PUNGUZENI VITENDO VYA UKATILI WA KIJINSIA MIMBA ZA UTOTONI
Na Wellu Mtaki, Dodoma
MKURUGENZI wa shirika la Kivulini linalojishughulisha na mapambano dhidi ya ukatili wa kijinsia na mimba za utotoni Yasini Ally amesema kuwa hali ya vitendo vya ukatili na mimba za utotoni katika mikoa ya Kanda ya Ziwa ipo kwa kiwango cha juu hivyo serikali na wadau wote hawana budi kushirikiana ili kuweza kukabiliana na tatizo.
Ally amesema hayo Jijini Dodoma alipokuwa akifanya mahojiano na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari juu ya utendaji kazi wa shirika lake.
Amesema kuwa Utafiti uliofanywa na shirika hilo umebaini katika kipindi cha mwaka 2015/ 2016 vitendo vya ukatili wa kijinsia ulikuwa wa hali ya uu ambapo mkoa wa Shinyanga ni asilimia 78, mkoa wa Mwanza asilimia 60 , mkoa wa Kigoma asilimia 61 na mkoa wa Mwanza pia una asilimia 25 kwa vitendo vya mimba za utotoni.
Aidha amefafanua kwamba hali hiyo pia inaweza kusababishwa pale jamiii ya kanda ziwa inapokuwa na hali nzuri ya kiuchumi kwa mfano wakati wa mavuno baadhi ya watu hutelekeza familia na kwenda kwenye mambo ya starehe.
Mkurugezi huyo ameongeza kuwa shirika Ilo limefanya kazi kubwa ya kujenga uwezo kwa klabu za wanafunzi Ili kudhibiti mimba za utotoni.
No comments:
Post a Comment