Monday, May 26, 2014

MATUKIO PWANI





  










 Na John Gagarini, Kibaha

WATU wawili wamefariki dunia na wengine wanne wamejeruhiwa baada ya magari waliyokuwa wakisafiria kugongana huko eneo la Bwawani kata ya Ubena Tarafa ya Chalinze wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 25 mwaka huu majira ya saa 10:30 jioni katika barabara kuu ya Dar es Salaam – Morogoro.

Kamanda Matei alisema kuwa ajali hiyo ilihusisha gari T 752 ADE aina ya Toyota Landcruiser likiendeshwa na Anthony Paul (47) raia wa Uingereza ambaye ni mkazi wa Rock Garden mkoani Morogoro akitokea Dar es Salaam kwenda Morogoro aligongana uso kwa uso na gari namba T 404 CSN aina Forester lililokuwa likiendeshwa na Hizza Semkubo na kusababisha vifo hivyo.

Aliwataja waliokufa kuwa  dereva Semkubo na abiria aitwaye Odino Haule (45) na majeruhi wanne amao ni Happy Michael (21), Jamila Jaffary (21) ambao ni wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM) Dar es Salaam.

Aidha aliwataja majeruhi wengine kuwa ni Joseph Mapunda (30) mkazi wa Iringa ambaye amelazwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dar es Salaam kutokana na hali yake kuwa mbaya.

Kamanda Matei alisema kuwa dereva Paul na majeruhi wengine wawili walikimbizwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro kwa matibabu, Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa gari namba T 404 CSN kuyapita magari mengine bila ya kuchukua tahadhari na miili ya maerehemu imehifadhiwa katika hospitali Teule ya Tumbi.

Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha

WATU 10 wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Pwani kwa tuhuma mbalimbali za uhalifu wakiwemo wanawake watatu waliopatikana na bangi kilogramu 2 ikiwa kwenye mfuko wa plastiki maarufu kama Rambo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Kibaha kamanda wa polisi mkoani humo Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACP) Ulrich Matei amesema kuwa watuhumniwa hao walikamatwa Mei 19 mwaka huu 19 majira ya saa 09:00 alasiri huko Mkuranga Kata/Tarafa ya Mkuranga Wilaya ya Mkuranga.

Kamanda Matei alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa na  askari waliokuwa doria,  watuhumiwa hao ni Ummy  Mkwachu (32) mkazi wa Mbagala Charambe, Amina Said (23), mkazi wa Mbagala Kiburugwa na Sarah Daud (19), mkazi wa Mbagala Charambe wakiwa na Bhangi yenye uzito wa kg 2 ikiwa imefungwa kwenye mfuko wa nailoni (Rambo), wakisafirisha katika gari lenye namba za usajili T117 BKN aina ya Toyota Hiace wakitokea Dar es Salaam kwenda Kisiju wilayani Rufiji.


Kamanda Matei alisema kuwa kwenye tukio lingine Salum Rashid (43) mkazi wa Ubena Zomozi anashikiliwa kwa tuhuma ya kupatikana na silaha aina ya Gobore bila ya Kibali.

Alibainisha kuwa tukio hilo lilitokea Mei 23 mwaka huu majira ya saa 05:41 asubuhi huko Kijiji cha Ubena kata ya Ubena Tarafa ya Chalinze Wilaya ya Bagamoyo, ambapo askari wakiwa doria walimkamata mtuhumiwa huku sila hiyo ikiwa na risasi moja.

 Katika tukio lingine watu watatu wanshikiliwa na jeshi hilo kwa tuhuma za kupatikana na Madawa ya kulevya aina ya Mirungi bunda 33 wakiwa ndani ya Basi la kampuni ya Tawfiq lenye namba za usajili T 248 KBT likitoka Tanga Kwenda Jijini Dar es Salaam.

Alisema kuwa watuhumiwa hao walikamatwa Mei 24mwaka huu majira ya saa 08:15 mchana huko kijiji cha Msoga kata/Tarafa ya Msoga Wilaya ya Bagamoyo.

Watuhumiwa hao walikamatwa na askari waliokuwa doria, ambapo waliwakamata walimkamata Hafidh Siraji, ( 22), mkazi wa Tanga, akiwa na Mirungi bunda 33 sawa na kg 33 ndani ya gari lenye namba za usajili T 248 KBT aina ya Isuzu Bus.

Katika hatua nyingen jeshi hilo linawashikilia watu watatu kwa tuhuma za kuvua samaki kwa njia haramu ya nyavu ambazo zimepigwa marufuku na serikali.

Alisema kuwa tukio hilo limetokea Mei 25 mwaka huu majira ya saa 1:30 asubuhi huko maeneo ya Bondeni Pwani Kata ya Kilindoni Tarafa ya kusini Wilaya ya mafia

Alifafanua kuwa askari wakiwa doria waliwakamata Ussi Juma, (50), mkazi wa Msufini, Ahmad Saleh,(22), mkazi wa Msufini na Ahmad Bakari,(27), mkazi wa Kichangachui wakivua samaki kwa kutumia nyavu haramu.


MWISHO.


No comments:

Post a Comment