Monday, October 19, 2015

WAFUGAJI WALIOINGIA KINYEMELA BAGAMOYO KUONDOLEWA


Na John Gagarini, Chalinze

 

WILAYA ya Bagamoyo imesema kuwa itawaondoa wafugaji wote walioingia kinyemela kwenye wilaya hiyo ili kuepusha migogoro ya wakulima na wafugaji.

 

Hayo yalisemwa na mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Hemed Mwanga, wakati akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kihangaiko wilayani humo.

 

Mwanga alisema kuwa kuna baadhi ya wafugaji wameingia kinyemela kwenye wilaya hiyo jambo ambalo ni kinyume cha taratibu.

 

“Tuna taarifa tunazo kuwa kuna baadhi ya wafugaji wanaingia kinyume cha taratibu hali ambayo inaweza kusababisha vurugu baina ya wakulima na wafugaji,” alisema Mwanga.

 

Alisema kuwa wafugaji wote walioingia kwa njia za panya wataondolewa kwani kila mahali kuna taratibu zake na kama walikuwa wanataka kuingia walipaswa kufuata taratibu.

 

“Wafugaji walioingia kinyume cha utaratibu wataondolewa na tumepata taarifa kuwa baadhi ya mgambo wamekuwa wakihusika kuwaingiza wafugaji hao kinyume cha utaratibu pale Mto Wami,” alisema Mwanga.

 

Aidha alisema kuwa wale wote wanaohusika kuwaingiza wafugaji hao kinyume cha utaratibu watashughulikiwa kwani wanataka kutoletea matatizo.

 

Mwisho.

No comments:

Post a Comment