Sunday, September 8, 2013

MWANAFUNZI ABAKWA NA WENZAKE

Na John Gagarini, Kibaha
MATUKIO ya uvunjifu wa maadili kwenye shule mbalimbali hap nchini yameendelea kuharibika baada ya wanafunzi wanne wa shule ya Msingi Lulanzi wilayani Kibaha mkoani Pwani kutuhumiwa kubaka mwanafunzi wa darasa la pili (9) na kumsababishia maumivu yalipelekea kulazwa hospitali ya Tumbi kwa matibabu.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana babu wa mtoto huyo (jina tunalo), Jacob Mrope alisema tukio hilo lilitokea Septemba 2 majira ya saa 6 mchana,  ambapo mjukuu wake ambaye ni yatima, alikuwa akitoka shuleni huku akiwa na wenzake wawili wakike walikimbizwa na watuhumiwa hao ambapo yeye alishindwa kukimbia kutokana na kuuumia mguu na kujikuta akikumbana na dhahma hiyo.
Mrope alisema kuwa wanafunzi wenzake aliokuwa nao walisema kuwa baada ya watuhumiwa hao kumkamata walimziba mdomo kisha wakaanza kumuingilia kwa zamu ambapo mwanafunzi huyo hakuweza kupata msaada wowote hadi watuhumiwa hao kutimiza haja zao.
“Wenzake waliokuwa nao walitoa taarifa nyumbani kwa mlezi wake ambaye ni dada yake ambapo alikwenda na kumkuta akitokwa na damu nyingi na alipomuuliza alisema kuwa wenzake wamembaka na kumchukua na kumpeleka shuleni na kutoa taarifa,” alisema Mrope.
Kwa upande wake dada yake Lwiza alisema kuwa yeye alipata taarifa kupitia kwa wanafunzi hao ambao walikuwa nao wakati wanatoka shule na kukimbizwa na watuhumiwa hao, ambapo walisema kuwa ilibidi warudi na kumkuta mwenzao akitokwa damu na kumkokota mwenzao hadi nyumba iliyojirani na kumjulisha.
“Alikuwa kwenye hali mbaya kwani alikuwa akitokwa na damu nyingi na nilipomuuliza alisema kuwa amebakwa na mtuhumiwa ambaye alimtambua na kumtaja jina mwenye umri wa miaka 10 akiwa na wenzake watatu,” alisema Lwiza.
Lwiza alisema kuwa baada ya kuona hali ile walimpeleka shule na uongozi wa shule ukamwelekeza kufuata taratibu za kisheria ambapo walikwenda serikali ya mtaa kasha kwenda polisi na baadaye hospitali ya Tumbi kwa matibabu zaidi ambapo hadi juzi mwanafunzi huyo alikuwa bado kalazwa na hali yake inasemekena kuwa ni mbaya.
Naye mwalimu mkuu wa shule hiyo ya Lulanzi Anna Bilali alisema kuwa wao kama uongozi wa shule hawawezi kusema lolote kwani sula hilo liko kwenye vyombo vya sheria pamoja na kitabibu na watakuwa tayari kusema mara taarifa zitakapokamilika.
“Ni kweli tukio hili limetokea lakini bado haijathibitishwa kama ni kweli au la na pia lilitokea nje ya shule na muda wa shule kwa wanafunzi wa madarasa ya chini walisharuhusiwa kurudi nyumbani mara baada ya masomo kwisha,” alisema Bilali.
Akizungumzia tukio hilo mjumbe wa mtaa wa Lulanzi Rasul Shaban alisema kuwa walipata taarifa hiyo na kushnagazwa na kitendo hicho ambapo tukio hilo ni la mara ya kwanza kutokea katika shule hiyo ambayo iko kwenye mtaa huo na pia walitoa barua za kuwadhamini wanafunzi wanaotuhumiwa kufanya tukio hilo.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa polisi mkoani Pwani Ulrich Matei alisema kuwa hadi sasa wanawashikilia wanafunzi wanne wenye umri kati ya miaka 10 na 13 kuhusiana na tukio hilo.
“Wanafunzi hao wanatuhumiwa kumbaka mwenzao wakati akitoka shule ambapo walimkamata na kumkimbiza kwenye kichaka na kumziba mdomo ili asiweze kupiga kelele kisha walimshika miguu na mikono na kumbaka kwa zamu  na kumsababishia maumivu makali ambapo amelazwa hospitali ya Tumbi kwa matibabu zaidi na hali yake bado haijawa nzuri,” alisema Matei.
Matei alisema kuwa watuhumiwa hao wanne wanahojiwa juu ya tukio hilo ambapo watafikishwa mahakamani mara upelelezi utakapokamilika ikiwa ni pamoja na uchunguzi wa daktari kuhusina na tukio hilo lakusikitisha.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment