Na John Gagarini, Kibaha
KIJANA aitwaye Ibrahimu Jumapili (30)mkazi wa Kongowe
wilayani Kibaha mkoani Pwani amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia kanga kwenye
mti wa mkorosho.
Kwa mujibu wa mwenyekiti wa mtaa wa Bamba wilayani Kibaha
Amry Mavala alisema kuwa marehemu hakuweza kuacha ujumbe wowote wa sababu ya
kuchukua maamuzi hayo ya kujiua.
Mavala alisema kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 17 mwaka
huu majira ya saa 6:30 mchana kwenye mtaa wa Bamba kata ya Kongowe wilayani
humo.
“Marehemu alikuwa akijishughulisha na kazi ya ufayatuaji
matofali na kabla ya kifo chake alikuwa akilalamika kuwa kuna watu walikuwa
wakitaka kumtoa kafara,” alisema Mavala.
Alisema kuwa kutokana na hali hiyo marehemu alisema kuwa
anamwachia Mungu na itambidi arudi nyumbani kwao mkoani Singida ili ajinusuru
na hali hiyo.
Kwa upande wake kaimu kamanda wa polisi mkoani Pwani Juma Ali
alisema kuwa mwili wa marehemu ulikutwa ukininginia kwenye mkorosho kwenye
shamba la Mzee Rafael.
Ali alisema kuwa chanzo cha kifo chake hakijaweza kufahamika
na mwili wa marehemu uko kwenye hospitali ya Tumbi kwa ajili ya uchunguzi wa
daktari na taratibu za mazishi.
Wakati huo huo mwili wa mtu asiyefahamika umeokwotwa huko
kwenye mtaa wa Kwa Mathiasi wilayani Kibaha ukiwa umeharibika vibaya ambapo
ulikutwa na jeraha shingoni na mtu mmoja anashikiliwa kuhusiana na tukio hilo,
na mwili huo ulizikwa hapo hapo baada ya kushindwa kuhamishwa.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WATU sita wanashikiliwa
na jeshi la polisi mkoani Pwani wakiwemo wawili wanaodai kuwa ni askari polisi kwa
tuhuma za kukutwa na nguo zinazosadikiwa kuwa ni za magendo kutokea nchini
Kenya.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana kaimu
kamanda wa polisi mkoani humo Juma Ali alisema kuwa watuhumiwa walikamatwa na
gari lililokuwa limebeba nguo za kike na kiume.
Ali alisema kuwa tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 9
alfajiri eneo la Vigwaza wilayani Bagamoyo kwenye kizuizi wakati askari wakiwa
doria kwenye barabara ya Dar es Salaam Chalinze.
Alisema kuwa watuhumiwa wawili ambao ndiyo walikuwa kwenye
gari aina ya Fuso lenye namba za usajili T 303 BAY lenye mzigo huo lilikuwa likiendeshwa
na Omary Salehe (66) mkazi wa Arusha na utingo Fuwad Salimu (46) mkazi wa Moshi.
“Wakati gari hiyo ikiwa inaendelea na safari yake ilikuwa
ikifukuzwa kwa kasi ilipofika Mbwewe na gari nyingine aina ya NOAH yenye namba
za usajili T 641 CCH ikiwa na watu wanne wakiwemo watu hao wawili ambao bado
hawajathibitishwa kama ni polisi kutokea mkoani Tanga au la huku mwingine akiwa
askari mstaafu na mtu mwingine,” alisema Ali.
Aidha alisema kuwa wanaendelea na uchunguzi juu ya kujua
thamani ya mzigo huo na kuwatambua watu hao kama ni askari kweli au la ili
hatua sahihi ziweze kuchukuliwa ambapo magari hayo bado yanashikiliwa na
watuhumiwa wanahojiwa kupata ukweli.
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
MTU mmoja mkazi wa Kongowe Joseph John (17) anashikiliwa na
jeshi la polisi kwa tuhuma za kumlawiti mwanafunzi (jina tunalo).wa shule ya
Msingi Kongowe mwenye umri wa miaka 11.
Akizungumza na waandishi wa habari shangazi wa mtoto huyo
Rukia Bora alisema kuwa alimgundua mtoto huyo kuingiliwa baada ya kulalamika
kuwa anasikia maumivu shemu za haja kubwa.
Bora alisema kuwa alimgundua mtoto huyo wa mdogo wake wa
kiume kuingiliwa Septemba 12 mwaka huu.
Alisema kuwa baada ya kumhojia alimwelekeza alipokuwa
akifanyiwa mchezo huo kwa muda sasa ambapo ni karibu miezi mitatu iliyopita
tangu kuanza kufanyiwa hivyo na mtuhumiwa na watu wengine ambao walikimbia na bado
wanatafutwa.
“Huyu mtoto anaishi na bibi yake lakini kwa kuwa mimi na bibi
yake tuko jirani hapa Kongowe Kati wakati mwingine anakuja kwangu hivyo
tunamlea kwa pamoja ambapo baba yake yuko Jijini Dar es Salaam na mke we
waliasha achana lakini kutokana na tabia za mtoto za utundu udhibiti wake
ulikuwa mgumu,” alisema Bora.
Aidha alisema kuwa baada ya kumhoji alikataa kusema ikabidi
wampeleke polisi na baada ya kubanwa ilibidi aseme ukweli na kueleza kila kitu.
“Alisema kuwa chumba (Ghetto) alichokuwa akifanyiwa mchezo
huo wanaishi vijana watupu ambao wanajihusisha na uimbaji kwenye shghuli
mbalimbali za sherehe, ambapo walikuwa wakimwingilia kwa nyakati tofauti muda
wa usiku na kumwambia asiseme kwa mtu yoyote,” alisema Bora.
Alibainisha kuwa chanzo cha yeye kujua hilo ni baadhi ya
majirani kuona kuwa mtoto huyo kuwa karibu na mtuhumiwa hali ilyowatia shaka
majirani.
“Baada ya kugundua nilimfuata mtuhumiwa na kumkamata na
kumpeleka polisi hata hivyo watuhumiwa wengien wawili walikimbia ambapo jana
watoto wawili ambao nao walikuwa wakimfanyia hivyo walipelekwa polisi kuhojiwa
na kinachosubiriwa ni mtoto huyo kwenda kuwatambua,” alisema Bora.
Alisema kwa sasa mtoto huyo anaendelea kupatiwa matibabu
kwenye hospitali ya Tumbi.
Kwa upande wake kaimu
kamanda wa polisi mkoani Pwani Juma Ali alisema kuwa mbali ya mtuhumiwa huyo
watuhumiwa wengine walikimbia na wanaendelewa kutafutwa.
Ali alisema kwa sasa
kinachosubiriwa ni gwaride la utambulisho wa watuhumiwa wawili wadogo ambao ni
wanafunzi ili nao waunganishwe na mtuhumiwa wa kwanza.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment