Na
Mwandishi Wetu, Kibaha
MGOMBEA
Udiwani wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kata ya Kawawa Jimbo la
Kibaha Vijijini Otto Kanyonyi amesema kuwa endapo atafanikiwa kuchaguliwa
kwenye nafasi hiyo atatoa asilimia 50 ya posho zake atakazokuwa anapata kwenye
vikao vya madiwani kwa ajili ya
kuchangia shughuli za maendeleo kwenye kata hiyo.
Kanyonyi
aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari huko Mlandizi
Kibaha juu ya mikakati yake ya kuwaletea maendeleo wakazi wa kata hiyo endapo
atashinda kwenye nafasi ya udiwani kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 25
mwaka huu.
Alisema
kuwa moja ya mkakati wake ambao ataupa kipaumbele ni ujenzi wa zahanati katika
kata hiyo ili kuwapatia huduma wananchi badala ya kupata huduma hizo kwenye
kata za jirani.
“Endapo
nitafanikiwa kuwa diwnai wa kata yetu ya Kawawa nitahakikisha natoa asilimia 50
ya posho nitakayokuwa npata naitoa kwa ajili ya shughuli za maendeleo hasa zile
huduma za jamii ikiwa ni pamoja na afya, elimu na maji,” alisema Kanyonyi.
Aidha
alisema kuwa ameamua kujitolea posho hizo kutokana na kuwa na uchungu wa
maendeleo na kuona kuwa moja ya njia za kuleta maendeleo ni kuchagia kwa hali
na mali.
“Fedha
hizo nataka zilete maendeleo katika kata yangu kwani ili kufanikisha mambo
kiongozi lazima uonyeshe njia kwa wale unaowangoza hivyo na mimi nataka niwe
kiongozi wa mfano ili niache kumbukumbu kuwa nilihamasisha maendeleo,” alisema
Kanyonyi.
Alibainisha
kuwa wananchi wanakabiliwa na changamoto nyingi hivyo moja ya njia za
kuwahamasisha kujiletea maendeleo ni pamoja na kuchangia shughuli za maendeleo.
Mwisho.
Na
John Gagarini, Chalinze
UMOJA
wa Wanawake Tanzania (UWT) wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani umetoa salamu za
rambirambi kufuatia kifo cha mwenyekiti wa tawi la Ubena Zomozi Kido Antoni (65)
kufariki dunia wakati wa mkutano wa kampeni wa diwani wa kata ya Ubena Jimbo la
Chalinze.
Mwenyekiti
huyo wa tawi alifariki Septemba 30 majira ya saa 7 mchana wakati wakiwa kwenye
shamrashamra ya kuwahamasisha wananchi kujiandaa kwa kucheza huku wakimsubiri
mgombea udiwani wa kata hiyo kupitia CCM Nicholaus Muyuwa kwa ajili ya mkutano
wa kampeni.
Akitoa
salamu za pole katibu wa UWT wilaya ya Bagamoyo Mwatabu Hussein alisema kuwa
wameupokea msiba huo kwa masikitiko makubwa kwani marehemu alikuwa kwenye
harakati za kukipigania chama wakati huu wa kampeni kuelekea uchaguzi mkuu.
Hussein
alisema kuwa familia pamoja na chama vimepata pigo kubwa la kuondokewa na
kiongozi wao na kumwomba Mungu aipe nguvu katika kipindi hichi bkigumu cha
majonzi.
“Tunawapa
pole familia pamoja na chama kwa kuondokewa na mpendwa wao kwani alikuwa kwenye
harakati za kuhakikisha chama kinapata ushindi kwenye uchaaguzi wa wagombea wa
chama kuanzia Rais, Mbunge na Diwani,” alisema Hussein.
Kwa
upande wake mgombea huyo wa udiwani Muyuwa alisema kuwa kifo amekipokea kwa masikitiko
makubwa kwani marehemu alikuwa mtu muhimu sana ndani ya chama na amekufa wakati
akipambana kuhakikisha ushindi unapatikana.
Muyuwa
alisema kuwa marehemu alikuwa mzima kabisa na alikuwa kifurahi na wenzake na
kutoa hamasa kwa wananchama na wasio
wanachama juu ya kukipigia kura ili kiweze kushinda kwenye uchaguzi m kuu ujao.
Alisema
kuwa marehemu alianguka ghafla wakati wakimsubiri yeye aweze kufika kwa ajili
ya kuhutubia kwenye mkutano wa kampeni na baada ya kuanguka walimpeleka kwenye
zahanati ya Ubena Estate na alifariki wakatia kipatiwa matibabu.
Naye
mgombea Ubunge kwenye Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alifika nyumbani kwa
marehemu na kutoa salamu za pole kwani wakati tukio hilo linatokea mgombea huyo
alikuwa kwenye mkutano wa kampeni katika kata hiyo kwenye Kijiji cha Mdaula.
Taarifa
toka kwa daktari mfawidhi wa zahanati hiyo zilisema kuwa alikufa kutokana na
presha na upungufu wa damu, marehemu alizikwa juzi kwenye makaburi ya Ubena na
ameacha watoto watano.
Mwisho.
Na John Gagarini, Bagamoyo
MGOMBEA ubunge jimbo la
Bagamoyo kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM),Dk Shukuru Kawambwa, amesema endapo
atachaguliwa kuongoza Jimbo hilo atahakikisha zahanati ya Yombo inapandishwa
hadhi na kuwa kituo cha afya ili kupanua huduma za kiafya.
Sambamba na kupandishwa hadhi
kwa zahanati hiyo pia Dk Kawambwa atahakikisha
kunakuwa na gari la kubeba wagonjwa wanaopata rufaa kwenda hospitali kubwa tofauti na ilivyo sasa.
Dk Kawambwa aliyasema hayo
kwenye Kijiji cha Yombo wakati wa mkutano wa kampeni na kusema kuwa vipaumbele
vyake ni kuhakikisha huduma muhimu za jamii zinapatikana kwa uhakika.
“Mara zahanati hii ikipandishwa
hadhi na kuwa kituo cha afya huduma zitaboreka ikiwa ni pamoja na kuwa na
wataalamu wa kutosha na huduma nyingi zitatolewa hapa hivyo itapunguza kutumia
muda mwingi kufuata huduma mbali,” alisema Dk Kawambwa.
Aidha alisema kuwa pia
kipaumbele kingine ni kuhakikisha anasimamia utekelezaji wa ujenzi wa barabara
kutoka Makofia-Yombo hadi Mlandizi-Mzenga kwa kiwango cha lami Dk ambapo kwa
sasa upembuzi yakinifu umeshafanyika na kilichobakia ni tathmini ya
watakaolipwa fidia ambako itapita barabara pamoja na hatua nyingine ili kupisha
mpango huo.
“Utekelezaji wa ujenzi wa barabara
hiyo kuwa kwa kiwango cha lami upo katika ilani ya Chama Cha Mapinduzi
2015-2020 na ukamilikaji wake utafungua fursa nyingi za kiuchumi hivyo kuleta maendeleo
na kuinua uchumi wa wananchi,” alisema Dk Kawambwa.
Katika hatua nyingine alisema
kuwa atahakikisha wakazi wa kata ya Yombo na maeneo ambayo hayajafikiwa umeme
kuwa atashirikiana na tanesco kupitia mradi wa wakala wa umeme vijijini (REA) kuondoa
tatizo hilo ndani ya miaka mitano ijayo.
"Nitahakikisha nasimamia
mipango yote,na ilani ya chama changu ili niweze kupunguza makali ya kero
zinazowakabili wana Bagamoyo ikiwemo kwenye afya,maji,nishati ya umeme ,elimu
na miundombinu"alisema Dk.Kawambwa.
Kwa upande wake mgombea udiwani
kata ya Yombo jimbo la Bagamoyo, kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Mohamed Usinga,aliwaahidi wakazi wanaoishi katika vijiji vinavyounda kata hiyo
kuwa atahakikisha anamalizia kazi ya kusambaza maji, umeme na kituo cha afya
kilichopo katani humo.
Alieleza kuwa pindi wakazi hao
wakimpatia ridhaa ya kushika nafasi hiyo atapambana ili kumalizia kazi ambayo
ilikuwa imeanzwa na mtangulizi wake Ubwa Idd Mazongera ambaye kwa sasa
ametangulia mbele za haki.
Awali akiwanadi wagombea
hao,meneja kampeni jimbo la Bagamoyo,AbdulSharif alisema wananchi jimboni hapo
wasifanye makosa kuchagua wapinzani bali wawachague wagombea kupitia CCM.
Mwisho
No comments:
Post a Comment