Na
John Gagarini, Bagamoyo
KATA
ya Miono wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani imetakiwa kutenga eneo kwa ajili ya
kufanya shughuli za watoto yatima na wale waishio kwenye mazingira magumu.
Akizungumza
jana kwenye kata hiyo wakati wa kuzindua mfuko wa kusaidia watoto yatima na
wale wanaoishi kwenye mazingira magumu Meya wa mji mdogo wa Bagamoyo Abdul
Sharifu alisema lazima viongozi wa vijiji wanapaswa kutenga maeneo kwa ajili ya
kundi hilo.
Sharifu
alisema kuwa kundi hilo limekuwa halitendewi
haki hasa zinapotokea fursa mbalimbali kutokana na baadhi ya viongozi kutoona
umuhimu wa watoto hao na kuwaona kama
hawastahili kwenye jamii.
“Watoto
yatima na wale waishio kwenye mazingira magumu ni sawa na watoto wengine na
wanastahili kuwekewa mazingira mazuri ili waweze kuishi na kupata huduma muhimu
za kijami hivyo ni vema mkawatengea eneo lao kwa ajili ya kufanyia shughuli
zao,” alisema Sharifu.
Alisema
kuwa katika eneo hilo
watakuwa wakilitumia kwa ajili ya mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusoma,
michezo, kujifunza ufundi na masuala mengine kwa ajili ya watoto.
“Mimi
mwenyewe nilikuwa yatima baada ya kufiwa na wazazi wangu ndiyo sababu nimeguswa
na jambo hili la kuanzisha mfuko kwa ajili ya kuwasaidia kwani najua taabu
wanazozipata na sisi ndiyo wa kuwasemea na kuwasaidia,” alisema Sharifu.
Kwa
upande wake moja ya watoto yatima Yusuph Ally alisema kuwa jambo alilolifanya
meya ni la kuigwa na viongozi wengine pamoja na jamii inayowazunguka.
Katika
uzinduzi huo Meya huyo alichangia kiasi cha shilingi 500,000 kwa ajili ya mfuko
huo na kuahidi kutoa shilingi milioni 2 mara ufunguaji wa akaunti
utakapokamilika, jumla ya watoto zaidi 200 walihudhuria.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment