkoa tunadhamira njema na kizazi cha nchi hii, ni wakati sahihi wakujiwekea sheria ambazo tutasimamia wenyewe zinazohusu Ukatili wa Kijinsia kwani inawezekana kubadilika kusiwe na vijana vibaka, wezi ili kupongeza wale wenye Maadili mazuri na kuwa mfano wa kuigwa "Amesema Senyamule. 

Naye Mwanakamati ya kupinga Ukatili Fatuma Madidi ametoa elimu juu ya Ukatili wa nafsi, watoto, vijana, wazee na Wanawake ili kuweza kutambua Madhara ya Ukatili kwa Ujumla na kuendelea kujihadhalisha .

Kwa Upande wake Diwani wa Chang'ombe Bw. Bakari Fundikira amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa ujio wake katika kata yake na kuahidi kuendelea kutekeleza maelekezo yake.