Na
John Gagarini, Kibaha
JESHI
la polisi nchini limeanza mradi wa majaribio wa matumizi ya kifaa cha kisasa
cha kuangalia mwenendo wa magari yanayokwenda mwendo kasi ili kupunguza ajali.
Akizungumza
na waandishi wa habari jana wakati wakifanya majaribio ya vifaa hivyo kwenye
barabara ya morogoro, kamanda wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Pwani
Nasoro Sisiwaya alisema kuwa vifaa hivyo vimeanza kufanya
majario mkoani humo kwa majaribio.
Sisiwaya
alisema kuwa vifaa hivyo ni vya kisasa kwani vitafungwa sehemu ya juu na
kuyaona magari tofauti na vile vya awali ambavyo hushikwa mkononi na vilikuwa
havina taarifa za kutosha hasa wakati wa kuthibitisha kosa .
“Kifaa
hichi kina uwezo wa kutoa taarifa za gari ambalo limeonekana kwenda kwa mwendo
kasi kwani kinauwezo wa kuonyesha kasi
ya gari, muda na namba za gari husika, tofauti na kile cha zamani ambacho
kinaonyesha mwendo kasi pekee ambapo dereva ana uwezo wa kukana kwani hakuna
ushahidi wa kutosha,” alisema Sisiwaya.
Naye
mwakilishi wa kikosi cha usalama barabarani nchini Notker Kilewa, alisema kuwa kifaa
hichi cha kisasa na kinauwezo wa kufungwa sehemu ambayo kitaona magari na
mienendo yao na
kulitambua gari lenye mwendo kasi kinyume cha sheria.
Kwa
upande wake mwakilishi wa kampuni ya TMT ya Afrika Kusini, hapa nchini Twaha
Ngambi ambayo inasambaza vifaa hivyo alisema kuwa kifaa hicho kitasaidia
kukabiliana na madereva wanaokwenda mwendo wa kasi pamoja na makosa mengine ya
barabarani.
Ngambi
alisema kuwa kifaa hicho kitakuwa na uwezo wa kuona umbali wa mita 200 toka
kilipofungwa hivyo itaondoa usumbufu wa kulisimamisha ghafla gari ambalo
linabainika kuwa kwenye mwendo wa kasi.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment