Na John Gagarini, Mkuranga
WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa nchi inauwezo wa kuzingatia Utumishi kwenye sekta binafsi ili wawekezaji watumie vijana wa hapa nchini na kuachana na mawazo ya kuleta wafanyakazi kutoka nje ya nchi kwani Watanzania wanaajirika na ni waaminifu.
Majaliwa aliyasema hayo Kisemvule Wilayani Mkuranga Mkoani Pwani alipokuwa anazindua kiwanda na mabati cha Lodhia Group of Company na kusema kuwa vijana wa Kitanzania wanauwezo wa kufanya kazi na hakuna sababu ya wafanyakazi kutoka nje ya Tanzania.
Alisema kuwa vijana wa Kitanzania wanaajirika na wanafanya kazi kwa bidii na kwa sasa hata vitendo vya kutopenda kufanya kazi hilo halipo tena wanawajibika ipasavyo.
"Waajiriwa zaidi ya 3,000 kitendo cha kutoa ajira umesaidia sana tutakuunga mkono uendelee kutoa vijana ambao wako mtaani itasaidia kufanya nchi kuwa na amani nchi imepanua wigo na fursa za uwepo wa viwanda,"alisema Majaliwa.
Aidha alisema uwepo wa kiwanda hicho umesaidia kutoa ajira na hiyo ni fursa kwa wengine inasaidia kuzalisha na kupanua wigo ili kusaidia watu wengine zaidi hapa ni ajira zaidi ya 2,500 hilo ni jambo kubwa.
"Serikali ya awamu ya sita imeweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji kuja kuwekeza kwa wale wa ndani na nje maelekezo tuliyopewa kuanzia kuomba kuwekeza na kuanza uwekezaji ni kuhakikisha hawapati shida wala kikwazo chochote ili kila upande unufaike mwekezaji na mwananchi,"alisema Majaliwa.
Aliongeza kuwa kampuni hiyo ni moja ya kampuni inayolipa kodi kubwa nchini ambapo inalipa zaidi ya bilioni 40 kwa mwezi ni kama lulu watatatua changamoto zinazoikabili kwani nachangia pato la serikali na kusaidia huduma za jamii na inamuunga mkono Rais kwa kupunguza changamoto ya ajira.
"Hapa Tanzania ni sehemu salama ya uwekezaji tunatambua na tunaheshimu uwekezaji huu kwani huyu ni wa kuenziwa na Halmashauri ili wapate fedha zaidi na hatimaye nchi inufaike hakika leo nimefurahi sana kutembelea kiwanda hichi ambapo Arusha nlitembelea walikuwa na kiwanda kidogo sana uwekezaji mkubwa na malengo kuweka mradi mkubwa zaidi naifurahi kutembelea,"alisema Majaliwa.
Alibainisha kuwa kiwanda hicho kinachozalishwa chuma mbalimbali zikiwemo nondo ni kikubwa kuliko viwanda vyote alivyotembelea na kuweka jiwe la msingi la kiwanda ukubwa wake ni hekari nane na nusu kitatengeneza bati.
"Uwepo wa viwanda vya nondo, plastiki, mabomba ya maji na bati itasaidia bidhaa kwani zitapatikana hapa nchini badala ya kuagiza nje na pia zina ubora bado eneo dogo kufikia kiwanda cha Afrika Mashariki itafikia hatua hiyo na kuwa kiwanda kikubwa hapa Afrika Mashariki,"alisema Majaliwa.
Aliongeza kuwa uwepo wa viwanda vijana Teknolojia na hilo limepewa kipaumbele ili wajifunze kupitia mitambo hiyo ya kisasa ni faida ya uwepo wa viwanda nchi itakuunga mkono na milango itakuwa wazi na azma ya kutembelea ni kuangalia uwekezaji unaofanywa ukiwemo kwenye mabomba ya maji na serikali inaona kuwa anafunga mkono jitihada za Rais Samia Suluhu Hassan alisema na kuwahakikshia kuwa uwekezaji hautakwama hata kidogo.
Kwa upande wake Mwenyekiti na mwanzilishi wa kampuni hiyo Haroun Lodhia alisema kuwa kiwanda chao kinalipa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 22 kwa ajili ya umeme na gesi ambapo baadaye watakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 40,000 za chuma kwa mwezi.
Lodhia alisema kuwa kwa siku za baadaye watazalisha umeme wao wenyewe ambapo wataanza kuzalisha megawati tano na baadaye kva 25 na wanaishukuru serikali kwa kuwawekea mazingira mazuri kuendesha shughuli zao.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Mkuranga Abdala Ulega alisema kuwa kutokana na uwekezaji mkubwa uliopo kwenye Wilaya ya Mkuranga na wingi wa magari yanayokwenda mikoa ya Kusini wangeomba barabara ya Kusini ipanuliwe na kuwa ya barabara nne.
Ulega alisema kuwa barabara hiyo kuanzia Mbagala Rangitatu kwenda Mwandege Vikindu na kuendelea ingepanuliwa ili bidhaa ziweze kwenda kwa urahisi na pia hapo Mkuranga viwanda vingi tumia umeme mkubwa na hakuna gari la Zimamoto ikitokea moto itakuwa ni shida sana hivyo wapatiwe huduma ya gari hilo.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment