Thursday, October 22, 2015

DK MAGUFULI KUUFANYA MJI WA CHALINZE KUWA WA KISASA

Na John Gagarini, Chalinze
MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli emesema kuwa endapo atachaguliwa kuwa Rais atahakikisha mji wa Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani unakuwa moja ya miji ya kisasa na wa uwekezaji ambapo utakuwa na barabara za juu Fly Over.
Aidha ujenzi huo ambao utakuwa wa barabara sita hadi jijini Dar es Salaam utagharimu kiasi cha shilingi trilioni 2.3 na Chalinze itakuwa kiunganishi cha njia hizo kwenda mikoa ya Kasakazini na mikoa ya Kati ambapo tayari wataalamu wa upembuzi wa ujenzio huo wamelipwa kiaisi cha shilingi billion 7.7.
Aliyasema hayo kwenye mkutano wa kampeni kwenye Jimbo la Chalinze mkoani humo ambapo alisema kuwa atahakikisha mji huo unakuwa wa kisasa na huduma zote muhimu zinapatikana hapo na kuwa mji mbadala wa Dar es Salaam.
Dk Magufuli ambaye ni Waziri wa Ujenzi na Miundombinu alisema kuwa mji huo utakuwa kituo kikubwa cha uwekezaji hapa nchini kwani faida nyingine iliyopo ni kugunduliwa gesi eneo la Ruvu hivyo kufanya uchumi wa mji huo kuwa juu na wananchi wataboresha maisha yao na kuwa na maisha bora.
“Msiuze kiholela maeneo yenu kwani baadhi ya watu wanauza maeneo kwa bei ndogo lakini watakao nunua watakuja kuuza kwa bei kubwa hivyo huu ni moja ya miji itakayokuwa ya kisasa hapa nchini na sasa maisha bora yanakuja na sitawaangusha naomba mnipigie kura nyingi za kutosha ili niweze kuwa Rais,” alisema Dk Magufuli.
Alisema kuwa kuhusu changamoto ya maji kwenye mji huo alisema kuwa atahakikisha suala hilo linakwisha ambapo aliipongeza awamu ya tatu na nne ambazo zimejitahidi angalau maji yanapatikana kwani mji huo ulikuwa na tatizo kubwa la maji.
Katika hatua nyingine amesema anashangazwa na baadhi ya wanasiasa kusema kuwa fedha zilizokuwa zijenge bandari ya Tanga zimepelekwa Bagamoyo kisa ni wilaya anayotoka Rais Dk Jakaya Kikwete.
“Kauli kama hizo ni za uchonganishi kwani kila eneo limetengewa fedha zake kwa ajili ya ujenzi wa Bandari kuanzia Tanga, Mtwara na Mwanza kote kutajengwa bandari hizo na Bagamoyo ni uwekezaji wa watu binafsi hivyo hakuna sababu ya kuwachonganisha watu kwa maneno ya uongo,” alisema Dk Magufuli.
Alibainisha kuwa hizo ni hoja hafifu na hazina msingi wowote zaidi ya kuleta uchonganishi kwani wanapaswa kutangaza sera zao na si kuongopa hali ambayo inajenga chuki baina ya wananchi wa eneo fulani na eneo jingine.
Alisisitiza kuwa endapo atapata ridhaa ya kuongoza atahakikisha ushuru mdogomdogo unaondolewa ili kuwaondolea kero wananchi ambao wanataka kujiongezea kipato kutokana na shughuli zao za ujasiriamali.
Kwa upande wake mgombea Ubunge wa Jimbo hilo la Chalinze Ridhiwani Kikwete alimshukuru Dk Magufuli kwa mipango hiyo na kusema kuwa changamoto iliyopo ni ujenzi wa kituo cha afya kikub wa ili kukabiliana na uwingi wa wagonjwa pamoja na majeruhi kwenye kituo cha afya chya Chalinze.
Ridhiwani alisema kuwa changamoto nyingine ni maji ambayo licha ya kupatikana bado kuna baadhi ya maeneo hayapati maji hasa kwenye makmao makuu ya vitongoji ambapo kwa makao makuu ya vijiji yote yanapata maji kwa asilimia 94 ambapo Dk Magufuli alisema atashughulikia changamoto hizo endapo atachaguliwa kuwa Rais.
Mwisho   

 Mgombea Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dk John Magufuli kulia na mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze wilayani Bagtamoyo mkoani Pwani Ridhiwani Kikwete wakiteta jambo wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo mchana kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze


 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete kushoto katikati ni mwenyekiti wa CCM mkoa Mwinshehe Mlao na kulia ni mwenyekiti wa CCM wilaya ya bagamoyo Almasa Maskuzi wakijadili wakati wakimsubiri mgombea Urais wa CCM Dk John Magufuli kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze.

 Mgombea Ubunge Jimbo la Chalinze CCM Ridhiwani Kikwete kulia akisalimiana na moja ya wanachama waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni wa Dk John Magufuli kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Ridhiwani Kikwete akisalimiana na mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM Josia Jackson 

Add caption



 Wagombea Ubunge kupitia CCM Ridhiwani Kikwete Jimbo la Chalinze kulia na Amoud Jumaa Jimbo la Kibaha Vijijini wakifurahi kwenye mkutano wa kampeni wa mgombea Urais kupitia chama hicho Dk John Magufuli. 

 Ridhiwani Kikwete na Dk John Magufuli wakiteta kabla ya kuanza mkutano wa kampeni uliofanyika uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Ridhiwani Kikwete katikati akiteta jambo na mgombea Urais CCM Dk John Magufuli kushoto ni Amoud Jumaa mgombea ubunge Jimbo la Kibaha Vijijini

 Dk Magufuli katikati wakitetea na Ridhiwani Kikwete kushoto na mjumbe wa kampeni Taifa CCM Abdala Bulembo 

 Abdala Bulembo akiwaonyesha wananchi wa Chalinze hawapo pichani namna ya kuwapigia kura wagombea wa CCM ngazi ya Urais

 Ridhiwnai Kikwete akizungumza kwenye mkutano huo wa kampeni

 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli akiongea

 Baadhi ya wagombea udiwani wa CCM kwenye Majimbo ya Chalinze na Bagamoyo wakitambulishwa kwenye mkutano huo wa kampeni

 Dk John Magufuli akifurahi jambo na Ridhiwani Kikwete wakifurahia jambo wakati wa mkutano wa kampeni 

 Baadhi ya wanachama wa CCM wakiwa wamejazana kwenye uwanja wa  Miembe Saba Chalinze kumsikiliza mgombea Urais wa chama hicho Dk John Magufuli

 Sehemu ya umati wa wanachama na wananchi wa Chalinze wakiwa wanawasikiliza wagombea mbalimbali wa CCM 

 Wanachama wa CCM wakiwa wamefurika uwanja wa Miembe Saba Chalinze

 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk John Magufuli kulia na Ridhiwani Kikwete kushoto wakiombewa duwa mara baada ya mkutano wa kampeni kwenye uwanja wa Miembe Saba Chalinze

No comments:

Post a Comment