Na Mwandishi
Wetu, Kibaha
WATU
wanne wanaodhaniwa kuwa ni majambazi wanatuhumiwa kumwua mtu mmoja mwenye umri
kati ya miaka (35) na (40) ambaye jina lake halikuweza kufahamika na kumjeruhi
mwingine baada ya kufanya tukio la uhalifu kwenye maduka yaliyopo kwenye stendi
ya Maili Moja wilayani Kibaha mkoani Pwani jirani na kituo cha polisi.
Kutokana
na tukio hilo Jeshi la polisi Mkoani Pwani linawatafuta watu hao ambao walikuwa
na bunduki hao ambao walivamia duka liitwalo Bahati mali ya Hashim Kisaka na
ofisi ya kukatia tiketi ya mabasi yaendayo mikoani kisha kupora fedha kwenye
maduka hayo.
Akithibitisha
kutokea kwa tukio hilo kaimu kamanda wa polisi mkoani
humo Athumani Mwambalasa alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 2 kasoro usiku Septemba 20 mwaka huu.
humo Athumani Mwambalasa alisema kuwa tukio hilo lilitokea majira ya saa 2 kasoro usiku Septemba 20 mwaka huu.
“Watu
hao walivamia katika maeneo hayo wakiwa na silaha ambayo bado haijafahamika na
kumuua mtu huyo kwa kumpiga na risasi ya kifuani kisha kumjeruhi mguuni mfanyabishara wa korosho Ambwene Mwambungu wakati
wa tukio hilo ambalo lilifanyika huku umeme ukiwa umekatika na hali iliyofanya kukawa
na giza nene na watu hao kutumia mwanya huo kutekeleza tukio hilo,” alisema
Kamanda Mwambalaswa.
Kamanda
Mwambalasa alielezea kuwa kwenye tukio hilo watu hao wakiwa na silaha hiyo walivamia
katika maduka hayo na kuanza
kupiga risasi hewani hali iliyowafanya watu waliokuwa katika eneo hilo kukimbia hovyo huku wakiacha mali zao kuhofia usalama wao kisha kupora fedha na mali ambayo thamani yake bado haijafahamika.
“Marehemu alifikwa na mauti wakati akipelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Pwani ya Tumbi huku majeruhi wa tukio hilo bado amelazwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha ya mguu aliyoyapata,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
kupiga risasi hewani hali iliyowafanya watu waliokuwa katika eneo hilo kukimbia hovyo huku wakiacha mali zao kuhofia usalama wao kisha kupora fedha na mali ambayo thamani yake bado haijafahamika.
“Marehemu alifikwa na mauti wakati akipelekwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Pwani ya Tumbi huku majeruhi wa tukio hilo bado amelazwa akipatiwa matibabu kutokana na majeraha ya mguu aliyoyapata,” alisema Kamanda Mwambalaswa.
Aliwataka
wananchi kushirikiana kwa pamoja kutoa taarifa mara moja watakapobaini walipo
watu hao pia kutoa taarifa mara wanapohisi watu wasioeleweka katika
maeneo yao.
Mwisho
Mwisho
No comments:
Post a Comment