Saturday, May 31, 2014

BILALI AZINDUA MFUKO WA ELIMU ACHANGIA MILIONI 10



Na John Gagarini, Kibaha
MAKAMU wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk Mohamed Gharib Bilali ameuchangia mfuko wa elimu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani kiasi cha shilingi milioni 10.
Alichangia fedha hizo jana wakati wa uzinduzi wa mfuko wa elimu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha uliofanyika kwenye uwanja wa Bwawani Maili Moja wilayani hapa.
Alisema kuwa katika kufikia malengo ya Matokeo Makubwa Sasa (BRN) kwenye sekta ya elimu lazima kuwe mikakati maalumu ya kuweza kufikia malengo kwa kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye sekta hiyo.
“Nawapongeza kwa kuanzisha mfuko huu na serikali itawaunga mkono kwa hali na mali na mimi nawachangia milioni 10 kwa ajili ya kukabiliana na changamoto kwenye sekta ya elimu katika mji wa Kibaha wilaya na mkoa mzima wa Pwani.
“Ningependa suala la choo kuwa historia kwani hii ni aibu na si changamoto ya kudumu na inapaswa kufanyiwa kazi mara moja na kuiondoa kabisa kwani ni jambo lisilo pendeza na changamoto nyingine zilizopo kama vile za upungufu wa madawati kwa shule za msingi, ukosefu wa maabara kwa shule za sekondari, upungufu wa nyumba za walimu, matundu ya vyoo, vyumba vya madarasa na maktaba kupitia mfuko huo utasaidia kukabiliana na hali hiyo,” alisema Dk Bilali.
Aidha alisema kuwa amefurahi kusikia kuwa fedha hizo zitatumika kujenga maabara tatu katika sekondari za Pangani, Visiga na Miembe Saba na kununua madawati 1,500 kwa ajili ya shule za msingi za Tandau, Lulanzi, Misugusugu, Zogowale, Msangani, Viziwaziwa, Vikawe, Mwanalugali, Mkuza na Kidimu.
Alizitaka halmahauri hapa nchini kuiga mfano wa Halmashauri hiyo ya Mji wa Kibaha kwa kuanzisha mifuko kama hii kwa ajili ya kutatua changamoto za elimu badala ya kuisubiri serikali kwani ni mgao inaoutoa ni mdogo na elimu na mafunzo bora ni mkakati wa kipaumbele katika kufikia malengo ya mipango ya maendeleo ya Taifa ya 2025 na kutumia Mkakati wa Kukuza Uchumi na Kupunguza umaskini MKUKUTA na malengo ya milenia.
Awali Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Kasimu Majaliwa alisema kuwa ubunifu wa kupata fedha kwa ajili ya Halmashauri 167 hapa nchini ni mzuri kwnai utasaidia kukabiliana na changamoto zilizopo kwenye sekta ya elimu.
Majaliwa alisema kuwa uboreshaji wa elimu unapaswa kusimamiwa na watu wote wakiongozwa na madiwani na wananchi wote wanapaswa kujitokeza kuuchangia na wizara yake itachangia kiasi cha shilingi milioni tano.
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Kibaha Mjini Silvestry Koka alisema kuwa amefurahishwa na uzinduzi huo ambapo alisema kuwa moja ya ndoto zake za kukabiliana na changamoto za elimu.
“Ili kuwa na elimu bora ni pamoja na kuwa na miundombinu mizuri na watu wa kuiboresha ni wazazi pamoja na wadau wote ndani ya Halmashauri licha ya kuwa wananchi wanachangamoto kubwa ya kuchangia hata hivyo wameonyesha nia ya kuchangia kwa kujitolea na mimi nawaunga mkono kwa kutoa kiasi cha shilingi milioni 16,” alisema Koka.
Awali mwenyekiti wa mfuko huo Anna Bayi alisema kuwa lengo la kuanzishwa mfuko huo ni kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia ambapo hadi sasa mfuko huo una kiasi cha shilingi milioni 210 na ahadi ni shilingi milioni 34 huku malengo yakiwa ni kukusanya kiasi cha shilingi milioni 300.
“Tunatarajia kati ya fedha hizo zitajenga maabara tatu katika shule ya sekondari Nyumbu, Miembe Saba na shule ya wasichana Kibaha ambapo tumejiwekea mikakati mbalimbali ikiwa ni pamoja na kujiunga na mfuko wa elimu nchini kwa lengo la kupata ruzuku ya miundombinu, samani, vifaa vya kufundishia na kujifunzia,” alisema Bayi.
Mwisho. 

   

Thursday, May 29, 2014

BILALI KUZINDUA MFUKO WA ELIMU KIBAHA MEI 31



Na John Gagarini, Kibaha
MFUKO wa elimu wa Halmashauri ya Mji wa Kibaha mkoani Pwani utazinduliwa Mei 31 mwaka huu ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Gharib Bilali.
Kwenye uzinduzi huo ambao utafanyika mjini Kibaha mgeni rasmi ataongoza matembezi ya hisani kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji wa mfuko huo ambao una lengo la kupata kiasi cha shilingi milioni 300.
Akielezea juu ya tukio hilo mwenyekiti wa mfuko huo Anna Bayi alisema kuwa  katika uzinduzi huo kutatanguliwa na matembezi ya hisani yatakayoanzia maeneo ya Mkoani hadi viwanja vya Maili Moja ambapo ndipo halfa itafanyika.
Bayi alisema kuwa  hadi sasa tayari wameshapata kiasi cha shilingi milioni 180 zitakazosaidia kuiwezesha halmashauri hiyo kukabiliana na changamoto za sekta ya elimu hususan madawati na maabara.
"Mara zitakapopatikana fedha hizo tutaanzia kununulia madawati 1,500 yenye thamani ya shilingi milioni 90 na kujenga maabara tatu kwa shilingi Milion 210,” alisema Bayi.
Alisema uchangiaji huo utakuwa ni zoezi endelevu ili kuhakikisha wanapunguza ama kumaliza kabisa changamoto za kielimu katika halmashauri ya Mji wa Kibaha.
“Kila mwananchi anatakiwa kuchangia kiasi cha shilingi 2,000 wakiwemo  ,wafanyabiashara, wamiliki wa makampuni na wadau wa elimu na hadi sasa mwamko unaonekana kwa wananchi hivyo kuwa na imani ya kuwa mfuko utafanikiwa,” alisema Bayi.
Kwa upande wake  Mkurugenzi wa Halmshauri hiyo, Jeniffer Omolo alisema mfuko huo umeundwa chini ya sheria namba 288 kifungu kidogo namba 80 katika tangazo la serikali namba 218 la tarehe 18 Juni 2010.
“Shule za msingi na sekondari za serikali bado zinakabiliwa na changamoto mbalimbali ambazo zinafanya lengo la utoaji elimu bora kushindwa kufikiwa kikamilifu,” alisema Omolo.
Alibainisha kuwa Shule za msingi zilizopo wilayani Kibaha Mji  zinakabiliwa na uhaba wa madawati 3,488 hali inayopelekea baadhi ya shule hizo wanafunzi kutumia kukaa zaidi ya watatu kwenye dawati moja.
Aidha alisema katika upande wa shule za sekondari kuna upungufu wa maabara 24 ambapo kwa sasa kuna maabara 9 pekee, Halmashauri ya mji wa Kibaha ina jumla ya shule za msingi 47 na shule za sekondari za serikali na binafsi 34 .
Mwisho.

HOUSE GIRL ATUPA KICHANGA ADAKWA



Na John Gagarini, Kibaha
MSICHANA Theresia Matai (19) ambaye ni mfanyakazi wa ndani mkazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani anashaikiliwa na Jeshi la polisi mkoani humo kwa tuhuma za kumtupa mtoto wake aliyejifungua.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 27 mwaka huu majira ya saa 3 usiku.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea eneo la Mwembe tayari nyuma ya nyumba ya Dalaida Samwel (54) ambaye ni bosi wake ambapo alikuwa akifanya kazi za ndani.
“Baada ya kufanya tukio hilo alirudi ndani na kulala na aliweza kufahamika baada ya wasiri kutoa taarifa kuwa mtuhumiwa alionekana kuwa na mimba na baada ya kujifungua alimwacha mtoto huyo nyuma ya nyumba hiyo,” alisema Kamanda Matei.
Alibainisha kuwa jirani yake na mwenye nyumba Filbert Sekeleno (31) alipata taarifa kutoka kwa jirani mwenzake aliyefahamika kwa jina la Mama Frank kuwa kuna sauti ya mtoto nyuma ya nyumba alipokutwa mtoto huyo.
“Majirani waliongozana hadi kwenye eneo la tukio na kumkuta mtoto mchanga wa kiume akiwa ametelekezwa na kutoa taarifa polisi ambao walianza uchunguzi juu ya tukio hilo,” alisema Kamanda Matei.  
Aidha alisema kuwa mtuhumiwa alipelekwa hospitali ya Tumbi kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi na daktari kujua chanzo kilichosababisha kufanya tukio hilo ambapo mtoto huyo anaendelea vizuri.
Mwisho.




Wednesday, May 28, 2014

HOUSE GIRL ATUPA KICHANGA AKAMATWA NA POLISI



Na John Gagarini, Kibaha
MSICHANA Theresia Matai (19) ambaye ni mfanyakazi wa ndani mkazi wa Kwa Mathias wilayani Kibaha mkoani Pwani anashaikiliwa na Jeshi la polisi mkoani humo kwa tuhuma za kumtupa mtoto wake aliyejifungua.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa Polisi mkoani Pwani Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Ulrich Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 27 mwaka huu majira ya saa 3 usiku.
Kamanda Matei alisema kuwa tukio hilo lilitokea eneo la Mwembe tayari nyuma ya nyumba ya Dalaida Samwel (54) ambaye ni bosi wake ambapo alikuwa akifanya kazi za ndani.
“Baada ya kufanya tukio hilo alirudi ndani na kulala na aliweza kufahamika baada ya wasiri kutoa taarifa kuwa mtuhumiwa alionekana kuwa na mimba na baada ya kujifungua alimwacha mtoto huyo nyuma ya nyumba hiyo,” alisema Kamanda Matei.
Alibainisha kuwa jirani yake na mwenye nyumba Filbert Sekeleno (31) alipata taarifa kutoka kwa jirani mwenzake aliyefahamika kwa jina la Mama Frank kuwa kuna sauti ya mtoto nyuma ya nyumba alipokutwa mtoto huyo.
“Majirani waliongozana hadi kwenye eneo la tukio na kumkuta mtoto mchanga wa kiume akiwa ametelekezwa na kutoa taarifa polisi ambao walianza uchunguzi juu ya tukio hilo,” alisema Kamanda Matei.  
Aidha alisema kuwa mtuhumiwa alipelekwa hospitali ya Tumbi kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi zaidi na daktari kujua chanzo kilichosababisha kufanya tukio hilo ambapo mtoto huyo anaendelea vizuri.
Mwisho.