Na John Gagarini, Kibaha
TIMU ya soka ya Mwanalugali imenyakua ubingwa wa Micho Cup
baada ya kuifunga timu ya Bamba zote za wilayani Kibaha mkoani Pwani kwa magoli
2-1.
Mchezo huo ilipigwa kwenye uwanja wa Kwa Mbonde wilayani
Kibaha ulikuwa mkali na wa kusisimua muda wote na kuwafanya mashabiki waliojazana
uwanjani hapo kushindwa kukaa kwenye viti vyao.
Washindi walianza kupata bao la kuongoza dakika ya nane ya
mchezo kupitia kwa Makida Makida baada ya gonga za hapa na pale na kuwainua
mashabiki wake.
Huku Bamba wakiwa hawajajiweka sawa walishtukia wakipachikwa
bao la pili kupitia kwa Laurence Mugia dakika ya 13, hata hivyo Bamba
walifanikiwa kupata bao la kufuta machozi dakika ya 44 ya mchezo.
Naye wandaaji wa mashindano hayo Athuman Shija alisema kuwa
jumla ya timu 14 zilishiriki mashindano hayo ambayo yalikuwa na lengo la
kuhamasisha michezo kwenye wilaya hiyo.
Kwa upande wake meneja wa kampuni ya 3 J’s ambao ndiyo
wadhamini wa mashindano hayo Samwel Mwegoha alisema kuwa wataendelea kudhamini
michezo ili vijana waweze kupata ajira kupitia michezo.
Kufuatia ushindi huo wa Mwanalugali washindi walipata zawadi
za jezi seti mbili, mipira miwili na mipira miwili, Bamba walipata mipira
miwili na fedha taslimu kiasi cha shilingi
150,000.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment