Na John Gagarini, Kibaha
VIZIWI mkoani Pwani wamependekeza kwenye katiba ijayo iwe na
kipengele cha matumizi ya lugha ya alama kwenye maeneo ya umma ili kurahisisha
utoaji huduma kwa watu wote.
Hayo yalisemwa na katibu wa klabu ya Michezo ya Viziwi mkoani
Pwani (PDSC), Daud Kulangwa wakati akitoa ripoti ya utekelezaji wa mradi wa
kuwawezesha watu wenye ulemavu kujadili rasimu ya katiba mpya ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, baada ya baraza la katiba lililofanyika Mlandizi wilayani
Kibaha.
Kulangwa alisema kuwa kwa katiba iliyopo inasema tu kuweka
mazingira ya matumizi ya lugha ya alama ambayo utekelezaji wake kwani sehemu za
umma na sekta binafsi matumizi ya lugha
hiyo hayapo kwa sasa.
“Tunataka kwanza kuwe na mafunzo ya lugha ya alama na nukta
nundu kama ilivyo masomo mengine mashuleni na kwenye vyuo kwa watumishi wa umma
na kila raia wa Tanzania awe anaijua lugha hiyo ambapo wafanyakazi wa umma
wataweza kuwasiliana na watu wenye ulemavu kama wafanyavyo ndani ya ndege,”
alisema Kulangwa.
Alisema kuwa kwa sasa watu wenye ulemavu wakiwemo viziwi
wasioona wanapata tabu sana wanapokwenda kwenye sehemu za kupata huduma kama
vile mahakamani, polisi, hospitali, maofisini, mahali pa kuabudia na sehemu
nyingine hivyo kushindw akupata huduma stahili.
“Kama unavyojua ukienda sehemu za huduma unashindwa
kuhudumiwa kwani wahusika hawajui kumwelekeza mteja kwa usahihi kutokana na
mawasailiano kuwa magumu hivyo kushindwa kupata kile kinachostahili,” alisema
Kulangwa.
Aidha alisema kuwa kwenye kipengele cha lugha ya Taifa ni
Kiswahili pia kuwe na nyongeza ya lugha ya alama ili iwe kisheria na endapo mtu
atashindwa kutekeleza iwe ni kosa kisheria.
“Uwepo wa lugha ya alama na nukta nundu utasaidia mawasiliano
kwa watu wote hasa kwenye shughuli za serikali na watu watu wenye ulemavu
watapata taarifa kwani kwa sasa upatajia wa taarifa ni mdogo sana kutokana na
matumizi ya lugha ya alama kutopewa kipaumbele,” alisema Kulangwa.
Aliongeza kuwa juu ya haki za watu wenye ulemavu zitajwe na
aina, kuwezeshwa na serikali vifaa maalumu vya kujipatia elimu, vyombo vya usafiri,
kupata hifadhi ya jamii kwa watu wenye ulemavu na kuw ana chombo cha
kuwaunganisha na kuwatetea kuanzia ngazi ya kata hadi Taifa. Mabaraza hayo
yaliwashirikisha wajumbe zaidi ya 100 na yalifadhiliwa na The Foundation for
Civil Society (FCS).
Mwisho.
Na John Gagarini, Kibaha
WAKAZI 5,720 wa mtaa wa Mwanalugali wilayani Kibaha mkoani
Pwani watanufaika na mradi wa maji safi na salama ya bomba wenye thamani ya
shilingi milioni 210,768,135 baada ya mradi wa maji kwenye mtaa huo kukamilika
na kuanza kutoa maji.
Mradi huo ambao ulizinduliwa na kiongozi wa mbio za mwenge
hivi karibuni Juma Simai ulianza rasmi mwaka 2009 kwa kufanywa utafiti wa
upatikanaji wa huduma ya maji ya ardhini na kukamilika Januari mwaka huu.
Mwenyekiti wa kamati ya maji wa mtaa huo Godfrey Mwandenga
alisema kuwa mradi huo uliibuliwa na wakazi wa mtaa huo kupitia mpango
shirikishi na kuwa kipaumbele cha kwanza cha jamii.
“Tumepata kisima kirefu cha mita 110 chenye kutoa maji ujazo
wa lita 15,00 kwa saa na mradi huu utawawezesha wananchi wa mtaa wetu wa
Mwanalugali sawa na asilimia 64 watapata maji safi na salama karibu na maeneo
wanayoishi kama ilivyoainishwa kwenye sera ya maji ya Taifa ya mwaka 2002,”
alisema Mwandenga.
Alisema kuwa kati ya fedha zilizofanikisha mradi huo kiasi
cha shilingi milioni 207,168,135 ni fedha kutoka serikali kuu na shilingi
milioni 3,600,000 ni michango ya jamii.
“Mradi huu umepunguza adha kwa akinamama kufuata maji mbali
na makazi yao hivyo kutumia muda huo katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na
mradi huu unasimamiwa na uongozi wa jumuiya ya watumiaji maji wa mtaa wa
Mwanalugali.
Aidha alisema kuwa wanajumuiya hao huwajibika kukusanya mauzo
ya maji, kulipia matumizi ya umeme, kufanya usafi wa mazingira, kukarabati
pamoja na kupanua huduma kwa maeneo yasiyofikiwa na huduma hii.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment