Na
John Gagarini, Bagamoyo
WAKURUGENZI
wa Halmashauri za wilaya na Miji mkoani Pwani wametakiwa kuwashirikisha maofisa
tarafa kwenye vikao mbalimbali vya maendeleo kwani wao ni wasimamizi wa mambo
yote kwenye tarafa zao.
Hayo
yalisemwa mjini Bagamoyo na katibu tawala wa mkoa wa Pwani Beatha Swai, wakati
wa mafunzo ya kuwajengea uwezo maofisa tarafa wa mkoa huo.
Swai
alisema kuwa anawashangaa wakurugenzi wa halmashauri kutowatenga maofisa hao
ambao ni kiungo muhimu baina ya serikali na wananchi lakini wamekuwa wakiwekwa
pembeni na kuonekana kama hawastahili
kushiriki kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.
“Inashangaza
hata kwenye vikao vya uongozi juu ya maendeleo hawashirikishwi kama ilivyo kwa wataalamu wengine kwenye halmashauri hawa
nao wanapaswa kupewa kipaumbele katika michakato mbalimbali ya maendeleo,”
alisema Swai.
Alisema
kuwa tayari serikali ilishawapa waraka wakurugenzi hao kuwashirikisha kwenye
masuala yote yanayohusu utendaji kazi ili wafanye kazi kwa pamoja lakini bado
wanakaidi maagizo hayo.
“Tumeona
kuwa kwenye vikao vya uongozi juu ya maendeleo hawashirikishwi jambo ambalo ni
kinyume cha taratibu hivyo tutawachukulia hatua kali za kisheria wakurugenzi
wote ambao wanakiuka taratibu za kazi,” alisema Swai.
Aidha
alisema kuwa wakurugenzi hao wamekuwa na dhana kuwa maofisa tarafa hao
wanakwenda kwa ajili ya kupata posho jambo ambalo halina ukweli kwani kushiriki
kwenye vikao kama hivyo ni haki yao .
Awali
akifungua mafunzo hayo mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza alisema kuwa
baadhi ya maofisa tarafa wengine hawajui wajibu wao.
Mahiza
alisema kuwa maofisa tarafa hao wanapaswa kujua wajibu wao kwa kutimiza malengo
ambayo yanawekwa na halmashauri na wanapaswa kuwa na taarifa zote za shughuli
za maendeleo na changamoto ndani ya tarafa zao.
Mwisho.
mkuu wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza akizungumza na maofisa tarafa wa mkoa huo alipokuwa akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo kwenye ukumbi wa chuo cha uongozi cha ADEM Bgamaoyo mkoani Pwani |
No comments:
Post a Comment