Na John Gagarini, Chalinze
MGOMBEA Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John
Magufuli amepongezwa kwa kuuachia mkoa wa Pwani hususani wilaya ya Bagamoyo
miradi mikubwa ambayo itakapokamilika itasaidia kuinua kipato cha wakazi wa
mkoa huo.
Miradi hiyo ambayo inatoka kwenye Wizara Ujenzi na
Miundombinu aliyokuwa akioongoza Dk Magufuli kabla ya kuteuliwa na chama chake
kuwa mgombea Urais kwenye kinyanganyiro kitakachofanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Pongezi hizo zimetolewa na mgombea Ubunge wa Jimbo la Chalinze
kupitia chama hicho Ridhiwani Kikwete, wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika
kwenye Kijiji cha Miono wilayani Bagamoyo na kusema kuwa mgombea huyo kila mkoa
ameupatia miradi ambayo itachochea maendeleo.
Ridhiwani alisema kuwa Dk Magufuli ni kiongozi ambaye
anastahili kuongoza nchi hii kwani wakati akiwa waziri alihakikisha kila mkoa
unatumia rasilimali zake viuzuri ili kujiletea maendeleo hali ambayo
imesababisha nchi kupiga hatua.
“Sisi wakazi wa wilaya ya Bagamoyo tunamshukuru kwani ametuachia
miradi mikubwa ikiwa ni pamoja na ule wa Barabara ya Afrika Mashariki
itakayoanzia Bagamoyo, Makuruge, Saadani hadi mkoa wa Tanga hadi Mombasa nchini
Kenya,” alisema Ridhiwani.
Alisema kuwa mradi mwingine ni ule wa Bandari ambayo itakuwa
ni kubwa ambao utaanza wakati wowote kuanzia sasa kwani mipango tayari
imekamilika huku mradi wa barabara tatu zitakazoanzia Jijini Dar es Salaam hadi
mkoani Morogoro pia mzaini wa kisasa uliopo Vigwaza ambao tayari unafanya kazi.
“Mradi mwingine ni ule wa upanuzi wa Daraja la Mto Wami ili
kupunguza ajali zinazotokea kwenye daraja hilo ambapo kwa sasa magari hayawezi
kupishana, hakika miradi hii ni mikubwa na itafungua fursa za maendeleo kwa
kukuza uchumi wao kutumia fursa zilizopo na zitakazokuwepo kwenye miradi hiyo,”
alisema Ridhiwani.
Aidha alisema Dk Magufuli ni kiongozi ambaye hana kashfa
yoyote na ameonyesha kuwa anafaa kuliongoza Taifa la Tanzania kutokana na
uchapa kazi wake pamoja na uadilifu aliokuwa nao ukilinganisha na viongozi
wengine wanaowania nafasi hiyo.
Aliwataka watanzania kumchagua kwa kumpiga kura nyingi za
kishindo ili awe Rais wa awamu ya tano na anaamini kuwa uwezo wa kuongoza nchi
anao akiwa chini ya CCM ambao kwa wakati huu imechagua viongozi wenye sifa na
wanaopendwa na wananchi.
Mwisho.
Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akizindua huku akiwa amekaa kwenye kigoda tawi la vijana wa Boda boda kwenye Kijiji cha Pongwemnazi |
Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze kupitia CCM Ridhiwani Kikwete akizindua tawi kwa kupandisha bendera kwenye moja ya matawi wakati wa kampeni kuwania kiti hicho. |
Mgombea Udiwani kata ya Kimange kwa tiketi ya CCM Husein Hadingoka akiwahutubia wananchi wa Kijiji cha Kikwazu wakati wa mkutano wa kampeni |
Mama Mwenye ulemavu ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja akiwa kwenye mkutano wa kampeni wa Mgombea wa CCM Ridhiwani Kikwete kwenye Kijiji cha Pongwemnazi kata ya Kimange. |
Baadhi ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea wa CCM Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kwenye kijiji cha pongwekiona kata kimange wilayani bagamoyo |
wananchi wa kijiji cha pongwekiona wakiwa wanamsikiliza mgombea ubunge jimbo la chalinze ridhiwani kikwete hayupo pichani wakati wa mkutano wa kampeni |
Mwigizaji aitwaye Puto akitoa burudani kwa wananchi waliohudhuria mkutano wa kampeni kwenye kijiji cha Pongwemnazi kata ya Kimange wilayani Bagamoyo |
Mwimbaji Sam wa Ukweli akiimba na moja ya wananchi kwenye mkutano wa kampeni wa CCM kwenye kijiji cha Pongwemnazi |
Wagombea Ridhiwani Kikwete kushoto akicheza na mgombea Udiwani kata ya Kimange Hussein Hadingoka wakati wa uzinduzi wa kampeni za udiwani kwenye kijiji cha Pongwekiona |
Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete akimkabidhi moja ya wanachama wapya kwenye Kijiji cha Pongwekiona |
No comments:
Post a Comment